Mapya yaibuka: Maafisa wa TMAA walipewa hela ili Smelter isijengewe Tanzania

Muda si mrefu mkono wa sheria utawapata tu.
Yani we kijana unajipa matumaini utafikiri mgonjwa wa ukimwi

Tatizo humu JF mnabadisha id mtakavyo na hakuna jinsi kuwapata watu wa style yako,maana najua mda unakuja na utasema.

Sorry can you submit your phone number kama unajiamini kwa hiki unachokitetea......?ili mda ukifika tukukumbushe kwa nia njema kama watz.
 
Yani we kijana unajipa matumaini utafikiri mgonjwa wa ukimwi

Tatizo humu JF mnabadisha id mtakavyo na hakuna jinsi kuwapata watu wa style yako,maana najua mda unakuja na utasema.

Sorry can you submit your phone number kama unajiamini kwa hiki unachokitetea......?ili mda ukifika tukukumbushe kwa nia njema kama watz.
My phone number contact me humuhumu katika private inbox. Unitumie yako then nitakujibu na Whatsap. Kie ninachokitetea ni jambo la kukusaidia wewe na mimi. Tuache uchama chama.
 
Yani we kijana unajipa matumaini utafikiri mgonjwa wa ukimwi

Tatizo humu JF mnabadisha id mtakavyo na hakuna jinsi kuwapata watu wa style yako,maana najua mda unakuja na utasema.

Sorry can you submit your phone number kama unajiamini kwa hiki unachokitetea......?ili mda ukifika tukukumbushe kwa nia njema kama watz.
Mkuu nenda kalale. Usiku mwema. Kesho kazi .
 
Namshauri Rais kwenye mambo kama haya wala asisumbue Polisi na Mahakama . Hawa TMAA wote wanatakiwa kufilisiwa na kufukuzwa kazi mara moja.
 
Wana JF kuna mambo mapya yanayozidi kujitokeza tangu rais Magufuli awasimamishe maafisa wakuu wa Taasisi ya TMAA inayosimamia MADINI ambayo pia ilimfanya rais Magufuli kumvua Uwaziri Mh.Muhongo kama Waziri wa Madini kwa sababu zilizo wazi.

Inavyosemekana ni kuwa mwaka wa 2009 TUME maalumu iliyojulikana kama PRESIDENTIAL MINING REVIEW COMMISSION,iliyoongozwa na JAJI Mark Bomani. Tume hii ilitoa MAPENDEKEZO kuwa SMELTER ijengwe hapa nchini.

Lakini cha kushangaza ni kuwa maafisa hao wa TMAA wakawa tayari wamekuwa COMPROMISED na Makampuni husika yaani WAKAHONGWA ili WANAYAMAZISHE matakwa ya Tanzania Kuwa na UWEZO wake na TEKNLOJIA HIYO.

Katika mbinu zao za kuzima ripoti na mapendekezo ya tume TMAA, miaka sita iliyopita hivi wakaanza mipango ya KUYAMWAGIA MAJI mapendekezo YOTE ya Tume ya Jaji Mark Bomani ili KUIDHOOFISHA kabisa
Na mwishowe KUZIZIMA kabisa NDOTO za Watanzania kuwa na mitambo yao ya SMELTER.
Na hivyo KUTUSALITI sawasawa ili tuendelee KUIBIWA VIZURI na hayo Makampuni.

Mwaka wa 2011 MAAFISA wa TMAA walitembelea miji ya TOKYO na SAGANOSEKI Copper concentrate Smelter nchini JAPAN ili WAJIONEE wenyewe TEKNOLOJIA hiyo na jinsi nchi yetu inavyoweza KUJIJENGEA Smelter yake yenyewe.

Katika safari yao ilikuwa pia wajue GHARAMA za UWEKEZAJI/UJENZI na uwezo na gharama za uendeshaji nchini.

Ikikikumbuka kuwa tume ya Jaji Mark Bomani ilikuwa pia imeenda huko kabla wakati ikiandika na kuchukuwa DATA, ili kutayarisha ripoti mpya ya sheria ya MINIMG LAW/Sheria mpya za MADINI.

Mwaka 2011 TMAA nao wakatoa ripoti yao iliyojulikana kama:
"A STUDY on VIABILITY to CONSTRUCTING a COPPER Concentrate SMELTER in Tanzania"

Ripoti yao ILIPINGA VIKALI mapendekezo ya Tume ya Jaji Bomani.
Na hivyo Kuwaachia wezi field day ya kuiba mchanga wetu WATAKAVYO na WAPENDAVYO. Maana tayari TMAA walikuwa wamekuwa compromised/WAMEHONGWA.

Kwa wale wanaolaumu uamuzi wa Rais Magufuli na kupendelea Makampuni wanaposikia haya si WAONE HUZUNI kuwa hakika TULIIBIWA Vya KUTOSHA na IMETOSHA?
Na Tanzania INAWEZA kabisa KUJIJENGEA yenyewe hiyo MITAMBO.

Maana NIA TUNAYO na UWEZO TUNAO tukishikana pamoja na kushirikiana kama Watanzania
HAKUNA lolote ambalo Tanzania HAITALIWEZA KULIFANYA.

Kwa Maafisa kama hawa wa TMAA WALIOTUSALITI wanastahili kuwa JELA bila HURUMA.

