Mapya CHADEMA, video zaidi zanaswa

Mapya CHADEMA, video zaidi zanaswa

Hicho chanzo chenyewe kishakuwa bias na hivyo kimepoteza umaana wa kuitwa chombo huru cha habari,
kipumzike kwa amani
Huko mtanzania si ndio kulikuwa na thread hapa juzi ikisema wale akina Yuda Iskariot(juliana na Mtela) walipeleka taarifa zao za kupikwa???
 
Huu upumbavu mtupu badala ya kutatufuta jinsi ya kujinasua kwenye taifa tegemezi au jinsi ya kulinda wanyama wetu wanaouliwa kila siku na majangili tunakimbizana na Cd fake kwanini kama kweli walikuwa wanaona hizo njama zikipangwa wasing'etoa taarifa polisi hao wahusika wakakamatwa siku hiyo hiyo je wang'ekuwa wamefanikisha na kusababisha vifo wangetuambia ushaidi upo studio?
 
Kwa namna moja au nyingine, CHADEMA inahusika na hizi tactics za utekaji. Wengine mnasema feki, wengine mnasema siyo feki ila alirubuniwa na wengine mnasemna siyo kosa kujadili.
 
Hizi zinaonyesha makada tu?, za kuwaonyesha mbowe na slaa bado ziko mitamboni?
 
Mwigulu anajitaftia sifa za kishamba ambazo hazitamsaidia zaidi ya kuosha upumbavu wake
 
tukio la kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa lwakatare limeibua mapya ndani ya chama hicho yaliyojificha mbali na video ya lwakatare inayomuonesha akipanga mipango ya kuteka na kuzuru watu pia imebainika kuwa kuna video zingine ambazo zimewasilishwa kwenye vyombo vya uchunguzi zikionesha viongozi wa chadema wakipanga mipango zaidi ya mauaji kwa baazi ya watu muhim wakiwemo wanahabari na watu wengineo wanajf hawa wanasiasa wanatupeleka wapi?
 
Hapana sijakurupuka mkuu,hebu rudia tena kuisoma habari yake kama utamwelewa! Au mkuu labda sijaona vizur,anaposema video zinawaonyesha makada wa chama....halafu huko mbele anasema ambao hawajajulikana...sasa alijuaje ni makada wa chama ilihali 'hawajajulikana'?soma hapo anaposema na watu wengine sita...
Makada wa chama na watu wengine wasiojulikana.
 
zikowapi sasa hizo video mpya tuanze kuzichambua locally kama ni feki au laa?
maana wataalamu sikuhizi pia wanatumika kudanganya
 
Hela za Swiss pembeni, EPA, wanyama wetu kuibwa hadi kupitishwa airport, Tembo kuwawa na bado wanaendelea kuwawa, serekali yenye vituko kuliko serekali yoyote duniani kote inayowanyanyasa wananchi wake bila kosa, kuwaua, kuwaadhibu na hata kuwawekea upofu wa maisha, mikataba feki kama hiyo 19 iliyosainiwa juzi tukaambiwa itawekwa wazi ndo wameishia mitini. Where are we going? Watanzania tuamke wote tuseme enough is enough, ona majirani zetu wakenya wasivyopenda mambo ya kuhisi kama watz na hawa wenzetu ndo wametuacha hivyo. Tusipoamka serekali hii ya kigaidi na yenye kuwanyanyasa wananchi wake itatumaliza sote. Tuchukue hatua. Pasaka njema
 
Mwigulu michembe anatakiwa ajue kwamba hapambani na chadema bali anapambana na umma,anajichimbia kaburi lake kisiasa
 
Hicho chanzo chenyewe kishakuwa bias na hivyo kimepoteza umaana wa kuitwa chombo huru cha habari,
kipumzike kwa amani

utaifa kwanza wewe waonekana ni mmoja wa wanaolipwa na muandaaji wa mkanda,subiri nawe ununuliwe kwa elfu 50.nakusikitikia kijana wewe,
 
Ngoja nimalize bia yangu nitarudi baadae...naona wanatujaza story za uchafu akilini...sh*t..!
 
Kuanzia sasa tutaona video nyingi sana, msishangae hata za ccm zitaanza kutoka. Kwa teknolojia ya IT Watu wengi watawacheza shere watanzania! Kutengeneza video sio kazi! Time will tell us!
 
Usikurupuke soma habari vizuri kasema makada wa CDM na watu wengine wasiojulikana. Vp bana mbona ushabiki ni zaidi kuliko hoja kuwa mpole kaka acha jazba!
 
Kweli CCM vichaa, sijui walimchaguaje huyu Mwigulu kuwa kiongozi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom