Mapenzi yanapo waunganisha watu wawili na kupelekea mushkeri katika jamii

Kuna siku niliwahi kuona chapisho lililosema."Najiuliza jinsi Dr Nandipha aliweza kupenda, kuishi na kufanya mapenzi na muuaji bila kuogopa, kwa mara ya kwanza nitakubaliana na watu wasemapo ogopa wanawake"Baada ya kuona chapisho hilo nikajiuliza huyu Dr Nandipha ni nani?

Nikagundua ni mwanamke aliyezaliwa Eastern Cape katika kijiji cha Bizana South Africa, kisha akaja kukulia huko Port Edward kwazulu-natal.Dr Nandipha ni mrembo anayevutia kumtazama Na zaidi ni mwanamke aliyejiweza kipesa, anamiliki nyumba nzuri, magari ya kifahari pamoja na
clinical yake inayoitwa Optimum Medical Aesthetics Solutions.

Hapa nikajiuliza tena why alishi na kufanya mapenzi na mwanaume Mwizi, Tapeli, muuaji na mbakaji.Na hapo ndipo kiu yangu ya kutaka kufahamu nisiyoyafahamu iliongezeka.Kwanza kabisa niliona chapisho lingine!!.
kwenye mtandao likisema.."Polisi wa Tanzania wamethibitisha kumkamata Thabo Bester na Nandipha Magudumana na mtu mwingine aliyefahamika kwa jina la Zakaria Alberto"Taarifa zilisema watu hao wameshikiliwa na jeshi la polisi la Tanzania na mawasiliano baina ya nchi 2

Tanzania na South Africa yanafanyika ili watu hao warudishwe South Africa.Bado udadisi wangu wa mambo ulitaka kudadisi juu ya watu hao wawili walifikaje Tanzania na why wote waitwe wauaji.?
Niligundua watu hawa ni wapenzi, ila nikaja kushangazwa.

nilipofahamu mwanaume ambaye ni Thabo Bester alikuwa gerezani kwa takribani miaka 10 Na hata Penzi Lao, lilianza rasmi wakati mwanaume huyo yuko gerezani.Hili likanifikirisha zaidi, jinsi gani na kwanamna gani mwanamke alivutiwa na mwanaume mfungwa.

Na hapo ndipo nilipopata
Kufahamu mwanaume ambaye ni Thabo Bester alikuwa gerezani kwa takribani miaka 10Na hata Penzi Lao, lilianza rasmi wakati mwanaume huyo yuko gerezani.Hili likanifikirisha zaidi, jinsi gani na kwa namna gani mwanamke alivutiwa na mwanaume mfungwa.

Na hapo ndipo nilipopata
taarifa chache za Thabo Bester,Kwamba mwaka 2006 Thabo Bester alikutana na Nandipha magudumana katika mchezo wa Tennes na majukwaa tofauti ya maonyesho. Bester alikuwa ni mjanja mjanja alijihusisha na mitindo na uimbaji.

Ndiko kulikofanya akutane
na Nandipha mara kwa mara sababu wakati huo Nandipha pia alikuwa akijitafuta kupitia uwana mitindo.walikuwa ni wadogo urafiki wao ulianzaia hapoMaisha yaliendelea huku Bester akiwa ni kijana wa mtaani tu! Asiye na kazi wala uhakika wa kula milo mi3, kuishi kwake hata kusoma kwake kuli tegemea juhudi zake.

Ni kijana aliyetelekezwa na wazazi wake kwa kuachwa na bibi yake, lakini bibi pia alikuwa ni mlevi wa kutupwa.Alijikuza mwenyewe, hakukuwa na mtu wa kumwambia ili fanya lile usifanye, yeye alifanya chochote ili mkono uende kinywani.