Hatuwezi kuwa taifa la OMBAOMBA wakati kila RASLIMALI tunayo.
Na hali watu wachache wenye tamaa wanataka tubaki Maskini huku wao wakijenga magorofa
TUNAKATAA kama Watanzania.
Mungu IBARIKI Tanzania na Rais Magufuli.
Chanzo: The EastAfrican.
Mkuu ingependeza sana kama maelezo haya yange ambatana na majina ya wale jamaa zetu wa TMAA walio kwenda Japan na kupinga mapendekezo ya Mzee Bomani. Ikishindikana kuyapata kabisa basi hata hao ambao Rais amewasimamisha ingekuwa vema tukawa tambua . Tunaishi na fisi mijini.
 
Hizo smelter za Japan zinapata wapi mchana?!.
Ha ha haaa, wenye akili zao kichwani wasiokuwa na mchanga wanapelekewa mchanga ili smelter zijengwe , sisi wenye mchanga kibao hatujengi chochote tunasafirisha macontainer ya mchanga kuelekea Japan, ama kweli wajinga ndio waliwao na tunaliwa haswa!
 
i
Mkuu ingependeza sana kama maelezo haya yange ambatana na majina ya wale jamaa zetu wa TMAA walio kwenda Japan na kupinga mapendekezo ya Mzee Bomani. Ikishindikana kuyapata kabisa basi hata hao ambao Rais amewasimamisha ingekuwa vema tukawa tambua . Tunaishi na fisi mijini.
nawezekana kabisa hao jamaa ni kipisi tu kinachoonekana juu cha iceberg kuubwa lililojificha baharini, nani anamiliki madini hapa nchini na nani alipokea 10 pasenti kusaini mikataba mibaya, tunataka waje hapa tuhangaike nao kwa sababu hao ndio wanatoa kinga kubwa mashirika ya kibepari kuliko hata mikataba na sheria zilizopo.
 
Katika hili sakata la mchanga, Mh. Rais J.P. Magufuli asitetereke wala asipunguze mwendo.

Ni kweli kwamba uzembe mwingi katika hili sakata la mchanga umefanywa na watu wetu, wafanyakazi wa serikali na viongozi waliokuwepo. Vilevile ni kweli kwamba katika kukimbilia kupendelea wawekezaji, sirikali iliweka sheria pamoja na usimamizi mbovu katika sekta ya madini. Katika hizo mbio, ni sirikali hiyohiyo iliyosaidia katika kuchukua maeneo ya wananchi ili kutoa nafasi kwa wawekezaji kufanya uwekezaji kwa mategemeo kwamba faida ingekuwa kwa wote, wananchi na wawekezaji. Wakati huo hatukusikia serikali ikishtakiwa na hao wawekezaji au washikaji wao, kwa kuwa walikua ndio wafaidika wakuu.

Kwa upande mmoja, Tanzania imefanikiwa kuwa moja ya wazalishaji wakubwa wa dhahabu barani Afrika. Lakini kwa upande mwingine, Watanzania bado hawajafaidi rasilimali zao. Hiki ndio kilio cha wengi, wakiongozwa na Rais wa Awamu hii. Umasikini bado uko palepale na hauelekei kama unapungua. Sasa serikali ya Rais. J.P. Magufuli imeshtuka na inataka kurekebisha mambo, na huu ni mwanzo tu. Hii ni haki, ni sahihi na muhimu kufanikiwa.

Mabadiliko haya ya kurudisha heshima ya Mtanzania yatafanikiwa na yatatekelezwa kwa kutumia sheria zilizopo. Rais Magufuli apewe support na wote wanaompenda, na wasiompenda ni bora wakae kimya tu kwani watapata fedheha kupinga ajenda hii. Hata hao wawekezaji katika boardroom zao wanajua kabisa kuwa Magufuli yuko sahihi na wakati wa mabadiliko umefika. Wengine wanaweza kutofautiana na approach ya Magufuli kwa sababu hawajazoea kuona kiongozi wa sampuli hii. Waoga na wenye moyo mdogo katika hii vita ya kiuchumi na kisaikolojia ni vema wakae kando na kumwacha Jemadari afanye kazi yake.

Mamlaka na nguvu ziliyotumika na viongozi waliotangulia katika kufanikisha uwekezaji holela ndio hizohizo zitatumika na Rais Magufuli kurudisha taifa katika mstari sahihi. Kwa kudokeza tu, Tanzania bado ina madini na raslimali nyingi sana. Kwa mfano, mchanga wa chuma huko Liganga & mchuchuma nao umeambatana na madini mkakati kwa wingi, kiasi kikubwa kuliko hata hayo tunayosikia kwenye mchanga wa dhahabu.

Magufuli akifanikiwa, Tanzania imefanikiwa. Magufuli akishindwa, Tanzania imeshindwa. Mambo ya chama na siasa after baadaye (2025).
 
Hilo ndo swali kwa nini tumwamini muwekezaji?
Na kwanini tuwaamini ccm walewale waliotudanganya kwa miaka 50?hao hao ndio walioshiriki kupitisha miswaada ya sheria mbovu za madini bungeni wakipiga makofi na vigeregere?
 
Kila ilivyo mali za nchi zitaibiwa tu,hesabu katika kila wafanyakazi 100 wa serikali mmoja tu anaweza kutokea ni mwaminifu na 99 wanaobaki wanajali maslahi ya matumbo yao na sio ya taifa
 
Hilo ndo swali kwa nini tumwamini muwekezaji?
Mwekezaji hana makosa,wenye makosa ni hao waliopewa madaraka na wakayatumia vibaya,wawekezaji ni muhimu katika kukuza taifa ambalo bado liko nyuma kimaendeleo kama TZ
 
Back
Top Bottom