Mamndenyi
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 40,565
- 52,202
Nawaachia mapishi haya (nimedesea mahali) kwa weekend hii, hasa wale mabinti zangu, then feed me back.
NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI
MAHITAJI
1. Chukua Amira ya chenga gram 11,
2. Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai,
3. Sukari gram 250,
4. Unga wa ngano kilo moja,
5. Maji ya uvuguvugu nusu lita,
6. Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu.
NAMNA YA KUANDAA
1. Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yote kwenye unga wako wa kilo moja.
2. Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndani ya andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji.
3. Weka sukari gram 250 katika unga wako.
4. Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250 changanya vizuri mafuta bado yakiwa ya moto.
5. Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano na kufanya amira kuweza kuumuka haraka. Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini.
6. Mchanganyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpaka uwe mkavu na laini.
7. Hapa safi sasa. Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata Sukuma unga wako mpaka saizi ya unene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe.
8. Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda. Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma.
9. Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi.
10. Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza.
Hili ni andazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa.
NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI
MAHITAJI
1. Chukua Amira ya chenga gram 11,
2. Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai,
3. Sukari gram 250,
4. Unga wa ngano kilo moja,
5. Maji ya uvuguvugu nusu lita,
6. Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu.
NAMNA YA KUANDAA
1. Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yote kwenye unga wako wa kilo moja.
2. Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndani ya andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji.
3. Weka sukari gram 250 katika unga wako.
4. Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250 changanya vizuri mafuta bado yakiwa ya moto.
5. Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano na kufanya amira kuweza kuumuka haraka. Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini.
6. Mchanganyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpaka uwe mkavu na laini.
7. Hapa safi sasa. Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata Sukuma unga wako mpaka saizi ya unene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe.
8. Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda. Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma.
9. Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi.
10. Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza.
Hili ni andazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa.