Mapokezi Global Publishers imenisikitisha

Mapokezi Global Publishers imenisikitisha

mamitod

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
914
Reaction score
385
Niende moja kwa moja kwenye mada. Nilifika mapokezi nikaomba kuonana na mkurugenzi. Huyu binti mnatooo sijui ndio mmiliki halali au vipi maana duuu anaongea km anapumua almasi kumbe hewa ya kawaida tu.

Akaniuliza una appointment? nikajibu la! Akasema nipe namba yako nitamfikishia ujumbe kisha nitakupigia siku utayopewa appointmet. Nikashukuru nikaondoka nikiwa na matumaini ya kupata fursa hiyo. Wiki ikapita hakuna simu wala nn. Nikarudi nikamuuliza vipi?

Nikamkumbusha nilipofika pale mara ya kwanza. Akasema bado lkn namba yako bado nimehifadhi. Nikarudi wa baridi na hivi sasa ni miezi imepita.

Najiuliza huyu sekretari alitimiza wajibu wake au aliniminyia makusudi? Yeye ndio huamua watu wa kumuona huyo Shig? Alijua kilichonipeleka pale? Shig alijua kuna mtu alikuwa anataka kumuona? Nina maswali mengi ila naona tu nisiyaweke yote hapa.

Sijui wenzangu mmewahi kukutana na adha km hizi?
 
Kumbe wanayo ofisi !!!
Uliacha namba ya simu bila hela ya vitumbua.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Kumbe wanayo ofisi !!!
Uliacha namba ya simu bila hela ya vitumbua.

:smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big::smile-big:.

Kama Sepetunga ana ofisi, Global Publisher watakosaje?!
 
ninavyojua mimi global huwezi kufika mapokezi kabla ya kukutana na mlinzi ambaye anaweza kukuruhusu baada ya mahojiano. mlangoni kuna tangazo la jitambulishe (kwa mlinzi) na kama ulifika mapokezi na hukuwa na mawasiliano na shigongo ya simu, basi hukuacha namba za simu, uliacha ujumbe tu wa kutaka kuonana na shigongo. mbona mimi nilishabahatika kufika na kuacha namba na nikapigiwa simu mara moja! kuwa mkweli ndugu.
 
ninavyojua mimi global huwezi kufika mapokezi kabla ya kukutana na mlinzi ambaye anaweza kukuruhusu baada ya mahojiano. mlangoni kuna tangazo la jitambulishe (kwa mlinzi) na kama ulifika mapokezi na hukuwa na mawasiliano na shigongo ya simu, basi hukuacha namba za simu, uliacha ujumbe tu wa kutaka kuonana na shigongo. mbona mimi nilishabahatika kufika na kuacha namba na nikapigiwa simu mara moja! kuwa mkweli ndugu.

Habari ya Bamaga mkuu!vipi OFM inaanzia wapi kipindi cha sikukuu
 
ninavyojua mimi global huwezi kufika mapokezi kabla ya kukutana na mlinzi ambaye anaweza kukuruhusu baada ya mahojiano. mlangoni kuna tangazo la jitambulishe (kwa mlinzi) na kama ulifika mapokezi na hukuwa na mawasiliano na shigongo ya simu, basi hukuacha namba za simu, uliacha ujumbe tu wa kutaka kuonana na shigongo. mbona mimi nilishabahatika kufika na kuacha namba na nikapigiwa simu mara moja! kuwa mkweli ndugu.
Yuk nilikuwa sifahamu kuwa kuna watu wana"bahatika" kuonana na his excellency Shi-rungu!
 
Bongo bhana tabu kweli kweli, eti kukuona Shigongo amrkuwa doctor ama? Hata hao mawaziri Ukienda ofisini mwao unawaona Bila urasimu huu
 
Bongo bhana tabu kweli kweli, eti kukuona Shigongo amrkuwa doctor ama? Hata hao mawaziri Ukienda ofisini mwao unawaona Bila urasimu huu, sasa mtu yupo ofisini eti huwezi kumuona hadi appointment, what a fucccvcck
 
ninavyojua mimi global huwezi kufika mapokezi kabla ya kukutana na mlinzi ambaye anaweza kukuruhusu baada ya mahojiano. mlangoni kuna tangazo la jitambulishe (kwa mlinzi) na kama ulifika mapokezi na hukuwa na mawasiliano na shigongo ya simu, basi hukuacha namba za simu, uliacha ujumbe tu wa kutaka kuonana na shigongo. mbona mimi nilishabahatika kufika na kuacha namba na nikapigiwa simu mara moja! kuwa mkweli ndugu.
Kwa nn nidanganye? Kwa faida gani? Nisene uongo kukufurahisha wewe? Km wewe ulipigiwa mimi sikupigiwa nielewe hivyo
 
Bongo bhana tabu kweli kweli, eti kukuona Shigongo amrkuwa doctor ama? Hata hao mawaziri Ukienda ofisini mwao unawaona Bila urasimu huu, sasa mtu yupo ofisini eti huwezi kumuona hadi appointment, what a fucccvcck

Ndipo niliposhindwa kbs kuelewa kwa nn iwe hivyo? Watz tuna urasimu wa ajabu sana
 
ninavyojua mimi global huwezi kufika mapokezi kabla ya kukutana na mlinzi ambaye anaweza kukuruhusu baada ya mahojiano. mlangoni kuna tangazo la jitambulishe (kwa mlinzi) na kama ulifika mapokezi na hukuwa na mawasiliano na shigongo ya simu, basi hukuacha namba za simu, uliacha ujumbe tu wa kutaka kuonana na shigongo. mbona mimi nilishabahatika kufika na kuacha namba na nikapigiwa simu mara moja! kuwa mkweli ndugu.

Umebahatika???? Yani kuonana na hao wahuni ni bahati??!
 
Sisi wabongo tukikamata hela ya kubadilisha mboga tunakuwa na mikwara hadi apointmenti duh!

Ndio maana IQ zetu ndogo eti ukifululiza kula nyama kila siku wewe ni Freemason.
 
Anaogopa anafikili labda wewe ni kachelo,kwani hujui kuwa hiyo kampuni ni ya kitapeli?
 
Ni jambo la kushangaza kweli, unaendaje kwa mtu na shida zako halafu unataka kuonana naye kadiri unavyotaka wewe? Ninavyojua, siyo tu ofisi, lakini kila mtu ana utaratibu wake wa maisha. Sioni ajabu Shigongo kuweka utaratibu wa kukutana na wanaomhitaji, ndiyo maana wanaoona ajabu kwa yeye kuweka utaratibu, ni wale wasio na shida naye. Niwaulize waungwana, hivi mtu anaweza kuja kwako akakukuta kwa mfano unaongea na baba yako akataka umuache umsikilize?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom