Maria umeandika makala nzuri sana na mie nakubaliana na wewe kuwa hivyo ndivyo inatakiwa kuwa.
Ila ukweli ni kwamba kwa wenzetu kama USA au UK, Vyombo vya usalama huwa vinafuatilia vyanzo vya mapato vya hawa Wagombea ili isije ikatokea kanunuliwa na Matajiri wa nje. Tuliona UK wakila sahani moja na PM Tony Blair kuwa alipokea laki kadhaa kutoka kwa wale Wahindi Ndugu (Mittal Brothers), matajiri wakubwa duniani. Tuliona German, Chancellor Helmet Kohl akiondolewa madarakani kwa kosa la kupokea fedha kutoka kampuni la mafuta la Wafaransa ELF kwa aiili ya chama chake.
Tatizo kubwa lililopo kwetu Tanzania ni kuwa unakuta kiongozi wa upinzani anafedha chafu na hakuna anayeuliza kazitoa wapi huku kipato chake kikiwa duni sana. Hawa watu huwa wanarubiniwa na kuanza kusaka madaraka kwa nguvu kwenye chama. Na kwa sababu Waafrica tuna tamaa sana ya hela (ona Kenya walivyonunuliwa kwa urahisi na El-Shabaab) basi huwa tupo tayari kumkaribisha nyoka kwenye nyumba.
Tuseme leo hii Zitto Kabwe na kitila Mkumbo waingie na kuwa Mwenyekiti na Katibu wake na huku Mwigamba akiwa sijui mtu wa habari. Umoja wa vijana wa Chadema warudishwe Juliana Shonza na Mwipamba na Davidi Kafulila arudi na kuchukua sijui nafasi ya Mnyika (ninaamni wataweka watu wao), je Chadema atabaki nani? Si kitakuwa kama CUF au NCCR kwa kuitwa Mke mdogo wa CCM? Je Zitto kama Mwenyekiti wa upinzani, ataendelea kuwa na uhusiano mzuri na chama tawala? Huo utakuwa upinzani kweli au mtu na shoga yake?
Kwa hali ilivyo sasa, kitendo cha Zitto kuwa Mwenyekiti, ndiyo utakuwa mwisho wa Chadema. Labda siku CCM ikija kuwa chama cha upinzani, Zitto anaweza kuchukua hicho cheo na kuwa kiongozi mzuri, labda waje sasa Wachina wamnunue.