Mapito ya career woman

Status
Not open for further replies.
Upo sahihi kbsa mkuu,jamaa ameongelea wanawake wanaotoka kwenye familia zenye uchumi mdogo
 
Wanatumika sana aise, unakuta vibinti vinalika kwa chips na ukiwa na ist ndio basi Tena kazi kwako
 
Upo sahihi kbsa mkuu,jamaa ameongelea wanawake wanaotoka kwenye familia zenye uchumi mdogo
Uchumi mdogo ndo upi mzee mwenzangu? Hivi vyuo vyetu vya kawaida kukuta mtoto wa tajiri anasoma ni ngumu sana, wengi wanatokea kwenye famiia za kawaida

halafu ukichunguza vizuri hao wanaotokea kwenye familia za hali duni huwa wanasingiziwa tu, hao wakifika chuo huwa wanapiga msuli kwa usongo sana na wanakua makini kwa sababu wanajua familia inawaangalia.

Malaya mashuhuri huko vyuoni ni mademu ambao wanatokea kwenye familia zenye uwezo wa kawaida, sio familia za hali chini kama wengi mnavyofikiria, na motive yao ya kufanya kikahaba ni kuweza kuishi ile extravaganza lifestyle wanayoona wanaishi watu maarufu uko mitandaoni, wala sio umasikini kama mnavyofikiria
 
Ndio maana siku hizi watu wanatia kwanza mimba then maswala ya ndoa baadae..
 
Kwanza kabisa maandiko yanasema toa kwanza boriti lililoko jichoni mwako kabla hujatoa kibanzi kilichopo kwenye jicho la mwenzako vinginevyo maandiko yanamuita mtu wa hivi mnafiki, wanaume kinachofanya wanawake wasiwasikilize ni kitendo cha kukemea mabaya yao tu na kuyaacha ya kwenu, kana kwamba ninyi ni watakatifu au ninyi ndio mna haki ya kutenda mabaya

Siku zote ukitaka watu wakusikilize kuwa fair kwenye kukemea mabaya na kusifia mazuri usiwe na any kind of biasness vinginevyo utaonekana mnafiki kama wanafiki wengine tu, na kingine nilishakuambia kwenye suala la ngono na mahusiano hakuna namna unaweza ukaihukumu jinsia moja ukaiacha nyingine, kwa sababu hilo ni tendo ambalo ili lifanyike linahitaji uwepo wa jinsia zote mbili huwezi kusema eti jinsia moja ikilifanya ni sahihi ila jinsia nyingine ikilifanya ni kosa

Yani logically ni either hilo tendo liwe sahihi kwa wote au liwe kosa kwa wote kulingana na mazingira na siyo mnasingizia eti ni nature ilihali ni social constructs tu, jamii nyingi hasa za kiafrika zimekuwa na mitazamo fulani ambayo haitumii logic bali lengo lake ni ili mradi kuwakandamiza tu wanawake na kuwanufaisha wanaume, maana ukitumia common sense tu ukaangalia hiyo mitazamo unaona mingi haina uhalisia bali ni hisia na mihemko tu kitu ambacho ni far from nature
 
MImi sio muumini wa hayo maandiko uliyoyafanyia rejea. Mshua alinikuza katika misinhi ya kitamaduni zaidi
Kwenye suala la sex tayari nilishakuambia mara nyingi sana, hauwezi kuwaweka kwenye mzani mmoja mwanaume na mwanamke. Mwanaume hata akiwa na mileage kubwa ya body count likija suala la kuoa ilo suala halizingatiwi cha muhimu tu awe amejipanga kutunza familia. Hii ni tofauti na mwanamke akiwa na body count ikawa inasoma namba kubwa inamchafulia profile. Kwaiyo mwanamke kama gatekeeper ya sex na fertility na victim wa consequencies za high body count na unplanned pregnancy anawajibika zaidi kujichunga

Hapo haimaanishi ya kwamba mwanaume anapendelewa kwa sababu hata yeye kuna vigezo ambavyo vinambana kutokana na jinsia yake, mfano suala la uchumi linapokuja suala la kuoa. Kila jinsia ina matamanio ya kiwa na mwenza wa jinsia nqingine lakininkwa mwanaume kufanikisha ilo ni lazima awe na stable income, hii ni tofauti na mwanamke ambae anaweza kuingia kwenye mahusiano/ndoa hata akiwa masikini ambae hana chochote.
 
Hivi si ni juzi tu hapa nimetoka kukuambia kwamba mwanaume kuwa judged kulingana na uchumi wake ni kwa sababu ya mgawanyo wa majukumu na si vinginevyo, ni kama ambavyo wanawake wanakuwa judged kwa uwezo wao wa kufanya kazi za nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto na kutunza mume nk, mbona wanaume wanapotaka kuoa hawaulizwi kama wanajua kufanya hizo kazi ilihali wanaweza kuzifanya, hiyo ni kwa sababu hayo yanaonekana ni majukumu ya wanawake kama ambavyo kutafuta pesa na kuhudumia familia yanaonekana ni majukumu ya wanaume, ndio maana wanakuwa judged kulingana na uchumi wao sababu mwanaume ndio sole provider wa familia ingawa wapo wanaume masikini wanaopata wanawake wa kuoa

Okay kwahiyo kumbe wanaume mnapowachezea wanawake mnafanya makusudi sababu mnajua jamii haiwahukumu ninyi katika suala la ngono na mahusiano basi hapo ndipo shida ilipo, maana hapa tatizo siyo jamii inamhukumu nani tatizo ni uhalisia uliopo kwamba the more wanaume wanavyozidi kuwachezea mabinti kuanzia wakiwa na umri mdogo ndio the more wanavyozidi kupunguza idadi ya bikira ambazo wanaume watakuja kuzihitaji wanapotaka kuoa maana kiuhalisia bikira hazina faida kwa wanawake wenyewe bali kwa wanaume, kwa mfano sasa hivi tunaona vilio vingi kwenye mahusiano vinatoka kwa wanaume kwa sababu ya kulilia bikira za wanawake ilihali wao ndio waliohusika kuzitoa halafu mwisho wa siku tunaona wanaoa hao hao wanawake waliotumika sababu bikira ni chache na haziko tayari kuolewa mapema

By the way nilirejea hayo maandiko nikidhani wewe ni muumini wa dini ya kikristo, lakini kama ni muumini wa misingi ya kitamaduni basi pia kaa ukijua si kila mtu nchi hii anaamini katika hizo tamaduni bila kujali alizaliwa katika jamii hizo au la, kuna watu hizo tamaduni wanaziona kama takataka tu sababu hazina maslahi yoyote kwao ilihali ninyi ambao mnaona zina maslahi kwenu ndio mnazikubali na kuzipigoa sana chapuo
 
Chuo unamalizaje na Bikra aisee labda Veta
Sasa unabisha nini mbona tuko Wengi tuliomaliza vyuo tena vikuu tukiwa na bikira, infact hadi leo wengine katika umri huu wa late 20s bado tuko na bikira na hazina dalili za kutolewa, yote yanawezekana ikiwa mwanamke utawadharau wanaume na ukiwa huna tamaa za kipumbavu kabisa
 
Wewe utakuwa Umepita Vyuo vya ufundi ambavyo ushawishi uko chini, Sisi wazee wa Political Science, Sijui Human resources na Business Admistration hakuna Mtu Kuchomoka na Bikra tena uwe dar hapa chances ni ndogo sana
 
Wewe utakuwa Umepita Vyuo vya ufundi ambavyo ushawishi uko chini, Sisi wazee wa Political Science, Sijui Human resources na Business Admistration hakuna Mtu Kuchomoka na Bikra tena uwe dar hapa chances ni ndogo sana
Acha ubishi na kujifanya unanijua sana mimi nimesoma Mzumbe nina Degree ya HR nina miaka 27 na bado bikira, chuo nilichosoma hakiko Dar lakini nimezaliwa Dar nimekulia Dar wazazi na ndugu wengi wako Dar na kwa sasa Nafanya kazi na biashara hapa hapa Dar, sema kingine maana hamchelewi kusema "oo wewe utakuwa huna tako na una sura ya baba" ilimradi tu mpate sababu
 
Career Focused Women ni hatari sana kuna Demu unakuta mnaishi Chuo for 4 yrs kula na Kupakua plus abortion kibao along the way yani Umevuruga haswa leo unasikia Kuna Mjuba anasweka Ndani iyo kazi ni balaa sana yani trip zake za kikazi akijua tu upo sehemu fulani brake ya kwanza Nikulete Bumbu utindue
 
Wewe utakuwa Umepita Vyuo vya ufundi ambavyo ushawishi uko chini, Sisi wazee wa Political Science, Sijui Human resources na Business Admistration hakuna Mtu Kuchomoka na Bikra tena uwe dar hapa chances ni ndogo sana
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ wazee wa political science
 
Wewe ni muongo
 
"Anapoteza Bikra zote Mbili".... Dah hii kitu ndio sitakagi ata kusikia wazee
 
Kuna demu nimemaliza nae chuo siku moja nikaona kapost picha zake za harusi mtandaoni nikamzoom bwana harusi nikabaki namsikitikia tu
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…