Marekani yaombwa kuiondolea Zimbabwe vikwazo

Marekani yaombwa kuiondolea Zimbabwe vikwazo

Unawalaumu wazungu wakati viongozi wetu ndio chanzo cha haya yote yanayotokea.

Mugabe aliwatimua wazungu akatuaminisha waafrika kuwa mashamba watapewa wananchi wakaida, kinyume na matarajio yale mashamba waliyopokonywa wazungu walipeana viongozi wa serikali na chama(Zanu pf) tu na kama hiyo haitoshi Grace Mugabe amehusika kwenye uporaji wa ardhi za wananchi zilizokuwa zinatumika kwenye kilimo. Mashamba yote waliyopeana hakuna alieyaendeleza ijapokuwa vifaa walikuwa navyo ila maarifa na utayari haukuwepo. Mugabe huyohuyo baada ya kufanya yote hayo bado akataka kumuachia nchi mke wake hadi jeshi lilipoingilia kati na kutolewa madarakani.

Al Bashir alikuwa dikteta aliewageuza aliewageuza wananchi wake kuwa wafungwa wa nje. Kaongoza muda mrefu nchi ikiwa na vikwazo na ilikuwa wazi asingweza kuiletea mabadiliko yoyote chanya, busara ilikuwa kuondoka lakini akawa muuaji wa wanaomkosoa.

Gadaffi alikuwa dikteta aliewasupport madikteta wenzake kama Iddi Amini, mminyaji wa haki na demokrasia nchini kwake(alikuwa anawaua wapinzani wake kwa kuwanyonga mbele ya halaiki bila kwenda mahakamani na wengine walipotea tu)lakini kuna mabadiliko kadhaa aliyaleta pia.

Hao wote walitolewa na wazungu kwa kwenda kinyume nao lakini pia wananchi wa hizo nchi waliwachoka pia sababu ya ubinafsi na roho mbaya zao.


Na Unaposema Afrika hatuhitaji kuvushwa stage na demokrasia ya Marekani unamaanisha nini hasa? changamoto ulizotaja hapo zinaweza kutatuliwa kwa njia gani?
Inasikitisha sana kuona kuna watu wanaupa kisogo ukweli mchungu kuhusu watawala wa Africa.
Et Mugabe nae ni shujaa!!! 😢😢
 
Unawalaumu wazungu wakati viongozi wetu ndio chanzo cha haya yote yanayotokea.

Mugabe aliwatimua wazungu akatuaminisha waafrika kuwa mashamba watapewa wananchi wakaida, kinyume na matarajio yale mashamba waliyopokonywa wazungu walipeana viongozi wa serikali na chama(Zanu pf) tu na kama hiyo haitoshi Grace Mugabe amehusika kwenye uporaji wa ardhi za wananchi zilizokuwa zinatumika kwenye kilimo. Mashamba yote waliyopeana hakuna alieyaendeleza ijapokuwa vifaa walikuwa navyo ila maarifa na utayari haukuwepo. Mugabe huyohuyo baada ya kufanya yote hayo bado akataka kumuachia nchi mke wake hadi jeshi lilipoingilia kati na kutolewa madarakani.

Al Bashir alikuwa dikteta aliewageuza aliewageuza wananchi wake kuwa wafungwa wa nje. Kaongoza muda mrefu nchi ikiwa na vikwazo na ilikuwa wazi asingweza kuiletea mabadiliko yoyote chanya, busara ilikuwa kuondoka lakini akawa muuaji wa wanaomkosoa.

Gadaffi alikuwa dikteta aliewasupport madikteta wenzake kama Iddi Amini, mminyaji wa haki na demokrasia nchini kwake(alikuwa anawaua wapinzani wake kwa kuwanyonga mbele ya halaiki bila kwenda mahakamani na wengine walipotea tu)lakini kuna mabadiliko kadhaa aliyaleta pia.

