Mapigano dhidi yako mwenyewe πŸ’ͺ

Wanaopigana vita dhidi yao wao wenyewe ni watu wasiojitambua na ni watu wasiojua wanataka nini kwenye maisha yao,

Ni watu wanaoendeshwa zaidi kwa hisia kuliko akili,

Sijawahi kupigana vita dhidi yangu na wala haitatokea,kila ninachokifanya ni maamuzi yangu mimi kama mimi,sijawahi kujuta na wala sitakuja kujuta coz kila jambo hua na thamani kwa wakati wake,

Live the life you love,
Love the life you live.
 
Okay πŸ‘
 
Kumbe hujasoma mada uwii
Okay!
Cognitive dissonance ni hali ya msuguano unaotokea kwenye akili yako pale unapokuwa na, (a) Imani mbili zinazopingana, (b)unachoamini hakifanani na tabia yako. Kwa mfano unajua JF inakupotezea muda lakini wewe bado unaendelea kuingia tu JF (inakuuma lakini huachi).

Unaoata stress. Katika kupunguza hizi stress akili inafanya mambo yafuatayo:
1. Unabadi imani juu ya jambo husika, kwa mfano unajisemea, "labda JF hainipotezei muda". Akili inatulia.

2. Kujihalalishia. Unajisemea, "mbona wengine wako tu JF masaa yote, nami naendelea tu kuperuzi". Akili inatulia.

3. Unapunguza uzito wa tatizo. Unajisemea, "hata hivyo sikai sana jukwaani". Akili inatulia.

4. Kuachana mazima na kile unavhoona hakikufai. Hii ni njia ngumu lakini ni muhimu sana. Unaacha kabisa kuingia JF unakwenda kulika mpunga majarubami na unapata manufaa makubwa.

NB: Akili ya binadamu hupendelea zaidi comfort zone ndiyo maana haitaki kuona unabadilika. Jaribio la kutaka kubadika ni tishio kwa akili yako, so yakupasa ujikaze sana.

Msome Leon festinger kwa mengi zaidi.
 
Nakumbuka mwaka 2000 niliitwa na bibi yangu kijijini aliniambia mambo mengi sana ila maneno ninayoyakumbuka hadi leo aliniambia "mjukuu wangu ipo siku moja watu wengi watapoteza mda wao kusoma comment yako"
 
Umemshauri vyema sana Madam, labda niongezee jambo hapa.

Ndugu shilaa hiyo ni vita ambayo watu wengi wanapambana nayo kimya kimya, wengi huwa wanaishia kusema ndiyo ili wasiwaudhi wengine, lakini mwisho wa siku huwa wanaishia kujiudhi wenyewe.

Kumbuka, kusema hapana pale ambapo huna uwezo ni self respect. Ukikubali kila ombi kwa kuogopa watu watakuchukuliaje, utaanza kubeba mizigo ambayo si yako, halafu mwisho wake stress na majuto vinakuwa sehemu ya maisha yako.

Sometimes, the most powerful word is simply No, watu wanaokuheshimu kweli wataelewa mipaka yako na wasiokuelewa, huenda walikuwa wanathamini manufaa wanayoyapata kwako kuliko ustawi wako.

Jifunze kusema, "Ningependa kukusaidia, lakini kwa sasa siwezi." Huu sio ubinafsi, ni wisdom. Ukijifunza hilo utaona amani ya moyo wako inaongezeka kuliko ulivyowahi kufikiria.
 
Mkuu sio kwamba wewe hauna msimamo.

Bali wewe ni mtu muelewa yani unaelewa tatizo la mwingine kama lako na unapenda kusolve problems ambalo sio jambo baya.

Ila kwa bahati mbaya unasolve matatizo yawatu wasio jielewa, ndiyo maana unakuja kuangukia kwenye majuto kwamba why nilisolve tatizo then matokeo yake napata hasi sio chanya.

Point nini mkuu solve your own problems achana na matatizo yao achakuwa muelewa kwenye matatizo yao.
 
1
kwenye mazingira au matukio ya userious mathalani kwenye vikao vya ofisini au sehemu yoyote utakayohitajika utoe mawazo yako huku watu wakiwa attention kukusikiliza wewe.
Mkuu, kitu cha kwanza ni kujikubali mwenyewe

Amini kwamba una uwezo wa kuzungumza na watu na kwamba mawazo yako yana thamani

Acha kujiuliza sana Watanichukuliaje nikiongea

Ukweli ni kwamba hakuna mtu mkamilifu

Kila mtu ana changamoto zake na kila mtu hujifunza kwa kupitia makosa

Wewe kama ni kuongea ongea ukikosea kesho utajifunza kupitia makosa yako ya leo

Anza kuongea taratibu bila kuogopa kuhukumiwa maana challenge utakutanazo na ni kawaida

Wengine watakuelewa, wengine watakosoa, lakini hata maneno mabaya yakitokea yachukulie kama changamoto ya kukufanya uwe bora zaidi

Ujue kabisa hata iweje huwezi kukubalika na wote haiwezekani ukijua hivyo utakua huru kufanya unavyopenda bila kujali matokeo hasi dhidi yako
 
Asante ndege Mdinya πŸ™πŸ™
 
Nakumbuka mwaka 2000 niliitwa na bibi yangu kijijini aliniambia mambo mengi sana ila maneno ninayoyakumbuka hadi leo aliniambia "mjukuu wangu ipo siku moja watu wengi watapoteza mda wao kusoma comment yako"
Sawa mkuu
 
Thank you 😊
 
Kwanza kabisa ishi vile unavyopenda.
Amejuaje kama uko full time kama na yeye hayuko hivo.
Kila mtu afanye anachokipenda.
Watuache.
 
kweli mkuu kwanza nimejihisi mwenye furaha baada ya kupata mawazo yenu hapa nimeajifunza kitu kiufupi mmenifundisha mbinu za kushinda vita vyangu kuliko ningepipana kimoyo moyo
 
Argentina Bingwa

Full time Argentina 2 Spain 1
Yes πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯
Ila hapo kwenye mbili moja ngoja nitunze comment
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...


Cc: Mahondaw
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…