Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Ndugu Wana-JF: katika gazeti la Mwanahalisi la leo kuna hii makala ya Saed Kubenea (Uk wa 10) ambayo nimejaribu kuweka hapa sehemi yake kubwa tu. Makala inaibua mapya kuhusu namna wajumbe wa Baraza la Mawaziri (cabinet) ya JK walivyokuwa na utii (loyalty) katika sehemu mbili. Kwa maneno mengine kuna ‘cabinet' nyingine kivulini (isiyo rasmi) ambao inachota utii kutoka kwa baadhi ya mawaziri wa JK. Nimejaribu ku-highlight sehemu husika:
Kitendawili cha uraia wa Hussein Bashe, mgombea ubunge Nzega (CCM) aliyoenguliwa kimeibua mapya.
Wiki iliyopita, Waziri wa mambo ya Ndani, Lawrence Masha aliutangazia ulimwengu kuwa Bashe ni raia halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akahoji, "nani mwenye mamlaka ya kusema Bashe si raia? Nikiwa waziri mwenye dhamana nasema, Bashe ni raia halali na hakuna atakayebadilisha uamuzi huu."
Aliyesema kuna utata katika uraia wa Bashe ni Rais Jakaya Kikwete, tena ndani ya vikao halali vya chama chake.
Taarifa zinasema, ndani ya ukumbi wa mkutano Kikwete alisimama kidete kutetea hoja yake kwamba Bashe si raia. Alisema amepata ‘taarifa za vyombo vya usalama' zinazothibitisha utata wa uraia wa Bashe.
Wengine walioendeleza kauli ya rais ni viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Katibu Mkuu Yusuf Makamba na Katibu Mwenezi John Chiligati.
Masha amenukuu vifungu kadhaa vya sheria ya uhamiaji akisema vinahalalisha uraia wa Bashe.
Kwa mfano, ananukuu vifungu Na. 5(1) na Na. 7(8) vya Sheria Na. 7 ya uraia ya mwaka 1995 na kusema, "Bashe ni raia halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tena kwa kuzaliwa." Anasema tayari amemjulisha Bashe kuhusu uamuzi huo.
Je, Masha hakushauriana na Kikwete, Makamba na Chiligati kabla ya kutoa uamuzi waliofikia? Kama walishauiriana, kwa nini wanaanika ngua zao za ndani hadharani?
Kama walishauriana, kipi kinachompa ujasiri Masha hadi kuamua kupigana na mwamba? Nani aliyemhakikishia usalama wake kisiasa na kimasilahi?
Akiongea kwa kujiamini, Masha alisema kwa mujibu wa nyaraka zilizopo na taarifa zilizofikia wizara yake. "….suala la uraia wa Bashe halina utata."
Katika maelezo yake, Masha anasema Bashe ni raia halali wa Tanzania, tena wa kuzaliwa. Hili nalo lina utata. Hata Bashe anajua hilo; kwamba si raia wa kuzaliwa.
Masha anajua kuwa wakati Bashe anazaliwa, baba yake mzazi alikuwa hajaomba uraia. Alikuwa raia wa Somalia. Alipoomba uraia wa Tanzania, hakumuingiza Bashe katika maombi aliyowasilisha katika fomu zake za kuomba uraia.
Aidha, Bashe mwenyewe amekana uraia wa Somalia akiwa na miaka 25.
Kama haya ndiyo maelezo ya Bashe, kwamba baba yake alipoomba uraia hakumuingiza yeye katika maombi yake; hiki ambacho Masha anaita "Bashe raia wa kuzaliwa" kinatoka wapi? Kinalenga nini?
Kama Bashe hakuzaliwa Tanzania, na baba yake hakuzaliwa nchini na hata wakati anaomba uraia, Bashe akiwa na miaka kumi; nani basi raia wa kuzaliwa? Je, Masha amelenga nani na kwa faida ya nani?
Kama Kikwete anasema Bashe si raia, huku Masha anasema tofauti, nani aaminike na yupi apuuzwe? Inawezekana Masha anajua vema nani anamtumikia, lakini siyo rais Jakaya Mrisho Kikwete na serikali yake.
Ingekuwa Masha anamtumikia Kikwete, waziri na rais wasingepanda gari moja, lakini wakaelekea tofauti. Ama watateremka na kila mmoja aende zake, au mmoja atabaki kwenye gari.
Lakini ukiyatafsiri vema haya utayafupisha kwa kauli hii: Kikwete ana serikali mbili. Zipi? Serikali anayozunguka nayo na nyingine iliyo kivulini.
Katika nchi zote ambako rushwa imekomaa na ufisadi umekuwa dini, dola linakuwa na sura mbili. Serikali mbili, mabunge mawili na mahakama mbili.
Kunakuwa na waasi wasioonekana kama majini ya Sheikh Yahya Hussein. Wanabaki kivulini.
Watatenda bila kuafikiana na wanaishi kwa kuviziana na kuzomeana. Hatimaye aliyeko kivulini anaangusha serikali iliyo wazi na iliyochaguliwa.
Wakati siyo rahisi kujua Masha yumo katika serikali ya dola lipi, katika hali ya kawaida, asingeweza kwenda kinyume na Kikwete, kama asingeweza kuwa na uhakika wa usalama wake kisiasa………..
……..Uamuzi wa masha wa kujitosa kumtetea Bashe, hata kwa kauli zenye utata, unachukuliwa na wengi kuwa njia ya kuonyesha kuwa ana msuli wa nje kuliko wa ndani ya serikali ya Kikwete…….
Kitendawili cha uraia wa Hussein Bashe, mgombea ubunge Nzega (CCM) aliyoenguliwa kimeibua mapya.
Wiki iliyopita, Waziri wa mambo ya Ndani, Lawrence Masha aliutangazia ulimwengu kuwa Bashe ni raia halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akahoji, "nani mwenye mamlaka ya kusema Bashe si raia? Nikiwa waziri mwenye dhamana nasema, Bashe ni raia halali na hakuna atakayebadilisha uamuzi huu."
Aliyesema kuna utata katika uraia wa Bashe ni Rais Jakaya Kikwete, tena ndani ya vikao halali vya chama chake.
Taarifa zinasema, ndani ya ukumbi wa mkutano Kikwete alisimama kidete kutetea hoja yake kwamba Bashe si raia. Alisema amepata ‘taarifa za vyombo vya usalama' zinazothibitisha utata wa uraia wa Bashe.
Wengine walioendeleza kauli ya rais ni viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Katibu Mkuu Yusuf Makamba na Katibu Mwenezi John Chiligati.
Masha amenukuu vifungu kadhaa vya sheria ya uhamiaji akisema vinahalalisha uraia wa Bashe.
Kwa mfano, ananukuu vifungu Na. 5(1) na Na. 7(8) vya Sheria Na. 7 ya uraia ya mwaka 1995 na kusema, "Bashe ni raia halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tena kwa kuzaliwa." Anasema tayari amemjulisha Bashe kuhusu uamuzi huo.
Je, Masha hakushauriana na Kikwete, Makamba na Chiligati kabla ya kutoa uamuzi waliofikia? Kama walishauiriana, kwa nini wanaanika ngua zao za ndani hadharani?
Kama walishauriana, kipi kinachompa ujasiri Masha hadi kuamua kupigana na mwamba? Nani aliyemhakikishia usalama wake kisiasa na kimasilahi?
Akiongea kwa kujiamini, Masha alisema kwa mujibu wa nyaraka zilizopo na taarifa zilizofikia wizara yake. "….suala la uraia wa Bashe halina utata."
Katika maelezo yake, Masha anasema Bashe ni raia halali wa Tanzania, tena wa kuzaliwa. Hili nalo lina utata. Hata Bashe anajua hilo; kwamba si raia wa kuzaliwa.
Masha anajua kuwa wakati Bashe anazaliwa, baba yake mzazi alikuwa hajaomba uraia. Alikuwa raia wa Somalia. Alipoomba uraia wa Tanzania, hakumuingiza Bashe katika maombi aliyowasilisha katika fomu zake za kuomba uraia.
Aidha, Bashe mwenyewe amekana uraia wa Somalia akiwa na miaka 25.
Kama haya ndiyo maelezo ya Bashe, kwamba baba yake alipoomba uraia hakumuingiza yeye katika maombi yake; hiki ambacho Masha anaita "Bashe raia wa kuzaliwa" kinatoka wapi? Kinalenga nini?
Kama Bashe hakuzaliwa Tanzania, na baba yake hakuzaliwa nchini na hata wakati anaomba uraia, Bashe akiwa na miaka kumi; nani basi raia wa kuzaliwa? Je, Masha amelenga nani na kwa faida ya nani?
Kama Kikwete anasema Bashe si raia, huku Masha anasema tofauti, nani aaminike na yupi apuuzwe? Inawezekana Masha anajua vema nani anamtumikia, lakini siyo rais Jakaya Mrisho Kikwete na serikali yake.
Ingekuwa Masha anamtumikia Kikwete, waziri na rais wasingepanda gari moja, lakini wakaelekea tofauti. Ama watateremka na kila mmoja aende zake, au mmoja atabaki kwenye gari.
Lakini ukiyatafsiri vema haya utayafupisha kwa kauli hii: Kikwete ana serikali mbili. Zipi? Serikali anayozunguka nayo na nyingine iliyo kivulini.
Katika nchi zote ambako rushwa imekomaa na ufisadi umekuwa dini, dola linakuwa na sura mbili. Serikali mbili, mabunge mawili na mahakama mbili.
Kunakuwa na waasi wasioonekana kama majini ya Sheikh Yahya Hussein. Wanabaki kivulini.
Watatenda bila kuafikiana na wanaishi kwa kuviziana na kuzomeana. Hatimaye aliyeko kivulini anaangusha serikali iliyo wazi na iliyochaguliwa.
Wakati siyo rahisi kujua Masha yumo katika serikali ya dola lipi, katika hali ya kawaida, asingeweza kwenda kinyume na Kikwete, kama asingeweza kuwa na uhakika wa usalama wake kisiasa………..
……..Uamuzi wa masha wa kujitosa kumtetea Bashe, hata kwa kauli zenye utata, unachukuliwa na wengi kuwa njia ya kuonyesha kuwa ana msuli wa nje kuliko wa ndani ya serikali ya Kikwete…….