Mapungufu ni mengi sana kwenye siku ya wananchi, burudani za hovyo na kiingilio kikubwa vyapunguza mashabiki

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,731
218,312
Nimefuatilia Siku ya Yanga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa , kiukweli haikufana kama ilivyotarajiwa , sielewi hasa kilichotokea , lakini kukosekana kwa Haji Manara kunaweza pia kuwa kumechangia kukosekana ama kupunguza Shamra shamra kwa kiasi fulani , Maulid Kitenge na Zembwela hawakutosha kuongoza shughuli ile kubwa , hawana mvuto , hasa baada ya kashfa ya Mkataba wa Bandari , hawaaminiki tena .

Wako wengine waliodai kwamba Ukubwa wa kiingilio ni sababu muhimu ya uwanja kupwaya , hasa ikizingatiwa anguko kubwa la Uchumi wa Wananchi wa Tanzania na hasa Wakazi wa Temeke , hili Yanga wanapaswa kujifunza , si rahisi kwa mtu aliyeshindia mihogo au chai kavu ya Rangi kulipa kiingilio cha tsh elfu 10 .

Jambo lingine lililodororesha siku ya Mwananchi ni Kukosekana kwa burudani bora ya Muziki , hasa baada ya Wasanii Wahuni kupewa nafasi ya kuimba nyimbo zenye matusi , labda kwa faida ya wengi ni kwamba kwenye kadamnasi kama ile , Burudani ni sehemu muhimu mno , uwanja ule ulikuwa umejaa watu wengi wazima sana , kualika Wasanii Wahuni wanaoimba matusi bila kujali walio mbele yao , kulikatisha tamaa wadau wengi waliokuwa wanaangalia kwenye TV na kuwafanya waendelee kubaki nyumbani , hapa ndipo wanamuziki wa Congo wanapowazidi wasanii wa kibongo , watu wengi wanapenda burudani , hawataki matusi na lugha za hovyo , Kwa hili Yanga Mmefeli sana , mbona bado nchi hii ina wasanii wakali wengi tu , kwanini mmetuletea Takataka hizi leo ?

Wakati mwingine mnapoandaa mambo haya chukueni ushauri wa wadau wa burudani , ukichagua msanii kwa sababu ana followers wengi Instagram au Twitter utapotea .
 
Kikubwa ni bei ya kiingilio mkuu, kiingilio cha 10k ni mtihani. Hata Derby za Simba na Yanga, kiingilio cha chini kikiwa 7,000 huwa uwanja haujai saana ila ikiwa 5,000 ni lazima kutapike.
Aiseeeee !!!
 
Nimefuatilia Siku ya Yanga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa , kiukweli haikufana kama ilivyotarajiwa , sielewi hasa kilichotokea , lakini kukosekana kwa Haji Manara kunaweza pia kuwa kumechangia kukosekana ama kupunguza Shamra shamra kwa kiasi fulani , Maulid Kitenge na Zembwela hawakutosha kuongoza shughuli ile kubwa , hawana mvuto , hasa baada ya kashfa ya Mkataba wa Bandari , hawaaminiki tena .

Wako wengine waliodai kwamba Ukubwa wa kiingilio ni sababu muhimu ya uwanja kupwaya , hasa ikizingatiwa anguko kubwa la Uchumi wa Wananchi wa Tanzania na hasa Wakazi wa Temeke , hili Yanga wanapaswa kujifunza , si rahisi kwa mtu aliyeshindia mihogo au chai kavu ya Rangi kulipa kiingilio cha tsh elfu 10 .

Jambo lingine lililodororesha siku ya Mwananchi ni Kukosekana kwa burudani bora ya Muziki , hasa baada ya Wasanii Wahuni kupewa nafasi ya kuimba nyimbo zenye matusi , labda kwa faida ya wengi ni kwamba kwenye kadamnasi kama ile , Burudani ni sehemu muhimu mno , uwanja ule ulikuwa umejaa watu wengi wazima sana , kualika Wasanii Wahuni wanaoimba matusi bila kujali walio mbele yao , kulikatisha tamaa wadau wengi waliokuwa wanaangalia kwenye TV na kuwafanya waendelee kubaki nyumbani , hapa ndipo wanamuziki wa Congo wanapowazidi wasanii wa kibongo , watu wengi wanapenda burudani , hawataki matusi na lugha za hovyo , Kwa hili Yanga Mmefeli sana , mbona bado nchi hii ina wasanii wakali wengi tu , kwanini mmetuletea Takataka hizi leo ?

Wakati mwingine mnapoandaa mambo haya chukueni ushauri wa wadau wa burudani , ukichagua msanii kwa sababu ana followers wengi Instagram au Twitter utapotea .
Usilete siasa kwenye starehe, mpira ni starehe na starehe ni gharama.

Kwenye show za muziki watu huwa wanalipia kiingilio kwa meza ya watu 10 shilling million 1.

Usidhani wachezaji wanasajiliwa kwa ruzuku za Chadema au join the chain.
 
Back
Top Bottom