Mapungufu katika Wimbo wa Taifa la Tanzania

Lakini pia tatizo kubwa tulilinalo mbele ya watu wa dunia nyingine Ni uafrica kwanza ndipo Tanzania.Yaani ukitaja wewe ni Mwafrica mtu hana haja ya kuuliza nchi gani.Moja kwa moja mtu hategemei jema kutoka kwako.Na hii ni kwasababu Africa tu wamaskini wa kila kitu yaani hadi upendo tunauwana ovyo. Nadhani Mungu akianza kwa kubariki Africa Then Tanzania ni jambo jema zaidi.Kumbuka Tanzania imo Africa kwaiyo mungu anaweza kuanzia hata Tanzania.


Asante kwa hoja zako, Naomba kupingana na wewe, Mimi nadhani ni muhumu kuiweka Tanzania mbele kama tai katika kila kitu, Charity begins at home.

Sijui ni kwa nini tumekua na hii kasumba ya kuwatanguliza wageni na kuona ni wa maana kuliko sisi watanzania wenyewe. Nadhani sisi ndio nchi pekee duniani yenye kasumba hii ya kuthamini wageni kuliko wananchi wake.

Ninaposema hivi simaanishi kuwachukia wageni, La hasha nina maanisha kuwathamini watanzania na kuwaenz, kuwajengea moyo wa uzalendo n.k. Kama sisi wenyewe tusipojithamini ndani ya nchi yetu ni nani atakaayetujali?

Kwa nini unataka Mungu aanza kuibariki Afrika na sio Tanzania? Kwanini asianzie kuibariki Tanzania na baraka zikifurika zimiminikie katika nchi nyingine za kiafrika? Kwanini unadhani sisi hatustahili na wanaostahili ni wengine kwanza?
Huoni kwamba wewe umeshajitolea mhanga kubaki maskini kwanza mpaka wengine wapate ndio na wewe upate?
 
Huo wimbo hasa baada ya kukaa nje ya Tanzania unaniudhi sana, kwa sababu unataja na kusifia Africa wakati wenzetu wengi wa Afrika wala huwa hawakumbuki nchi nyingine za Afrika. Ukombozi uliisha sasa ni kuubadili na kusema yetu ya Tanzania full stop.

Mambo mengine ni ya kurekebisha hapa na pale. Tunapenda uafrika lakini Afrika hawatupendi kwa hiyo tujipende wenyewe.
Mapungufu ya jirani yasitufanye tuharibu vipaji vyetu. Kukosa upendo kwa jirani yetu kama ni kweli (kwa utafiti wako) sio kibali cha sisi kuchukia kila kitu kinachotuunganisha na waafrika wenzetu. Napendekeza tuendelee kuwapenda ili nao wajifunze kutoka kwetu na waone ni kitu kizuri, kwa kawaida mtu mwenye upendo wa kweli hachoki.
 
mbona hata huo mnaouchambua utafutwa kuupisha wa afrika mashariki?
 
Nimekua nikitafakari Wimbo wetu wa taifa nikabaini kua una mapungufu kadhaa ambayo aidha yangetakiwa yarekebishwe au kutafuta wimbo mbadala.


Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Pili naona kwamba wimbo wetu haumjali mtanzania na wala haumpi kipaumbele hata kidogo, Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba mambo baraka kwa mtanzania zimetajwa katika beti la pili, badala ya kuwa Beti la kwanza. Hii ni aibu na laana kwa watanzania. Tunajilaani wenyewe kwa kuwajali wageni kuliko sisi watanzania. Bahati mbaya hali hii imekua kama self fulfilling prophecy, ndio maana wageni wanatetemekewa na wenyeji wanaonekana mafala ndani ya nchi yao.

Huu wimbo umepitwa na wakati, Unazungumzia kudumisha uhuru wakati hakuna nchi inyotawaliwa sasa hivi. Ilikua sawa wakati wa kupigania uhuru na kipindi cha ujamaa kuwa na wimbo kama huu lakini sasa mambo yamebadilika, nchi zote zimejikomboa, wale tuliojipendekeza kuwasaidia kupigania uhuru wameshapata uhuru wao, hawatujali wala kututhamini na huku sisi tunaendeleza wimbo wa enzi hizo.

Vilevile naona wimbo huu haumjengei mtanzania mapenzi na nchi yake, haumfanyi mtu kuwa proud na nchi yake. Hakuna kitu chochote kinachozungumzia uzuri wa nchi yetu wala uzuri wa watanzania au ushujaa wa watanzania….hakuna.
.
naomba tuendeleze mapungufu ya wimbo huu
.
.
Napendekeza wimbo wa ‘Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote….’ ukifanyiwa marekebisho kidogo ungefaa zaidi


Kaka haya ndiyo mambo yamo kwenye sera zetu, vuta subira....
 
hata huo unaotaka wa tanzania tanzania unamapungufu yake mfano "Nilalapo nakuota wewe" unaiota kwa lipi?
 
I always like this song, makes me to love my motherland,

sing with me;

Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote

wimbo wa taifa hauoni ndani hapa!!

muanzisha thread, ukiweka kongamano la watanzania watunge wimbo wa taifa leo hii, bado utakuwa na mapungufu tu,somethings just happens and live!

Ubeti wa pili

Tanzania, Tanzania
ninapo kwenda safaraini.
Kutazama Maajabu, biashara nayo Makazi.
Sitaweza Kusahau Mimi, nambo mema ya kwetu kabisa,
Tanzania, Tanzania
nakupenda kwa moyo wote

Kwa wale wanaopenda ngeri pia unapanda tu as:-

Tanzania Tanzania
I love you with all my heart
My country Tanzania
Your name is very sweet
When I sleep I dream of you
When I wake I am at peace
Tanzania Tanzania
I love you with all my heart

Nafikiri wimbo huu Umetulia hata fisadi akiuimba unamsuta vibaya sana ndani ya roho yake - ana Feel Guilty, wa wakristo ni kama ile sala ya toba.
 
hata huo unaotaka wa tanzania tanzania unamapungufu yake mfano "Nilalapo nakuota wewe" unaiota kwa lipi?

hakuna mapungufu, umesema tanzania unaipenda sana, sasa ukilala unategemea utaona nini? si ni upendo wa tanzania nchi yako ama?

hapo wimbo huu upo sawa tu mkuu.
 
I always like this song, makes me to love my motherland,

sing with me;

Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote

wimbo wa taifa hauoni ndani hapa!!

muanzisha thread, ukiweka kongamano la watanzania watunge wimbo wa taifa leo hii, bado utakuwa na mapungufu tu,somethings just happens and live!

mie nimeimba pamoja na wewe
 
Ubeti wa pili

Tanzania, Tanzania
ninapo kwenda safaraini.
Kutazama Maajabu, biashara nayo Makazi.
Sitaweza Kusahau Mimi, nambo mema ya kwetu kabisa,
Tanzania, Tanzania
nakupenda kwa moyo wote

Kwa wale wanaopenda ngeri pia unapanda tu as:-

Tanzania Tanzania
I love you with all my heart
My country Tanzania
Your name is very sweet
When I sleep I dream of you
When I wake I am at peace
Tanzania Tanzania
I love you with all my heart

Nafikiri wimbo huu Umetulia hata fisadi akiuimba unamsuta vibaya sana ndani ya roho yake - ana Feel Guilty, wa wakristo ni kama ile sala ya toba.

hawa mafisadi mala ya mwisho kuuimba nadhani ilikuwa skuli ya msingi ..
baada ya kujitambua na kukumbwa na tamaa ya mali za nji hii hawawezi kufungua mdomo na kuimba wimbo huu
 
Nimekua nikitafakari Wimbo wetu wa taifa nikabaini kua una mapungufu kadhaa ambayo aidha yangetakiwa yarekebishwe au kutafuta wimbo mbadala.


Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Pili naona kwamba wimbo wetu haumjali mtanzania na wala haumpi kipaumbele hata kidogo, Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba mambo baraka kwa mtanzania zimetajwa katika beti la pili, badala ya kuwa Beti la kwanza. Hii ni aibu na laana kwa watanzania. Tunajilaani wenyewe kwa kuwajali wageni kuliko sisi watanzania. Bahati mbaya hali hii imekua kama self fulfilling prophecy, ndio maana wageni wanatetemekewa na wenyeji wanaonekana mafala ndani ya nchi yao.

Huu wimbo umepitwa na wakati, Unazungumzia kudumisha uhuru wakati hakuna nchi inyotawaliwa sasa hivi. Ilikua sawa wakati wa kupigania uhuru na kipindi cha ujamaa kuwa na wimbo kama huu lakini sasa mambo yamebadilika, nchi zote zimejikomboa, wale tuliojipendekeza kuwasaidia kupigania uhuru wameshapata uhuru wao, hawatujali wala kututhamini na huku sisi tunaendeleza wimbo wa enzi hizo.

Vilevile naona wimbo huu haumjengei mtanzania mapenzi na nchi yake, haumfanyi mtu kuwa proud na nchi yake. Hakuna kitu chochote kinachozungumzia uzuri wa nchi yetu wala uzuri wa watanzania au ushujaa wa watanzania….hakuna.
.
naomba tuendeleze mapungufu ya wimbo huu
.
.
Napendekeza wimbo wa ‘Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote….’ ukifanyiwa marekebisho kidogo ungefaa zaidi
ni kweli hata mimi nakuunga miguu na mikono Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote; ungefaa na ni mzuri tena sana na hata baadhi ya maneno ya Mungu ibariki Tanzania yangeongezwa kwenye wimbo huu wa Tanzania,Tanzania nakupenda kwa moyo wote na kufanyiwa nakshi ungekuwa bora sana.

Naona nchi nyingi nyimbo zao za Taifa zinajivunia nchi zao na mambo mengi mazuri yaliyomo kwenye nchi zao. kwa mantiki hiyo wageni wanakuwa wanavutika kuzitembelea nchi zao kuona kile kinachoimbwa kuwa je ni kweli ndivyo kilivyo.
 
Mungu ibariki Afrika- kwa nn ubeti wa kwanza uanze na africa. No priority
Wabariki Viongozi wake
Hekima Umoja na Amani I think neno uzalendo nila muhimu
Hizi ni ngao zetu
Afrika na watu wake.

CHORUS:
Ibariki Afrika(x2)
Tubariki watoto wa Afrika.

Mungu ibariki Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja- are these two the only or most important
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.

CHORUS:
Ibariki Tanzania(x2)
Tubariki watoto wa Tanzania.


Nyongeza
Huu wimbo umekaa kama tunamlilia lia mungu. why kwann tusitunge wimbo wa kuonyehs wajibu wetu sababu huyo mungu katupa akili.

Serikali yetu haina dini kwa nn mungu atajwe kwenye beti zote. Zitunge betiza kuhamashiha watu wafanye kazi, watoe haki na kuwa huru. Though I belivein God kwa serikali it too much

Nawasilisha kwa mjadala
 
Wimbo wa Kenya umekaa sawa!


Ee Mungu nguvu yetu
Ilete baraka kwetu
Haki iwe ngao na mlinzi
Natukae na undugu
Amani na uhuru
Raha tupate na ustawi.

Amkeni ndugu zetu
Tufanye sote bidii
Nasi tujitoe kwa nguvu
Nchi yetu ya Kenya
Tunayoipenda
Tuwe tayari kuilinda

Natujenge taifa letu
Ee, ndio wajibu wetu
Kenya istahili heshima
Tuungane mikono
Pamoja kazini
Kila siku tuwe na shukrani
 
Wimbo wa Kenya umekaa sawa!


Ee Mungu nguvu yetu
Ilete baraka kwetu
Haki iwe ngao na mlinzi
Natukae na undugu
Amani na uhuru
Raha tupate na ustawi.

