Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,425
Taarifa ikufikie kwamba Maandalizi ya Mapokezi kabambe ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu yamekamilika, ambako wanachama wa CHADEMA na wapiga kura wake waliomchagua kwa kishindo 2020 kabla ya Sarakasi za Dr. Mahera, wametakiwa kujipanga kuanzia uwanja wa ndege hadi Temeke.
Habari zaidi kutoka kwenye Kamati ya Mapokezi zinasema kwamba, baada ya kuwasili, Tundu Lissu ataenda moja kwa moja kwenye Mkutano wa Hadhara ulioandaliwa na chama chake Viwanja vya Bulyaga -Temeke, mkoani DSM, ambako anatarajiwa kuhutubia taifa.
Binafsi nimesikia gari la matangazo likipita mitaani kwetu huku Tandika Mwembeyanga likihamasisha Wananchi kumpokea Shujaa wao.
Usiondoke JF kwa taarifa zaidi.
Habari zaidi kutoka kwenye Kamati ya Mapokezi zinasema kwamba, baada ya kuwasili, Tundu Lissu ataenda moja kwa moja kwenye Mkutano wa Hadhara ulioandaliwa na chama chake Viwanja vya Bulyaga -Temeke, mkoani DSM, ambako anatarajiwa kuhutubia taifa.
Binafsi nimesikia gari la matangazo likipita mitaani kwetu huku Tandika Mwembeyanga likihamasisha Wananchi kumpokea Shujaa wao.
Usiondoke JF kwa taarifa zaidi.