Mapungufu ya Kikwete: Constructive Criticisim!


Pasco, hapa ninataomba msaada zaidi.... Raisi kuzima swala la EPA, kwa nini tuseme/tuone ni moyo wa HURUMA na si CORRUPT HEART?
Mtu kama Rais si anaapa kuilinda Katiba ya nchi na Katiba imetoa msimamo wa wazi juu ya hatua za kumchukulia mwizi wa kuku na mwizi wa EPA? sasa rais anatoka wapi kuingilia Katiba kwa kuhurumia mwizi wa EPA? Je haya si mambo yanoweza kumfanya baadae akawa kama Mubaraka? Mtu anayempenda mwenzake umwambia ukweli na ukweli kwa raisi wetu, Ndugai na wote wa jinsi hii ni kwamba mambo yanabadilika sana!! mfano mzuri ni chales Taila na Mubaraka
 
ukiwa kiongozi dhaifu na ukathibitika kweli wewe ni dhaifu basi hata uongozi wako utakuwa legelege daima,na hata wasaidizi utakaokuwa nao hawayakuwa tofauti na wewe,JK ni dhaifu kiuongozi na hilo sio suala la kujadili hapa.tusubiri tu hiyo miaka 3 iishe huku nchi ikiendeshwa kama hamna watu makini wa kuiongoza
 
Pasco na jouneGwalu,
Naomba turejee kwenye hii Makala. Iliandikwa na Rafiki yangu Ansbert Ngurumo tarehe 23/11/2008 akiwa hapa Uingereza masomoni.


Mwisho wa kunukuu!

TUMBIRI (PhD, University of Hull, UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Wakati mwingine huwa najiuliza sana, huenda huyu bwana (JK)hana akili timamu!

 
critic nyingine kwa rais wa Nne ni kutokumulika kwa karibu kule katika halmashauri zetu hapa nchini,ambako ndio fedha za watanzania zinapotea bila habari.wale aliowatimua juzi ni trela tu.azimulike halmashauri kule ndio kuna uozo uliotukuka


Aidha mimi rais wa tano,namshauri akumbuke ahadi yake kwa watanzania kuwa "IM SMILING BUT FIRM IN SERIOUS ISSUES"
 
kasoro nyingine ya Mh rais wa Nne ni kuwaamini wasaidizi wake kwa asilimia mia moja,hii ni dosari kubwa sana.

Rais wa tano nasema hili si lakufumbia macho.akumbuke kuwa hakuna binadam aliekamilika asilimia zote,hivyo ajitahidi kuwa anawakumbusha mara kwa mara wafanye kazi kwa kuzingatia misingi ya sheria na taratibu pamoja na kujali haki na wajibu.
 
jadi..umeshasema binadamu tunamapungufu, sasa nayy c ndo pungufu lake au umemtoa kwny ubnadam?
 
H wana JF. kumbe inafaa kusoma kwa makini kabla ya kuchangia. All the best!
Mkuu Baba Gaston, kwanza karibu sana jf, pili hongera kwa kukubali kuwa mvumilivu wa kutafuta ufahamu kwanza, kabla hujaanza kuchangia, natamani wana jf wengi wangekuwa kama wewe, mautumbo mengi humu jukwaani yangepungua!.
 
Mkuu Omukajunguti, lets be fair, hivi ulitaka rais wako afanya nini zaidi hiki alichofanya?, njia si ameshatonyesha ya kuelekea kwenye maisha bora?, au unataka akubebe mpaska akufikishe hapo?. Anayeshindwa kufikia maisha ni aliyekuonyesha njia au aliyeshindwa kufika?.

Si tumemchagua wenyewe?, na baada ya miaka mitano, tukaridhika na utendaji wake, tukamuongezea mingine!. Hi kiukweli ukishachaguliwa kuwa kiongozi unajipima mwenyewe au unapimwa na waliokuchagua?. Kama sisi tuliomchagua mwanzo na baada ya miaka mitano tukampima tukamuona anaweza, tukamuongezea, wewe ni nani wa kumuuliza ajipime na kuwapisha wengine?.

Hivi katiba yetu ndivyo inavyosema tukishamchagua rais, ajipime, akijiona hawezi apishe?.
 


Mkuu unachosema ni kweli, lakini tatizo ni kwamba ukiangalia mazingira ya kisiasa ya Tanzania, mtu akichaguliwa na CCM kugombea urais ni kama automatic anakuwa Rais, hata kama wengine hawakumtaka. Wananchi tunategemea rais aweke mazingira na njia zinazoweza kutumiwa kwa haki na watu kuiendeleza. So far JK na serikali yake wameshindwa katika hilo. Walichofanya ni kwamba wanatumia njia wanazoweza kuzitumia kuwawekea fursa watanzania kwa manufaa yao binafsi. Huko ni kuwa na uwezo wa kujineemesha na kutokuwa na uwezo wa kuendeleza nchi na wananchi.

