Hakika kila anayedhulumu, kamwe hatayamaliza maisha yake ya hapa Duniani kwa amani, na wala pepo hatairithi, bila ya toba iliyo kuu. Laana hata siku moja haikupi amani. Wote waliodhulumu mali, haki na uhai wa watu, wanaishi kwa majuto makubwa mioyoni mwao. Wanahangaika, wasijue watue vipi mizigo yao.
Mwalimu katika kujutia, alisema, "katiba ya Tanzania hii iliyopo ni mbaya, inamfanya Rais kuwa dikteta", maana yake ni kwamba alikuwa anajutia udikteta wowote alioufanya, na akaeleza kuwa chanzo chake ni katiba. Alikuwa akijuta, kwa nini hakuweza kufanya mabadiliko ya katiba, na kuifanya Tanzania kuwa na katiba bora yenye kuwapa haki Watanzania. Mwalimu, pamoja na kujua kuwa Katiba yetu ni mbaya, hakuibadili. Hili ndiyo kosa alilolijutia. Katika kupunguza simanzi moyoni mwake, aliamua kuweka wazi kuwa Katiba ambayo yeye alishiriki kuiandaa, na ambayo aliitumia kuongoza nchi, ilikuwa katiba mbaya kwa sababu inamfanya Rais kuwa dikteta na mungu mtu.
Akaja Mwinyi, alijua katiba ni mbaya, na mtangulizi wake alishuhudia hilo kwa kauli yake, lakini Mwinyi hakusimamia uanzishaji wa katiba mpya. Alifurahia kuwa Rais dikteta, japo katika kutenda, aliamua kuwa muungwana wa kiasi fulani, lakini hakuwahi kuonesha dhamira ya kuwataka Watanzania waongozwe kwa misingi ya haki inayosimamiwa na katiba bora. Laana itamwandama.
Akaja Mkapa, akaitumia vyema katiba inayomfanya Rais kuwa dikteta. Akafurahia. Akaitumia katiba hiyo hiyo, kuminya haki za kikatiba kwa wapinzani. Akawanyima Watanzania haki ya kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi. Akawaua Wazanzibari, bila ya kuhojiwa na yeyote. Laana haikumwacha. Hakuyamalizia maisha yake kwa amani Duniani. Dhamira ilimtesa na kumsuta. Akaona aheri akiri na kuwaomba msamaha Watanzania. Kwenye kitabu chake, akasema, mauaji ya Wazanzibari, yaliutesa moyo wake. Pia akasema, anapenda nchi iwe na Tume huru ya uchaguzi. Wakati wa uongozo wake hakufanya, lakini baadaye dhamira yake iliendelea kumshtaki na kumtesa. Baada ya majuto na toba, Mungu akampumzisha.
Jakaya aliyafurahia mamlaka ya kidikteta. Akamaliza awamu yake ya kwanza bila ya kuandaa katiba bora. Mwishoni mwa muhula wake wa pili, akataka kujikosha, akanzisha mchakato wa katiba. Kwa vile Mungu hataki unafiki, hakufanikiwa. Ulikiwa na miaka 10, kwa nini ukasubirie mwaka wa 9 ndiyo uanzishe mchakato wa katiba mpya? Yaani wewe ulifurahia Urais wa kidikteta halafu unajikosha na kutaka katiba mpya mwishoni mwa muhula wako, katiba ambayo wewe hutaiishi kwa sababu hutakuwa madarakani! Mungu hataki unafiki, mchakato haukukamilika ili katika kumbukumbu ibakie kuwa ulifurahia kuwa Rais dikteta.
Akaja Magufuli, hakuwa mnafiki, yeye alinena wazi kuwa hataki Watanzania waongozwe kwa haki, hataki katiba mpya, hataki Watanzania wachague viongozi, wa kuchagua ni yeye tu. Akahakikisha kila mahali, si bungeni, si mahakamani, kote, ni yeye ndiye mwamuzi. Akasema kwamba muhimili wake, wa Urais, ndiyo una mizizi mirefu. Mingine yote au haina miziz au miziz yake inaelea hewani. Akataka afurahie mamlaka yasiyo na mipaka wala yasiyo hojiwa. Pamoja na kufanikiwa kuzima sauti za watu wote, pamoja na kuwafanyia uovu wa kila aina wanaohoji mamlaka yake, hakupata amani. Japo hakuna kipimo, lakini ukweli ni kuwa huyu ndiye Rais aliyeishi kwa kukosa amani kuliko kiongozi yeyote. Na mwisho Mungu akawapelekea injili wale wote walioamini kuwa wanaweza kutenda uovu wowote alimrudi Rais amewaruhusu, akawaonesha kuwa hakuna mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ambaye mamlaka yake hayana mipaka, ukiiondoa mipaka inayowekwa na wanadamu wenzako, utakutana na mamlaka ya aliyetuba. Akamwondoa Duniani mapema, akiwa hajafanikisha mambo mengi aliyoamini yangeweza kumwongezea utukufu.
