DR.MBWEMBWE
Member
- Nov 27, 2012
- 19
- 20
KAMA ULIKALILI TU MAANDIKO KAA PEMBENI HAUKUHUSU
Kama mafundisho ya Dini yanatuambia kuwa Mungu ananijua kabla hata sijazaliwa, maana yake anajua kila kitu ninachofanya na hadi nitakacho fanya baadae (kwa future)
(A) Maana yake mimi siwezi kwenda kinyume na anachokijua Mungu, sasa hii kauli ya kusema nimetenda kinyume na mapenzi au mpango wake inatokea wapi? Kwani kabla sijatenda je alijua kama nitatenda kinyume na mapenzi au mipango yake? (NDIYO/HAPANA) k
(B) Kama alijua kabla sijazaliwa kuwa nitatenda kinyume na mapenzi yake sasa kwanini kama nikitenda kinyume na mapenzi au mipango yake anachukia? Na kama hakujua kama nitatenda kinyume basi je kwanini anaitwa Mungu mjua vyote?
Swali jingine
(C) Je, kuna mtu anaweza kubadilisha mapenzi au mipango ya Mungu? (NDIYO/HAPANA)
kama ni jibu ni NDIYO kipengele C litazaa swali hili
(D) Je, huyo Mungu ambaye anakujua kabla hujazaliwa je alijua before kuwa utakuja kubadili mapenzi au mipango yake? (NDIYO/HAPANA)
Kama jibu ni HAPANA kipengele C basi huyo Mungu hastahili kupewa sifa ya mjua vyote.(Omniscient)
Kama jibu ni NDIYO kipengele D. Maana yake ni kwamba bado hujabadili alichokuwa anajua. Sasa kama huwezi je kwanini unapoteza muda kumuomba akusaidie kutatua matatizo yako? Maana hata ukiomba na kulia kwa machozi ya damu hawezi kubadili mpango wake juu yako.
Kama jibu ni HAPANA kipengele D. Maanake huyo Mungu hakujua kuwa utabadili mipango yake.
Huyu Mungu wa kwenye Hivi Vitabu hii sifa ya kuwa yeye ni mjua yote, hapana sio mjua yote, hata maandiko ya hivyo vitabu yanadhihirisha kuwa yeye si mjua yote.
Mjua yote hawezi kuwa na hasira maana hasira inakuja pale unapopata au kufanyiwa kitu ambacho hukutarajia, hukujua.
Sasa cha kushangaza hadithi za hivyo vitabu vinadhihirisha kuwa huyo Mungu kuna wakati alipatwa na hasira, ghadhabu, hata kukata tamaa.
Rejea
Kutoka 32:10
Mwanzo 6:6
Ukihitaji rejea nyingine nifahamishe.
AMKENI MJITAMBUE
IMEANDALIWA NA FRANK A. CHALE
Kama mafundisho ya Dini yanatuambia kuwa Mungu ananijua kabla hata sijazaliwa, maana yake anajua kila kitu ninachofanya na hadi nitakacho fanya baadae (kwa future)
(A) Maana yake mimi siwezi kwenda kinyume na anachokijua Mungu, sasa hii kauli ya kusema nimetenda kinyume na mapenzi au mpango wake inatokea wapi? Kwani kabla sijatenda je alijua kama nitatenda kinyume na mapenzi au mipango yake? (NDIYO/HAPANA) k
(B) Kama alijua kabla sijazaliwa kuwa nitatenda kinyume na mapenzi yake sasa kwanini kama nikitenda kinyume na mapenzi au mipango yake anachukia? Na kama hakujua kama nitatenda kinyume basi je kwanini anaitwa Mungu mjua vyote?
Swali jingine
(C) Je, kuna mtu anaweza kubadilisha mapenzi au mipango ya Mungu? (NDIYO/HAPANA)
kama ni jibu ni NDIYO kipengele C litazaa swali hili
(D) Je, huyo Mungu ambaye anakujua kabla hujazaliwa je alijua before kuwa utakuja kubadili mapenzi au mipango yake? (NDIYO/HAPANA)
Kama jibu ni HAPANA kipengele C basi huyo Mungu hastahili kupewa sifa ya mjua vyote.(Omniscient)
Kama jibu ni NDIYO kipengele D. Maana yake ni kwamba bado hujabadili alichokuwa anajua. Sasa kama huwezi je kwanini unapoteza muda kumuomba akusaidie kutatua matatizo yako? Maana hata ukiomba na kulia kwa machozi ya damu hawezi kubadili mpango wake juu yako.
Kama jibu ni HAPANA kipengele D. Maanake huyo Mungu hakujua kuwa utabadili mipango yake.
Huyu Mungu wa kwenye Hivi Vitabu hii sifa ya kuwa yeye ni mjua yote, hapana sio mjua yote, hata maandiko ya hivyo vitabu yanadhihirisha kuwa yeye si mjua yote.
Mjua yote hawezi kuwa na hasira maana hasira inakuja pale unapopata au kufanyiwa kitu ambacho hukutarajia, hukujua.
Sasa cha kushangaza hadithi za hivyo vitabu vinadhihirisha kuwa huyo Mungu kuna wakati alipatwa na hasira, ghadhabu, hata kukata tamaa.
Rejea
Kutoka 32:10
Mwanzo 6:6
Ukihitaji rejea nyingine nifahamishe.
AMKENI MJITAMBUE
IMEANDALIWA NA FRANK A. CHALE