Kuna maswala mengi ambayo tunaweza kumjudge Kikwete na serikali yake. Tuangalie macheche....kesi ya akina Zombe, mpaka sasa hakuna kinachoendelea kesi imetupwa, hadi siku ndugu watakapoamua kuchukua sheria mkononi. Kumbuka keshi ya Dito iliendeshwa kihuni huni tu...kuna mifano mingi.

Angalia issue ya EPA, Kagoda, Kiwira, Radar, ndege ya Rais, Richmond etc etc etc...yeye kama rais anatakiwa kushughulikia maswala haya, hata kama mengine hayakutokea wakati wa utawala wake. So far inaonekana kuwa yote hayo hajashughulikia na hana nia au hana uwezo wa kuyashughulikia.

CCM kama chama kwa sasa kiko in shambles, kila mtu ni msemaji ni muongeaji, cabinet same same waziri huyu anasema hili mwingine anasema lile.......manaibu waziri sasa wanaonekana kuwa ni play boys, hakuna nidhamu na maadili.

Uchumi nadhani kila mtu anaweza kuwa shahidi hakuna haja ya kuelezea.

Tunatakiwa kukumbuka kuwa unapoamua kudeligate power ujue kuwa, yule unayempaka kazi akifanya vizuri credit ni kwako, lakini akifanya ovyo responsibility bado iko kwako. Kusema kuwa washauri wa JK ni wabaya it is absolutely **** since those washauri are his appointees. It is only an idiot who will argue in that line, because the government bureaucracy does not work that way.

Ni kweli naibu waziri akichukua changudoa au akifumaniwa, au Waziri Mkuu akiongopa, au baraza zima la mawaziri kutokuwa na nidhamu, kweli si kosa la rais, lakini anawajibika moja kwa moja kutokana na kuteua madudu, na kuchangia kwa kiasi kikubwa kuteua watu ovyo, na bila kuweka rules za kulinda integrity ya serikali, the responsibility goes all the way up to the top. Tumesikia mara nyingi Obama akisema "as commander in chief the responsibility is mine", Bush alipoingia mkenge wa kusema Iraq inasilaha za sumu na kufanywa asome maneno ya uongo, alisema wajibu ni wake. McCain alaiposhindwa urais kutokana na chaguo baya la VP, hakumlaumu Steve kwa kumchagulia S Palin, alisema kuwa ni yeye ameshindwa. Kuna mifano mingi tu. Kwa hiyo hoja ya kuwalaumu washauri, wasaidizi, na aliowateua ni ufinyu wa akili.

We may have voted for JK, we may have voted for CCM, but that does not change the fact that there is a big mess that needs cleaning. Let's call mess a mess, not a miss.
 
"Mfano wa kwanza wa udhaifu huu wa huruma uliyopitiliza ni pale alipoyasamehe yale majizi ya EPA kwa kuyaruhusu yarudishe fedha yalizo kwiba kwa exchange ya kusemehewa na kutofikishwa mahakamani!. Hata Spika Sitta pia alimlaumu rais JK kwa upole huu!. Lingekuwa ni bunge makini, imperchment process ingeanzia pale pale right away kwa sababu rais hana mamlaka ya kuizuia sheria kuchukua mkondo wake!, huu ni uvunjaji wa katiba ya JMT!."