Hao wote walitolewa na wazungu kwa kwenda kinyume nao lakini pia wananchi wa hizo nchi waliwachoka pia sababu ya ubinafsi na roho mbaya zao.


Na Unaposema Afrika hatuhitaji kuvushwa stage na demokrasia ya Marekani unamaanisha nini hasa? changamoto ulizotaja hapo zinaweza kutatuliwa kwa njia gani?
Maelezo mazuri japo hao wazungu wamejaa unafiki mkubwa na kujitahidi kupenyeza mawazo hasi juu ya viongozi wanao kwenda kinyume nao.
Kwanini hawaendi kumdhibiti north korea?
Kwanini hawakwendi kudhibiti jamhuri ya watu wa china wakati aina ya utawala wa kiafrika unafanana sana na utawala wa watu wa china?
 
sasa kwa utawala wa viongozi wa waafrica why nisifurahie vikwazo?.
yaan umuue baba, mwanangu, mjomba wangu et yangu kisa unataka kujenga fry over?.
acheni kutete udhalimu
Ila ni sawa na unabariki kwa wazungu kuja kuua watu wa mataifa wengine kwa ajili ya kujenga nchi zao?
 
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa Alhamisi ameiomba Marekani kuondoa vikwazo dhidi ya Zimbabwe akisema kwamba vimeongeza janga la kibinadamu pamoja na kudorora kwa uchumi, wakati akipendekeza kuwepo kwa mashauriano ili kumaliza uhasama uliopo.

Alena Douhan ambaye ni mjumbe maalum wa UN wa masuala yanayohusiana na vikwazo na amekuwepo nchini Zimbabwe kwa karibu wiki mbili sasa wakati akitathmini athari zitokanazo na vikwazo vya Marekani kwenye taifa hilo la kusini mwa Afrika.

Marekani iliweka vikwazo vya kifedha na vya kusafiri kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa na kijeshi pamoja na wafanyabiashara yakiwemo makampuni yanayohusishwa na serikali, takriban miongo miwili iliyopita.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AP hatua hiyo ilichukuliwa baada ya wakulima wa kizungu kupokonywa mashamba yao pamoja na wizi wa kura na ukiukaji wa haki za binadamu kutoka kwa kiongozi wa muda mrefu marehemu Robert Mugabe.

Ubalozi wa Marekani mapema wiki hii umesema kwamba unaweza kuondoa vikwazo hivyo baada ya kuthibitisha kwamba watu waliowekewa wameacha kuhujumu demokrasia, kushiriki ufisadi pamoja kukiuka haki za kibinadamu.
Viongozi hao yaani mtu limesababisha wenzake wanaishi km mashetani lenyewe limejifia teyari...

Hapa KWETU Mungu alitupenda mapema mapenzi yake yakatimizwa maana hadi 2025 tungekuwa Zimbabwe ya pili .
 
nafurahia Karma inavyotenda Kazi.
Gaddafi aliua na yeye akauawa.
ukiua kwa shoka remember karma treat everybody equal.
Kwa mtazamo wa kisasi unaweza kuwa sahihi kwa 30%!

Lakini je nani adui yako mkubwa kati ya wazungu na hao viongozi wa africa?

Je ni sahihi kwako ukaukabidhi ugomvi wa familia ukawa unatatuliwa na jirani ambae una uhakika hana upendo na familia yako?

Je wao wakiwa na tofauti zao (utawala wa trump ulivyo pingwa na wanaharakati) wanaweza wakatoa upenyo mtu mweusi akawatatulie matatizo?

Kwanini mataifa yenye nguvu kama china huwa hawasogezi pua zao kutaka kuingilia ugomvi hata kama kuna uvunjifu wa hizo zinazo itwa haki za binadamu?

Mwisho, je wao ni wasafi sana au wamekamilika sana mpaka waache kushughulikia ya kwao waje huku kwetu??
 
