Marekani yajiondoa kwenye mkataba wa silaha

Marekani yajiondoa kwenye mkataba wa silaha

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,618
Reaction score
9,607
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Mike Pompeo amesema Marekani itajitoa kwenye mkataba huo Februari 2, akiongeza kuwa ikiwa Urusi haitarudi katika njia ya kuheshimu utekelezwaji wa mkataba huo, basi utavunjika.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Mike Pompeo ametangaza kuwa Marekani inajitoa kwenye mkataba kati ya Marekani na Urusi wa kuzuia urundikiaji wa silaha tangu kumalizika kwa Vita Baridi.

Kujiondoa kwa Marekani kumekuwa kukitarajiwa kwa miezi kadhaa. Hatua hiyo imetokana na mzozo ambao haujasuluhishwa kwa miaka mingi wa madai kuwa Urusi imekuwa ikikiuka mkataba huo ulioafikiwa mwaka 1987 ambao unapiga marufuku baadhi ya makombora ya kufyatuliwa ardhini. Urusi imekana madai ya kukiuka mkataba huo.

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Mike Pompeo amesema Marekani itajitoa kwenye mkataba huo kesho Jumamosi, akiongeza kuwa ikiwa Urusi haitarudi katika njia ya kuheshimu utekelezwaji wa mkataba huo, basi utavunjika. Pompeo ameeleza kuwa:

''Tuliipa Urusi muda wa kutosha wa kurekebisha mienendo yake na kujitolea kikamilifu kuheshimu mkataba wa INF. Muda huo unamalizika kesho lakini Urusi imekataa kuchukua hatua yoyote ya kurejesha hali halisi na inayoweza kuthibitishwa ya kuheshimu mkataba katika kipindi cha siku 60 tulizoipa. Kwa hivyo kuanzia kesho, Jumamosi, Marekani itajiondoa kwenye mkataba huo''

DW
 
Kujitoa katika Mkataba huu ni manufaa kwa Nchi ya Marekani, maana sasa watajitanua na kuwa na uwezo wa kuwa-counter Wachina ambao hawapo kwenye huo mkataba na walikuwa wanapunguza ushawishi wa Marekani huko Asia.
 
Kujitoa katika Mkataba huu ni manufaa kwa Nchi ya Marekani, maana sasa watajitanua na kuwa na uwezo wa kuwa-counter Wachina ambao hawapo kwenye huo mkataba na walikuwa wanapunguza ushawishi wa Marekani huko Asia.
Nia ya marekani ni kupambana Na China Ila ukipitia makala mbali mbali kuvunjika kwa huu mkataba ni manufaa kwa Russia Kwa sababu uzalishaji wake ni nafuu Sana kwake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makombora ya masafa ya kati ambayo ni land based yalizuia purely kwa advantage ya europe,
makombora hayo ni ya km 2000-5000,ukicheki ramani utaona kuwa marekani imepakana na mexico na canada,kwingine kushoto na kulia ni maelfu ya kilomita za bahari,kwahiyo hakuna namna Russia ingetumia medium range ya ardhini dhidi ya marekani,marekani walimrubini Russia kuingia huo mkenge ukichukulia europe na Russia zinapakana kwa hiyo Russia angekosa uhalali wa kutumia land based medium range missile
 
Makombora ya masafa ya kati ambayo ni land based yalizuia purely kwa advantage ya europe,
makombora hayo ni ya km 2000-5000,ukicheki ramani utaona kuwa marekani imepakana na mexico na canada,kwingine kushoto na kulia ni maelfu ya kilomita za bahari,kwahiyo hakuna namna Russia ingetumia medium range ya ardhini dhidi ya marekani,marekani walimrubini Russia kuingia huo mkenge ukichukulia europe na Russia zinapakana kwa hiyo Russia angekosa uhalali wa kutumia land based medium range missile
Kwa hiyo Russia ...wame shtuka !?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu eti wakaruhusu sea based medium range missile mfano Tomahwk,marekani akijua kabisa manowari zake zina base kibao arround Russia,huku Russia akiwa hana navy base arround US,kwa hiyo hata hayo makombora yangekuwa useless kwa Russia,wakati marekani wakiwa na fursa ya kuyatumia,
hakuna manowari ya mrusi inaweza toka Russia kwenda karibu na marekani ili tu kurusha medium range missile kwani itaonekana ikiwa bado iko bahari ya medditerania na hivyo itakuta marekani wamejiandaa,
unaweza jiuliza kwanini medium range missile is so important,
jibu ni kuwa ukishambuliwa na intercontinental missile,unakuwa na window oppoyunity ya kujiandaa,kwa mfano mrusi akirusha inachukua nusu saa kitu kutua new york,kwahivyo wana nusu saa ya kureact,
tofauti na medium range ni suala la dakika mbili tatu
 
Yap,warusi walishituka,ukichukulia mkataba unamfunga russia na marekani wakati nchi kama israel,china,iran,north korea etc wanazo,na ukichukulia marekani hazihitaji kwani hana jirani wa kumshambulia na land based medium range missile,kwani wana manowari zao zinamfuata adui kwani base zao ni nyingi na kila nchi iko within range na manowari za marekani
 
Halafu eti wakaruhusu sea based medium range missile mfano Tomahwk,marekani akijua kabisa manowari zake zina base kibao arround Russia,huku Russia akiwa hana navy base arround US,kwa hiyo hata hayo makombora yangekuwa useless kwa Russia,wakati marekani wakiwa na fursa ya kuyatumia,
hakuna manowari ya mrusi inaweza toka Russia kwenda karibu na marekani ili tu kurusha medium range missile kwani itaonekana ikiwa bado iko bahari ya medditerania na hivyo itakuta marekani wamejiandaa,
unaweza jiuliza kwanini medium range missile is so important,
jibu ni kuwa ukishambuliwa na intercontinental missile,unakuwa na window oppoyunity ya kujiandaa,kwa mfano mrusi akirusha inachukua nusu saa kitu kutua new york,kwahivyo wana nusu saa ya kureact,
tofauti na medium range ni suala la dakika mbili tatu
Point tupu dadekii!
 
Yap,warusi walishituka,ukichukulia mkataba unamfunga russia na marekani wakati nchi kama israel,china,iran,north korea etc wanazo,na ukichukulia marekani hazihitaji kwani hana jirani wa kumshambulia na land based medium range missile,kwani wana manowari zao zinamfuata adui kwani base zao ni nyingi na kila nchi iko within range na manowari za marekani
Aisee " .... Basi imekula kwao ...

(1) Je endapo USA wakijitoa katika huo mkataba ? Inaweza kuchangia athari zozote katika dunia !? ...

(2) Tutarajie dunia ya namna gani baada ya USA kujitoa katika huo mkataba .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makombora ya masafa ya kati ambayo ni land based yalizuia purely kwa advantage ya europe,
makombora hayo ni ya km 2000-5000,ukicheki ramani utaona kuwa marekani imepakana na mexico na canada,kwingine kushoto na kulia ni maelfu ya kilomita za bahari,kwahiyo hakuna namna Russia ingetumia medium range ya ardhini dhidi ya marekani,marekani walimrubini Russia kuingia huo mkenge ukichukulia europe na Russia zinapakana kwa hiyo Russia angekosa uhalali wa kutumia land based medium range missile
Nime kupata vizur sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu eti wakaruhusu sea based medium range missile mfano Tomahwk,marekani akijua kabisa manowari zake zina base kibao arround Russia,huku Russia akiwa hana navy base arround US,kwa hiyo hata hayo makombora yangekuwa useless kwa Russia,wakati marekani wakiwa na fursa ya kuyatumia,
hakuna manowari ya mrusi inaweza toka Russia kwenda karibu na marekani ili tu kurusha medium range missile kwani itaonekana ikiwa bado iko bahari ya medditerania na hivyo itakuta marekani wamejiandaa,
unaweza jiuliza kwanini medium range missile is so important,
jibu ni kuwa ukishambuliwa na intercontinental missile,unakuwa na window oppoyunity ya kujiandaa,kwa mfano mrusi akirusha inachukua nusu saa kitu kutua new york,kwahivyo wana nusu saa ya kureact,
tofauti na medium range ni suala la dakika mbili tatu

Warusi wana uhusuano wa karibu na nchi zilizoizunguka marekani kama Cuba na Venezuela.. hivyo wamarekani hawapo salama sana
 
Back
Top Bottom