MTOA mada asante kwa ku post hii. Lakini npenda kusema kuwa katika mfumo wa uongozi uliopo Tz ni vigumu rais aliyeko madarakani kutenda vile anavyotaka kwa sababu rais aliyepita nyuma yake anakuwa bado na mamlaka nyingi tu: mojawapo ni kuwa na ukaribu zaidi na viongozi wa vyombo vya dola, mbili ni kuwa na timu kubwa ya watendaji watekelezaji wa majukumu kwenye nyidhifa nyeti (wakurugenzi). hawa ndo watekelezaji wa majukumu ya kila siku ya serikali. kwa mtindo huo rais aliyeko madarakani anakuwa hana ubavu wa kuporomosha maswahiba wa rais aliyeondoka labda awe kichaa fulani. JKN aliweza kwa sababu waliondoka hawakupendwa (wakoloni)
Suala la EPA- siyo rais hivyo, kwani waliohusika walikuwa ni mawahiba wa rais Mkapa ndo kipindi ambacho ufisadi huo ulipotokea na yeye kuhusishwa na KIWIRA- wanaharakati walipohoji JK akasema " mwache mzee wetu apumzike kwa amani" kwani nini kauli hii? wenye akili alijua sababu yake-Kulindana. JK angechukua maamuzi makali -hata BM angejikuta anahusika. HAwakutaka haya yabainike.
kikatiba rais ndo mtendaji wa mwisho lkn ikitumika vibaya nchi itayumba tu, lkn pia isipotumika nchi itachechemea kama hivi sasa.
USHAURI: Kama nchi ni lazima tuwe na msimamo wa kitaifa-hakuna kulea ubovu wa mkubwa aliyepita-ikibainika achukuliwe hatua hata za kimahakama. Hii itawafanya watendaji kuwa waoga hivyo kuwa wadilifu. wataogopa kutenda ufisadi kwa kuw ahakuna kigogo cha kuegemea pindi mambo yakifumuka. HUU NDO UKWELI.
Tazama influence ya JKN wakati wa utawala wa AHM. Uhuru wa rais ulikuwa wapi? Mikonini mwa JKN. Hii ndo Tz. Katiba mpya utumike kuweka wazi kuwa ubaya/uovu wowote ukitendwa mtendaji bila kujali nafasi yake atapambana na mkono wa sheria. Nchi itanyooka. Sababu ya viongozi wakubwa kumiliki maeneo wasiyomudu kuyatunza kwa kisingizio cha kuandalia maisha watoto na wajuu wake, kitaisha, uadilifu utarudi bila kushikiwa fimbo
 
Kwa nini ahurumie majizi asihurumie wananchi maskini walioibiwa hizo fedha na walistahili kupatiwa huduma kwani hawawezi hata kupata mlo wa siku na huduma nyingine za kijamii
 
tatizo kubwa kwa nchi yetu ni 1!! tunaongozwa na sera za vyama lakini hatuna sera za nchi ambazo zinauwajibikaji na utekelezaji!! pia kama ua vission na mission usipotekeleza anayekuwajibisha ni nani!1 taifa letu bado lina changamoto nyingi nduguzanguni!1 lazma tuwe na sera ya nchi ili kila kiongozi anayeingia madarakani aifuate na akishindwa kufulfil anatakiwa ajiuzulu pia attupe dedline ya kuflfill ahadi zake!!
 
Kwa kifupi JK aliingia madarakani kwa nguvu ya watu wengine akina EL, ROSTAM na wenzao. Hao ndio waliokuwa na Maono yao wenyewe na wala si ya JK. Baada ya kulazimishwa kuachana nao ndio ukawa mwisho wa 'maono na mtazamo' wa JK!
 
Kwani mnafikiri JK hafahamu kinachoendelea!!!!!?? Anafahamu sana lakini atafanya nini endapo mtandao wake ndo unaomtesa?? Wakati wa uchaguzi aliwaona watu wazuri (kwa vile walimsaidia kuingia ikulu) na hivyo kulipa fadhila, sasa wanaboronga na hana namna ya kufanya.

Ushauri wangu kwa waTZ ni kufikiria namna gani tutajikwamua kuanzia 2015 na si sasa kwani TUMEKWISHACHELEWA (It is too late). Yote yanayoendelea anayafaham ila hata yeye hana namna, ni sawa na kuona nyumba yako inaungua moto halafu unataka kuuzima kwa maji ya ndoo!!!
 
inawezekana huyu jamaa naye ana mambo yake mabaya hivyo hawezi kuwashtaki wanachama wake ktk uhalifu maana watamtaja.
 
mimi ninaamini hakuna mtu asiye na makosa! lakini yakizidi kipimo hugeuka na kuwa zigo zito. kama ulifumaniwa unakwiba mke ya m2 na wewe mwenyewe akamfumania yule aliyekufumania jana anakwiba ya kwako. Hauwezi kumwajibisha maana utasutwa. Hii ndo mambo yanayomsumbua mkulu
 
"Asiyekubali kushindwa si mshindani"
Inaonekana wanaume tunaendekeza sana kujuana na undugu usiokuwa na Tija.
Wanaume sasa tumeshidwa kuendesha hii nchi, inabidi sasa tujaribu kuikabidhi kwa mwanamke kama walivyofanya Malawi ili tuone kama mabadiliko yatakuwepo.

Tunao wanawake ambao ni wasomi na wasiokuwa na mzaa kazini ambao naamini wanaweza kuleta mabadiliko ya haraka katika mfumo mzima wa uongozi hasa wa kiutendaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…