Sasa kuwekea nchi vikwazo sababu ya viongozi wenye uwezo wa kuishi watakavyo huku wananchi ndio wakiwa wahanga nayo sio kukiuka haki za binadamu?

Kosa la viongozi adhabu ya wananchi halafu unasema unatetea haki za binadamu kweli?
Marekani na washkaji zake wauaji wakubwa.
Hii adhabu ya vikwazo vya kiuchumi ililenga hasa viongozi wajirudi baada ya kuona mateso ya wananchi wao, lakini ukweli ni kwamba viongozi wengi, hasa Africa, hawajali shida za wananchi wao, wao wanachojali ni namna watakavyobaki madarakani, hata kama wananchi wanakufa kwa hivyo vikwazo.
 
Maelezo mazuri japo hao wazungu wamejaa unafiki mkubwa na kujitahidi kupenyeza mawazo hasi juu ya viongozi wanao kwenda kinyume nao.
Kwanini hawaendi kumdhibiti north korea?
Kwanini hawakwendi kudhibiti jamhuri ya watu wa china wakati aina ya utawala wa kiafrika unafanana sana na utawala wa watu wa china?
Wazungu wanapenyeza mawazo hasi au ndivyo walivyo viongozi wengi wa Afrika. kabla ya wazungu kuja kuwatoa kwa maslahi yao ilitakiwa tuanze kuandamana sisi wenyewe tuwatoe kwa maslahi yetu ila kwakuwa wametushinda nguvu basi hata wakitolewa na hao wazungu hatuna tunachopoteza sababu hawakuwahi kuwa watumishi wetu kama walivyoapa.

Mzungu kushindwa kutoa utawala fulani wa kidhalim popote pale duniani hailalishi sisi kuwakubali watawala madikteta.

Utawala wa China haufanani na wa nchi za kiafrika.
 
Hii adhabu ya vikwazo vya kiuchumi ililenga hasa viongozi wajirudi baada ya kuona mateso ya wananchi wao, lakini ukweli ni kwamba viongozi wengi, hasa Africa, hawajali shida za wananchi wao, wao wanachojali ni namna watakavyobaki madarakani, hata kama wananchi wanakufa kwa hivyo vikwazo.
Mfano, Samia ameanza kuongelea uchaguzi ujao miezi kadhaa tu baada ya uchaguzi uliopita, huyu maana yake madaraka ndio kipaumbele.
 
Kwa mtazamo wa kisasi unaweza kuwa sahihi kwa 30%!

Lakini je nani adui yako mkubwa kati ya wazungu na hao viongozi wa africa?

Je ni sahihi kwako ukaukabidhi ugomvi wa familia ukawa unatatuliwa na jirani ambae una uhakika hana upendo na familia yako?

Je wao wakiwa na tofauti zao (utawala wa trump ulivyo pingwa na wanaharakati) wanaweza wakatoa upenyo mtu mweusi akawatatulie matatizo?

Kwanini mataifa yenye nguvu kama china huwa hawasogezi pua zao kutaka kuingilia ugomvi hata kama kuna uvunjifu wa hizo zinazo itwa haki za binadamu?

Mwisho, je wao ni wasafi sana au wamekamilika sana mpaka waache kushughulikia ya kwao waje huku kwetu??
yaan vile vijana wa Jiwe walivyokuwa wanamuwinda Tundu Lissu mithili ya anawindwa Digi digi alafu unamtaka Tundu Lissu awaombe akina Ali bongo,Omary bashiri na akina kagame ndio waje kusuruhisha kubakwa kwa demokrasia Tanzania, kweli?.

2:, moja ya sababu ndogo kati ya nyingi na kubwa ni kwamba:, wanaingilia mambo yetu kwasababu tunapokea misaada mingi kupitia mgongo wa kukuza demokrasia.
achen kupokea misaada yao na msifuate miundo ya serikali zao mambo ya bunge na mahakama yafutwe ibaki serikali ya KITEMI tu.
kwa muda huu kiongozi fulan wa Africa anapewa sehemu fulan ya kodi anayokatwa Mbappe ili kujenga mashimo ya vyoo na kukuza demokrasia nchini kwake then baada ya muda kiongozi huyo atatumia pesa hiyo kulipa wasiojulikana ili waue wapinzani wake alafu waliyompa hizo pesa wakihoji anasema WANAMUNGILIA.

3:, China hataki kujiingiza kwenye mambo ya haki za binadamu etc kwasababu kimikakati zaidi.
china hataki kukaruzana na akina Kageme kwasababu ya haki za binadamu china yeye ni kuchuma chake nyie uaneni hadi KATA nzima abaki mtu mmoja, china ilo halimhusu.
 
Wazungu wanapenyeza mawazo hasi au ndivyo walivyo viongozi wengi wa Afrika. kabla ya wazungu kuja kuwatoa kwa maslahi yao ilitakiwa tuanze kuandamana sisi wenyewe tuwatoe kwa maslahi yetu ila kwakuwa wametushinda nguvu basi hata wakitolewa na hao wazungu hatuna tunachopoteza sababu hawakuwahi kuwa watumishi wetu kama walivyoapa.

Mzungu kushindwa kutoa utawala fulani wa kidhalim popote pale duniani hailalishi sisi kuwakubali watawala madikteta.

Utawala wa China haufanani na wa nchi za kiafrika.
Je ni kweli viongozi wetu wote ni waasi kama wanavyo sema hao wazungu?

Je kwao kuna usafi mkubwa kama wanao uhubiri upatikane huku?

Swali la mwisho, je baada ya hao wazungu kufanikiwa kuwaondoa hao watawala wetu hali inabakije kwa wewe mwananchi wa kawaida?
 
yaan vile vijana wa Jiwe walivyokuwa wanamuwinda Tundu Lissu mithili ya anawindwa Digi digi alafu unamtaka Tundu Lissu awaombe akina Ali bongo,Omary bashiri na akina kagame ndio waje kusuruhisha kubakwa kwa demokrasia Tanzania, kweli?.

2:, moja ya sababu ndogo kati ya nyingi na kubwa ni kwamba:, wanaingilia mambo yetu kwasababu tunapokea misaada mingi kupitia mgongo wa kukuza demokrasia.
achen kupokea misaada yao na msifuate miundo ya serikali zao mambo ya bunge na mahakama yafutwe ibaki serikali ya KITEMI tu.
kwa muda huu kiongozi fulan wa Africa anapewa sehemu fulan ya kodi anayokatwa Mbappe ili kujenga mashimo ya vyoo na kukuza demokrasia nchini kwake then baada ya muda kiongozi huyo atatumia pesa hiyo kulipa wasiojulikana ili waue wapinzani wake alafu waliyompa hizo pesa wakihoji anasema WANAMUNGILIA.

3:, China hataki kujiingiza kwenye mambo ya haki za binadamu etc kwasababu kimikakati zaidi.
china hataki kukaruzana na akina Kageme kwasababu ya haki za binadamu china yeye ni kuchuma chake nyie uaneni hadi KATA nzima abaki mtu mmoja, china ilo halimhusu.
1. Hao uliwataja au viongozi wa africa kwa ujumla wanatofauti gani na hao weupe?
Mbona mzee jakaya amekuwa akisuluhisha migogoro mingi tu wakati alipokuwa mwenyekiti wa AU?
Je, hakuna viongozi wa mfano huo walioko katika nchiz nyingine za africa?

2. Mkuu sijapingana na kuwepo demokrasia lakini kama utakuwa umenielewa.
Demokrasia sio kuzuia kuvunja sheria ila demokrasia ni kuchukua hatua stahiki pale sheria zinapo vunjwa na hilo sio tatizo la kwetu pekee hata kwao lipo mf: mara ngapi CIA wameshitakiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kuvunja haki za binadamu kwenye magereza yao lakini hakuna hata mmoja alie adhibiwa kwa hilo?
Kwanini wao wasikamilishe usafi nyumbani mwao ila wanakimbilia kurukia kwa jirani ilhali kwao kuna uchafu?

3. Ni kweli China hataki kujiingiza kwa sababu kimkakati lakini hata hao wazungu wanajiingiza kwa sababu za kimkakati vivyo hivyo
 
Je ni kweli viongozi wetu wote ni waasi kama wanavyo sema hao wazungu?

Je kwao kuna usafi mkubwa kama wanao uhubiri upatikane huku?

Swali la mwisho, je baada ya hao wazungu kufanikiwa kuwaondoa hao watawala wetu hali inabakije kwa wewe mwananchi wa kawaida?
Sio wote ila wengi wanaofanyiwa njama za kutolewa ni madikteta tayari,mifano ya viongozi wachache ni Malcom Lumumba ambae alitolewa sababu ya kuegemea Russia ila hakuwa dikteta nchini kwake, kuna huyu mwingine Thomas Sankara nae alitolewa sababu ya kuegemea ujamaa lakini hakuwa dikteta.

Hakuna nchi ambayo ni safi kabisa ila mifumo ya hizo nchi ni mizuri ukifananisha ni hii ya kuongozwa na madikteta lakini pia hata kama ingekuwa mibaya je maana yake na sisi tuvumilie tu haya mateso wanayotuletea viongozi wetu.

Pia wazungu hawawaondoi viongozi wa nchi sababu ya kulinda demokrasia na wala hawajali mfumo gani unatumia kuongoza nchi yako, ni hadi uende kinyume na maslahi yao ndio wanakufata na watakuondoa bila kujali kulikuwa na demokrasia au hakuna.

Baada ya kuondolewa hali inabaki kuwa mbaya sababu hawa madikteta wanajiweka kuwa kitovu cha kila kitu kwahiyo akifa tu na mfumo mzima umekufa lakini pia vikwazo ambavyo nchi ilikuwa imewekewa haviondoki mara moja baada ya kufa dikteta fulani kwa hiyo kiongozi anaefuata bado atakuwa kwenye wakati mgumu kunyanyua uchumi na kurudisha usalama kama kulikuwa na vita.
 
1. Hao uliwataja au viongozi wa africa kwa ujumla wanatofauti gani na hao weupe?
Mbona mzee jakaya amekuwa akisuluhisha migogoro mingi tu wakati alipokuwa mwenyekiti wa AU?
Je, hakuna viongozi wa mfano huo walioko katika nchiz nyingine za africa?

2. Mkuu sijapingana na kuwepo demokrasia lakini kama utakuwa umenielewa.
Demokrasia sio kuzuia kuvunja sheria ila demokrasia ni kuchukua hatua stahiki pale sheria zinapo vunjwa na hilo sio tatizo la kwetu pekee hata kwao lipo mf: mara ngapi CIA wameshitakiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kuvunja haki za binadamu kwenye magereza yao lakini hakuna hata mmoja alie adhibiwa kwa hilo?
Kwanini wao wasikamilishe usafi nyumbani mwao ila wanakimbilia kurukia kwa jirani ilhali kwao kuna uchafu?

3. Ni kweli China hataki kujiingiza kwa sababu kimkakati lakini hata hao wazungu wanajiingiza kwa sababu za kimkakati vivyo hivyo
wanaua wanabaki huru kwasababu mahakama imewaacha huru ama wanaua na wanabaki tu huru bila kuchukuliwa hatua zozote za
kisheria kama waliomtoa Matumbo Mwangosi then wakapandishwa vyeo?.
Data za akina Musiba kuwa:, marekani dakika 10 wanakufa watu 40 lakini Tanzania wakifa 3 mnamsakama magufuli" ndizo unazisema hapa ama una data nyingine nje na hizo, Chief?
 
Back
Top Bottom