Kule Zanzibar, Komandoo mwisho umekuwa wa majuto. Karume hana ani moyoni. Na sasa ameelezea jinsi CCM, kupitia Jecha, walivyopora ushindi wa Maalim Seif. Anasema , aliwaambia viongozi wenzake wa CCM kuwa, mboba hata wapinzani ni Wazanzibari? Kwa nini wananyimwa haki ya kuongoza. Akawaambia kuwa Maalim Seif ni mtu muungwana sana, tofauti na CCM walivypkuwa wakimpaka matope. Karume hana amani wala furaha kwa kushiriki dhuluma dhidi ya Seif. Jecha, ndiyo usiseme. Hawa wote wanatafuta njia ya kupungiza simanzi mioyoni mwao.
Sasa tunaye Samia, huyu naye kwa mwelekeo uliopo, anataka kutenda kama Kikwete, kuuleta mchakato wa katiba mpya mwishoni mwa awamu yake ya pili. Yaani hiyo katiba mpya ikambane Rais mwingine, na siyo yeye. Hakika naye hatafanikiwa maana Mungu hataki unafiki. Anayetaka Watanzania waongpzwe kwa haki, ni yule atakayeleta mchakato wa katiba mpya, mara tu baada ya yeye kushika madaraka ili yeye mwenyewe akawe mtu wa kwanza wa kuongoza kwa kutumia katiba hiyo inayotoa mamlaka makubwa kwa wananchi na siyo Rais. Hakika, na Samia, kama mchakato wa kupata katiba mpya, hautakuja kwenye awamu yake hii ya kwanza, laana ijuu yake, atajutia, na mwisho wake hautakuja kuwa na amani.
Watu kama Siro, Kingai, Mahita, na wengineo, wafiatilieni, kamwe hawataufurahia uzee wao hapa Duniani, na wala hawataonja furaha huko ahera. Hawa hata kama watapata mali na vyeo, lakini kamwe mioyo yao haitaionja furaha ili mateso yao ya ndani yakayazidi ya wale wadhulumiwa.
Ujumbe wa Jumla:
Kubambikia watu kesi za uongo, kutesa na kusababsha watu wafungwe bila hatia, ni matendo ya dhuluma. Dhuluma huleta laana kuanzia wewe mpaka kizazi chako cha 4.
Huu ni ujumbe maalum wa kitume kwa watu wenye Roho wa Mungu.
Msisitizo: Yafurahie maisha yako ya ujanani kwa kutenda haki, ili uzee wako ujae neema, matumaini na furaha.
Mwalimu katika kujutia, alisema, "katiba ya Tanzania hii iliyopo ni mbaya, inamfanya Rais kuwa dikteta", maana yake ni kwamba alikuwa anajutia udikteta wowote alioufanya, na akaeleza kuwa chanzo chake ni katiba. Alikuwa akijuta, kwa nini hakuweza kufanya mabadiliko ya katiba, na kuifanya Tanzania kuwa na katiba bora yenye kuwapa haki Watanzania. Mwalimu, pamoja na kujua kuwa Katiba yetu ni mbaya, hakuibadili. Hili ndiyo kosa alilolijutia. Katika kupunguza simanzi moyoni mwake, aliamua kuweka wazi kuwa Katiba ambayo yeye alishiriki kuiandaa, na ambayo aliitumia kuongoza nchi, ilikuwa katiba mbaya kwa sababu inamfanya Rais kuwa dikteta na mungu mtu.
Akaja Mwinyi, alijua katiba ni mbaya, na mtangulizi wake alishuhudia hilo kwa kauli yake, lakini Mwinyi hakusimamia uanzishaji wa katiba mpya. Alifurahia kuwa Rais dikteta, japo katika kutenda, aliamua kuwa muungwana wa kiasi fulani, lakini hakuwahi kuonesha dhamira ya kuwataka Watanzania waongozwe kwa misingi ya haki inayosimamiwa na katiba bora. Laana itamwandama.
Akaja Mkapa, akaitumia vyema katiba inayomfanya Rais kuwa dikteta. Akafurahia. Akaitumia katiba hiyo hiyo, kuminya haki za kikatiba kwa wapinzani. Akawanyima Watanzania haki ya kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi. Akawaua Wazanzibari, bila ya kuhojiwa na yeyote. Laana haikumwacha. Hakuyamalizia maisha yake kwa amani Duniani. Dhamira ilimtesa na kumsuta. Akaona aheri akiri na kuwaomba msamaha Watanzania. Kwenye kitabu chake, akasema, mauaji ya Wazanzibari, yaliutesa moyo wake. Pia akasema, anapenda nchi iwe na Tume huru ya uchaguzi. Wakati wa uongozo wake hakufanya, lakini baadaye dhamira yake iliendelea kumshtaki na kumtesa. Baada ya majuto na toba, Mungu akampumzisha.
Jakaya aliyafurahia mamlaka ya kidikteta. Akamaliza awamu yake ya kwanza bila ya kuandaa katiba bora. Mwishoni mwa muhula wake wa pili, akataka kujikosha, akanzisha mchakato wa katiba. Kwa vile Mungu hataki unafiki, hakufanikiwa. Ulikiwa na miaka 10, kwa nini ukasubirie mwaka wa 9 ndiyo uanzishe mchakato wa katiba mpya? Yaani wewe ulifurahia Urais wa kidikteta halafu unajikosha na kutaka katiba mpya mwishoni mwa muhula wako, katiba ambayo wewe hutaiishi kwa sababu hutakuwa madarakani! Mungu hataki unafiki, mchakato haukukamilika ili katika kumbukumbu ibakie kuwa ulifurahia kuwa Rais dikteta.
Akaja Magufuli, hakuwa mnafiki, yeye alinena wazi kuwa hataki Watanzania waongozwe kwa haki, hataki katiba mpya, hataki Watanzania wachague viongozi, wa kuchagua ni yeye tu. Akahakikisha kila mahali, si bungeni, si mahakamani, kote, ni yeye ndiye mwamuzi. Akasema kwamba muhimili wake, wa Urais, ndiyo una mizizi mirefu. Mingine yote au haina miziz au miziz yake inaelea hewani. Akataka afurahie mamlaka yasiyo na mipaka wala yasiyo hojiwa. Pamoja na kufanikiwa kuzima sauti za watu wote, pamoja na kuwafanyia uovu wa kila aina wanaohoji mamlaka yake, hakupata amani. Japo hakuna kipimo, lakini ukweli ni kuwa huyu ndiye Rais aliyeishi kwa kukosa amani kuliko kiongozi yeyote. Na mwisho Mungu akawapelekea injili wale wote walioamini kuwa wanaweza kutenda uovu wowote alimrudi Rais amewaruhusu, akawaonesha kuwa hakuna mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ambaye mamlaka yake hayana mipaka, ukiiondoa mipaka inayowekwa na wanadamu wenzako, utakutana na mamlaka ya aliyetuba. Akamwondoa Duniani mapema, akiwa hajafanikisha mambo mengi aliyoamini yangeweza kumwongezea utukufu.
Kule Zanzibar, Komandoo mwisho umekuwa wa majuto. Karume hana ani moyoni. Na sasa ameelezea jinsi CCM, kupitia Jecha, walivyopora ushindi wa Maalim Seif. Anasema , aliwaambia viongozi wenzake wa CCM kuwa, mboba hata wapinzani ni Wazanzibari? Kwa nini wananyimwa haki ya kuongoza. Akawaambia kuwa Maalim Seif ni mtu muungwana sana, tofauti na CCM walivypkuwa wakimpaka matope. Karume hana amani wala furaha kwa kushiriki dhuluma dhidi ya Seif. Jecha, ndiyo usiseme. Hawa wote wanatafuta njia ya kupungiza simanzi mioyoni mwao.
Sasa tunaye Samia, huyu naye kwa mwelekeo uliopo, anataka kutenda kama Kikwete, kuuleta mchakato wa katiba mpya mwishoni mwa awamu yake ya pili. Yaani hiyo katiba mpya ikambane Rais mwingine, na siyo yeye. Hakika naye hatafanikiwa maana Mungu hataki unafiki. Anayetaka Watanzania waongpzwe kwa haki, ni yule atakayeleta mchakato wa katiba mpya, mara tu baada ya yeye kushika madaraka ili yeye mwenyewe akawe mtu wa kwanza wa kuongoza kwa kutumia katiba hiyo inayotoa mamlaka makubwa kwa wananchi na siyo Rais. Hakika, na Samia, kama mchakato wa kupata katiba mpya, hautakuja kwenye awamu yake hii ya kwanza, laana ijuu yake, atajutia, na mwisho wake hautakuja kuwa na amani.
Watu kama Siro, Kingai, Mahita, na wengineo, wafiatilieni, kamwe hawataufurahia uzee wao hapa Duniani, na wala hawataonja furaha huko ahera. Hawa hata kama watapata mali na vyeo, lakini kamwe mioyo yao haitaionja furaha ili mateso yao ya ndani yakayazidi ya wale wadhulumiwa.
Ujumbe wa Jumla:
Kubambikia watu kesi za uongo, kutesa na kusababsha watu wafungwe bila hatia, ni matendo ya dhuluma. Dhuluma huleta laana kuanzia wewe mpaka kizazi chako cha 4.
Huu ni ujumbe maalum wa kitume kwa watu wenye Roho wa Mungu.
Msisitizo: Yafurahie maisha yako ya ujanani kwa kutenda haki, ili uzee wako ujae neema, matumaini na furaha.