Mapenzi yanaumiza

Mapenzi yanaumiza

Dorcas21

Member
Joined
Dec 7, 2021
Posts
16
Reaction score
65
Kwanini wanaume mnatuumiza wanawake hisia zetu, najuta kupenda. Nilikua na mwanaume nilimpenda haswaa na ndiye mwanaume wangu wa kwanza, nina miaka 30, tatizo la huyu mwanaume ni malaya sanaa, anawanawake wengi, sasa nimeamua kumuacha, japo nikikaa namkumbuka lakini sitaki niendelee kuumia.

Nifanye nini ili nimsahau kabisa?
 
Amekubikiri halafu akasepa. Na huyu huyu kesho na kesho kutwa utamkuta kwa akina Jokajeusi akilalamika kuwa siku hizi hakuna mabikra wa kuoa!

Kuhusu kuumia hakuna njia ya mkato binti yangu. Ni lazima uumie tu. Ila kwa kadri siku zinavyokwenda maumivu yataanza kupungua, kutaanza kupambazuka na hatimaye jua litachomoza tena, moyo wako utapona polepole; na furaha yako itarudi.

Jitahidi kujiweka bize. Kama una marafiki wa kweli kuwa nao karibu. Ndugu pia na hasa mama. Huu ndiyo wakati wa kumuomba akupe stori za usichana wake...pia soma neno la Mungu na kusali sana (kama ni muumini)

Na usiache kulia. Ukijisikia kulia we lia tu. Hiyo ndiyo tiba yenyewe hasa. Utapona na ukija kuangalia experience yako hii ya kwanza na wanaume utakuwa umejifunza mengi....

Na safari ndo imeanza rasmi sasa. Kwa wanaume wa Kibongo sisi, definitely it gonna be a bumpy ride ahead. You better fasten your seat belt. Kila la heri
 
Aiseee pole Sana
Nimetoka kumuacha mwanamke niliempenda kwa moyo wangu wote kisa amemimbishwa na jamaa mwingine nikiwa masomoni.
 
Furaha na amani ya moyo utaipata kupitia wewe mwenyewe Ukitegemea mtu au kitu kikupe furaha utaumia Kila siku Kila kitu hubadilika Kitu pekee kisichobadilika ni mabadiliko yenyewe.
 
Back
Top Bottom