Amkeni ndugu zetu
Tufanye sote bidii
Nasi tujitoe kwa nguvu
Nchi yetu ya Kenya
Tunayoipenda
Tuwe tayari kuilinda

Natujenge taifa letu
Ee, ndio wajibu wetu
Kenya istahili heshima
Tuungane mikono
Pamoja kazini
Kila siku tuwe na shukrani

Kwa kuangaliawimbo wa aifa unaweza kuona ifa lenye vision.
Wimbo wetu umejaaaaa mungu mungu, Hekima, Umoja na Amanai

huu wa kenya wamejitahidi kuna Kujenga taifa. Kazi na Haki......
 
Naona tuombe kwanza Mungu atupe viongozi wazuri wenye kuchapa kazi vizuri wasiopenda zuluma, Ufisadi, bali wenye nia ya Maendeleo ya nChi, wenyeUpendo wa kweli na Uzalendo wa Tanzania ,wenye moyo safi wenye upendo na watu wake, na ndipo sa mabadiliko kama wa Wimbo wa Taifa utafanyila kama kuna Ulazima maana kwa tafsiri yangu Unamtanguliza Mungu kwenye mambo yote, akupe Amani , ya kufanya Kazi yako , Utulivu, Hekima, na Umoja ndio ujumbe hivyo vitu vitatu , vinaleta , Ufanisi wa Kazi, maarifa mapya, Uzalendo wa nchi, na Maendeleo. sioni haja ya kubadilisha wanaokwamisha maendeleo ya Tanzania ni Viongozi wetu wanaopenda Zuluma, wauwaji, na wasiojali maisha ya watanzania.
 
Hili nalo lazima tuliweke kwenye katiba, yaani katiba mpyaaa itakuwa bomba saana
 
wATANZANIANIA NI WAVIVU WA KUFIKIRIA.
HUU WIMBO TULIUKOPI KUTOKA AFRIKA YA KUSINI NA TUKAUTAFSIRI.
HUWA NACHEKA SANA ETI KUNA LIJAMAA LINASEMA ETI LENYEWE NDIO LILIUTUNGA HUO WIMBO WAKATI UNAJULIKANA KABISA ASILI YAKE
Mungu ibariki Afrika- kwa nn ubeti wa kwanza uanze na africa. No priority
Wabariki Viongozi wake
Hekima Umoja na Amani I think neno uzalendo nila muhimu
Hizi ni ngao zetu
Afrika na watu wake.

CHORUS:
Ibariki Afrika(x2)
Tubariki watoto wa Afrika.

Mungu ibariki Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja- are these two the only or most important
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.

CHORUS:
Ibariki Tanzania(x2)
Tubariki watoto wa Tanzania.


Nyongeza
Huu wimbo umekaa kama tunamlilia lia mungu. why kwann tusitunge wimbo wa kuonyehs wajibu wetu sababu huyo mungu katupa akili.

Serikali yetu haina dini kwa nn mungu atajwe kwenye beti zote. Zitunge betiza kuhamashiha watu wafanye kazi, watoe haki na kuwa huru. Though I belivein God kwa serikali it too much

Nawasilisha kwa mjadala
 
ushauri wako ni mzuri, ila kuna siku nilisika kuwa huu wimbo umenyambulishwa kutoka nyimbo za kanisa so kama ni kweli basi mungu lazima atajwe kila mahali kutaka msaada. Huo wimbo ulivyo hauna tofauti na wale ndugu zetu waliohamia pale uwanja wa ndege Dar wakitarajia kupitia jina la bwana wangeenda ulaya kwenda kuhubiri neno lake na matokeo yake wakaishia kuugulia njaa na kuomba msaada. sisi bila kujishughulisha hakutatengeneza differences, napendekeza hata mimi kuwa tuache tu kumtegemea mungu bila ya sisi kujishughulisha. wewe mvua inanyesha halafu umelala huku ukiomba mungu uvune mahindi, hivi huu siutakuwa uchizi? tunaambiwa kuwa mungu habadilishi yaliyo kwa binadamu mpaka yeye (binadamu) abadilishe yaliyo kwenye moyo (matendo) wake. naunga mkono huu wimbo ubadilishwe
Nawasilisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom