MAPIGO: Mbeya City yaagiza ‘ndege ya chini’

MAPIGO: Mbeya City yaagiza ‘ndege ya chini’

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,267
mbeya.jpg
Suala la usafiri ambalo linatarajia kukamilika muda si mrefu kutoka sasa, klabu hiyo inatarajia kununua basi jipya la kisasa lenye huduma zote ndani. Basi hilo litakuwa ama Yutong au Higer.
 
MBEYA City imemaliza Ligi Kuu Bara kwa kushika nafasi ya tatu na sasa imeanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msimu ujao kwa maana na usajili pamoja na kutengeneza miundombinu yake, likiwamo suala la usafiri kwa kununu basi la kisasa litakalokuwa ‘ndege ya chini'.

Mikakati mingine ya miundombinu hiyo ni kujenga uwanja wao. Kwa suala la uwanja, inatarajia kuanzisha kazi ya kuujenga katika eneo la Iwambi mjini Mbeya. Eneo lao limeelezewa kuwa na ukubwa ekari 15.

Ukija kwenye suala la usafiri ambalo linatarajia kukamilika muda si mrefu kutoka sasa, klabu hiyo inatarajia kununua basi jipya la kisasa lenye huduma zote ndani. Basi hilo litakuwa ama Yutong au Higer.

Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe, ameliambia Mwanaspoti kuwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya ambayo ndiyo mmiliki wa timu hiyo, imeshatangaza tenda kwa kampuni mbalimbali zinazouza magari baada ya kuweka wazi sifa za basi wanalolihitaji.

"Tulitangaza mara ya kwanza, hakukuwa na kampuni iliyojitokeza, tukarudia ndipo kampuni tatu zimejitokeza na hivyo itapendekezwa kampuni moja kulingana na makubaliano yatakayofanyika," alisema Kimbe.

"Tupo katika hatua za mwisho za ununuzi wa basi la timu, tutahitaji moja lenye hadhi tunayoitaka, fedha zipo."

MAPIGO: Mbeya City yaagiza ‘ndege ya chini’ - Soka - mwanaspoti.co.tz

 
Nayaona Mapinduzi ya soka Tanzania kwa mbaaaaaaali yanakuja kama ti yale ya 2015
 
nasisimkwa sana kwa hili

naona wanataka kutujibu AZAM FOOTBALL CLUB mabingwa wa tanzania....!?
sio mbaya huo ndio wivu wa kimichezo sio kama wakongwe SIMBA na YANGA baraka ya majungu tu.
ila mwakani tutanunua ndege kama TP MAZEMBE..
 
Katika michezo haya ndio maendeleo tunayoyataka sio timu kongwe hadi zihongwe na kili time,viongozi wananeemesha matumbo ya familia zao tu.
Hongera mcc kwa mipango hiyo.baada ya hapo mje na uwanja sasa
 
Nini maana ya ndege ya chini?
Ni huduma safi au spidi kali?
 
Safi mbeya city!

Lengo letu ni kuondoa hizo timu mbili za kariakoo ambazo zipo toka nchi yetu inaitwa tanganyika hadi leo hata uwanja hazina.

Simba tumeishaweka nafasi ya 4 na mwakani inashuka daraja kabisa.

Mwakani yanga watashika nafasi ya 3.
 
natamani kila mkoa uwe na timu kama hii
 
Ndanda fc nayo inakuja sasa hawako mbali wanajipanga kila mkoa wakiwa na timu kama mcc mbona mpira wa tanzania utakuwa juu sana hongereni mcc
 
Mkuu wahinga wamenina kipya hakinyime au ivumayo haidumu hilo basi kweli letabeba wachezaji kwa muda baadaye litakuwa lenasanya kama dala dala na hayo tushayaona na hiyo ni sawa sawa na shati jipya
 
mwanza ndi hakuna kitu siasa ndio zimetawala jiji halina timu hata 1,ona tanga ona mbeya
amkenu wana mwanza
 
Safi mbeya city!

Lengo letu ni kuondoa hizo timu mbili za kariakoo ambazo zipo toka nchi yetu inaitwa tanganyika hadi leo hata uwanja hazina.

Simba tumeishaweka nafasi ya 4 na mwakani inashuka daraja kabisa.

Mwakani yanga watashika nafasi ya 3.

Haya ni mapinduzi safi kuliko kufurahia basi!!!!
 
Katika michezo haya ndio maendeleo tunayoyataka sio timu kongwe hadi zihongwe na kili time,viongozi wananeemesha matumbo ya familia zao tu.
Hongera mcc kwa mipango hiyo.baada ya hapo mje na uwanja sasa

kwa kweli kwa uwanja neno hilo
 
hizi za kariakoo zimekuwa pango na kichaka cha mafisadi wa kisiasa, hadi kichefuccjefu yaani
Safi mbeya city!

Lengo letu ni kuondoa hizo timu mbili za kariakoo ambazo zipo toka nchi yetu inaitwa tanganyika hadi leo hata uwanja hazina.

Simba tumeishaweka nafasi ya 4 na mwakani inashuka daraja kabisa.

Mwakani yanga watashika nafasi ya 3.
 
Mkuu wahinga wamenina kipya hakinyime au ivumayo haidumu hilo basi kweli letabeba wachezaji kwa muda baadaye litakuwa lenasanya kama dala dala na hayo tushayaona na hiyo ni sawa sawa na shati jipya

hakuna taabu, hata Castaal hawajafikia hapo
 
Back
Top Bottom