Alikuwa ni tapel katika mitaa ya Durban na Cap Town, vijana wenzake wakamuita chokolaa Mwaka 2009 Thabo Bester alikamatwa kwa tuhuma za utapeli na alihukumiwa miaka Miwili jera.Akiwa jera alipitia maswahibu mazito, alibakwa na kundi la wafungwa kisha akaingiziwa chupa sehemu ya haja kubwa.

Watu hao walidai Bester ana mali kwenye mwili wake ivyo walimlazimisha azitoe Baada ya tukio hilo Bester alipeleka malalamiko mahakamani.

Kwamba huko jera wafungwa kadhaa humfanyia mchezo mchafu, lakini mahakama haikutaka kusikiliza malalamiko hayo.

ikatupilia mbali mashtaka na kumuacha Bester aendelee kusota hapo jera.
Hakikupita kipindi jamaa zake aliofahamiana nao walikuja na kumtoa.Thabo Bester akarejea tena uraiani.
Akiwa uraiani akili na mawazo yake yote yaliwaza pesa, jamaa zake wakampa dili mbalimbali za kuiba vitu vya samani.

Anamuonekano mzuri "Body Language" hata jamaa zake waliliona hilo, walimtumia kuwalaghai wanawake.

Aliijua vyema mitandao ya kijamii Aliitumia hiyo kujiingizia mamilioni ya pesa, mtandao aliokuwa akipenda kuutumia ni Facebook.

ndani ya mtandao huo alitapeli makundi ya wanawake.

Aliijua miji mingi ya South Africa, miji mikubwa na maarufu alikuwa na nyumba hapo au pango kwa ajili ya kufanya kazi zake za kitapeli.

Mwaka 2011 mwezi wa7 Thabo Bester alijitambulisha kama mtu anayetokea kwenye kampuni ya kuandaa matamasha ya mitindo, aliwafanyia usahili wanawake wengi ambao walilazimika kulipia pesa za usahili.

Akiwa anatumia jina la Tom kelly, alikodi mabasi mawili na kwenda Cap Town ndani ya mabasi hayo kulikuwa na warembo aliotoka nao Johannesburg.

Kulikuwa na wapiga picha waliokuwa na vifaa vyao vya kazi, safari hii ya kwenda Cap Town ilikuwa ni yakwenda kuwapiga picha warembo hao ambao tayari walisha lipia pesa za usahili wa awali na pesa za upigaji picha.

Walipofika Cap Town, Bester alilipia chakula cha mchana na kuandaa kikao kifupi.

Akawataka wapiga picha wake pamoja na warembo waache vitu vyao vyote kwenye mabasi kwa sababu za kiusalama.

Thabo Bester ambaye sasa alifahamika kama Tom Kelly, aliwatuma vijana wake wakaiba vitu vyote vilivyopo kwenye mabasi hayo.

Kisha yeye akawa wa kwanza kwenda kuripoti polisi kuwa wameibiwa mali zao na vifaa vyao hivyo.

Kati ya warembo hao alikuwepo pia Nandipha Magudumana ambaye Wakati huo tayari alikuwa anasoma chuo na huku akiendelea kufanya uwana mitindo.

View attachment 2922308View attachment 2922309
I will be back, I mean no malice to nobody

Salute to wisdom,
Naifatilia hii kesi nadipha alikua na chance ya kuplay victim ila apperence yake na thabo beaster siku wamekutana mahakamani imemcost mnoo sijui kama atashinda hii case.
 
Yule manzi ni nyoka wa chini chini, ninge kuwa hakimu ninge muhukumu anyongwe tu.
Yes tamaa imemponza alikua na kila kitu kazi nzuri, mume na watoto ila akacha vyote sababu ya tamaa ya mali.
Imemcost sana kwenye dhamana ile appearance yake aisee ila anaweza akatoboa kwa kupunguziwa adhabu si uliona juzi kesi ilivyotajwa alimpita thabo kama hamjui.
 
Episode 2.

Ulikuwa ni muendelezo wa Nandipha na Thabo Bester kuendelea kufahamiana.

Kila mmoja alikuwa na namba ya mwenzie ivyo waliendelea kuwasiliana, lakini kikapita kipindi wakapotezana.

Nandipha alikomaa na chuo,

Huku mtaani Bester akiendelea kuwaibia watu kwa njia mbalimbali za udanganyifu,
alikuwa akitumia majina mengi kama, Thabo Bester, Thabo Magagulu, Kelly Johnson, Rufus Mahopo, Tom kelly, Thomas Bester, Thomas Better, TK, Thomas Kelly Young, Kelly Young na Thomas Magagulu. Yote hayo ni majina yake.

Mwaka 2012 Thabo Bester alikutana na mwanamke alipokwenda kununua gari kwenye kampuni ya BMW,

mwanamke huyo aliyefahamika kwa jina la Nomfundo Thyulu alikuwa akifanya kazi hapo na alikuwa mwanamitindo pia.
FwkQ9lIWwAAc84K.jpeg


Bester alizungumza kwa Lugha ya kutongoza, NAMFUNDO akajaa, penzi likazaliwa.

NAMFUNDO alimpenda BESTER na zaidi BESTER alikuwa ni mzungumzaji mzuri mwenye maneno ya kulaghai hasa linapokuja swala la kitu anachokitaka.

Ndipo weekend moja walipo kubaliana kuonana,
Bester alikwenda Cape Town, akalipia hotel na usiku ulipofika Bester aliamka akimuacha NAMFUNDO kitandani, alikwenda mpaka sebleni alichukua kisu kisha akarudi chumbani.

Hatua kadhaa kutoka alipolala NAMFUNDO, BESTER alinyanyua kisu chake lakini wakati huo NAMFUNDO alishituka usingizini na ndipo walipoanza kugombania kisu.

Ni kweliii
Mvutano uliendelea na kisha kisu kikatua kwenye kifua cha NAMFUNDO, damu nyingi zikaanza kumtoka.,
hapo ndipo Bester anapoamua kuchukua simu, pesa, na Laptop ya NAMFUNDO na kutoka nje ya hotel.

Kabla ya kufungua mlango mkubwa wa nje macho ya Bester yana gongana na mtu mmoja ambaye alikuwa ni msimamizi wa hotel hiyo.

Sasa tayari yalikuwa ni majira ya saa 10 alfajiri.
Ana mwambia ana hitaji usafiri ili aweze kuwahi anapokwenda.!!

Msimamizi wa hotel aliamua kumpatia Bester lift sababu yeye pia alikuwa anataka kwenda kununua baadhi ya mahitaji,
ambayo asubuhi hiyo yangetumika kuandalia breakfast ya hotelini hapo.

Wakiwa njiani Bester ali msisitiza msimamizi kwamba mchumba wake amemuacha chumbani amelala.

Hivyo aliomba asisumbuliwe mpaka yeye atakapo rudi hotelini hapo.

Yalipofika majira ya saa8 mchana msimamizi akapata wasiwasi baada ya kuona Bester hakurudi mpaka muda huo.
na ndipo msimamizi alipolazimisha chumba hicho kufunguliwa.

NAMFUNDO alikutwa akiwa amefariki na swala la kumpata Bester likabaki kitendawili.

Bester hakuishia hapo aliwatapeli tena wanawake wawili pesa nyingi na kisha akawabaka wote kwa mpigo,
na kutokomea zake kama afanyavyo siku zote.

Mara hii Askari waliifahamu sura ya Bester kupitia CCTV Camera ambazo kabla au baada ya tukio Camera ziliinasa Sura ya Bester.

Thabo Bester akakamatwa na kuhukumiwa kifungo jera, akiwa jera ndipo kesi ya Namfundo Thyulu ilipo ibuka.
"Umemuua mwanamke huyo kwa kumchoma kisu na kuiba mali zake"Hakimu alisema Huku akisoma makosa mengine ambayo yange mfunga Thabo Bester miaka 50 jera.

Bester alisimama na kujitetea.Akisema...

"Nimekuwa mtu ninayekosa haki tokea udogoni mwangu, Kwanza mama akatoroka na kuniacha na bibi, bibi naye alikuwa ni mraibu wa pombe.

Marafiki zake walio onyesha kunisaidia walinifungia ndani week nzima na kunibaka, nilipo mwambia bibi hakutaka kusikia habari hizo.

Thabo Bester alisema.Na aliendelea kusema
Nimezaliwa South Africa ni nyumbani lakini hapo nyumbani Hakuna mtu anayenipenda,
utotoni nimekuwa nikiitwa chokolaa, nililichukia sana hilo jina nilifanya kila nililoweza ili kuukwepa umaskini.

Bester ambaye siku hii aliongea mbele ya pirato kwa huzuni kubwa, alisema maisha yake yametawaliwa na maumivu makubwa na sio Furaha,

Aliongeza kwamba aliendelea tena kubakwa mara kadhaa na Jamaa wakaribu na bibi yake mpaka ikabidi aende kwa Daktari na kufanyiwa oparesheni sehemu ya haja kubwa.

Alipachukia nyumbani na hiyo ndio ikawa sababu ya kuwa kijana wa mtaani.

Bester ali endelea kusema tena

"Nilihama nyumbani na kwenda mtaani niliona huko ni sehemu sahihi, nilijitafutia Chakula huko na marafiki ambao walikuwa ndio Ndugu niliowatazama.
Na ndipo nilipoanza kuonyeshwa njia ya kutengeneza pesa kwa kutumia cheki fake,

Bester ali endelea kusema kuwa ali fanya yote haya sababu ya hali ngumu ya maisha.


Bester hakuishia hapo aliendelea kujitetea juu ya kuhusiswa na kumua NAMFUNDO, alisema yeye na NAMFUNDO ni watu waliopendana asingeweza kumuua mpenzi wake,

siku hiyo walikuwa na ugomvi wa kimapenzi juu ya NAMFUNDO kumuona yeye na mwanamke mwingine.

ugomvi wa wivu ni jambo linalotokea kwenye mapenzi, nikawaida siku lichukulia kama tukio kubwa".

Bester alisema..Aliongeza kwamba..Wakiwa hotelini mida ya usiku alikwenda sebleni na kuchukua kisu Kwaajili ya kumenya tunda lililo karibu na kitanda chao.

na ndipo NAMFUNDO alipomuona ameshika kisu !!.
Pengine baada ya ugomvi alihisi mimi nataka kumpiga, nisingeweza kufanya ivyo huku nimeshika kisu ikiwa najua madhara ya kisu".
Bester alijitetea kwamba ilitokea kama ajali tu, baada ya mvutano kisu kikatua kwenye kifua cha NAMFUNDO.

kwa hofu akaondoka na kumuacha mpenzi wake akiwa na jeraha la kisu ambalo lilisababisha kifo chake.
Licha ya Bester kujitetea hakimu hakutaka kuelewa chochote, akampiga mvua ya miaka 50 jera.
You are very cruel"Hakimu alisema huku akijitayarisha kwa kushika nyundo na kusoma hukumu hiyo.


Thabo Bester alikwenda gerezani na kukitumikia kifungo hicho kwenye gereza la Mangaung, gereza ambalo lipo chini ya ulinzi mkali, likilindwa na kampuni ya kimataifa G4s.Story za Bester zikaishia hapo.

Salute to wisdom,

I will be back. I mean no one to nobody.
FwkQoxlWIAAgJ0n.jpeg
 
Yes tamaa imemponza alikua na kila kitu kazi nzuri, mume na watoto ila akacha vyote sababu ya tamaa ya mali.
Imemcost sana kwenye dhamana ile appearance yake aisee ila anaweza akatoboa kwa kupunguziwa adhabu si uliona juzi kesi ilivyotajwa alimpita thabo kama hamjui.
Yule mi ninge hukumu anyongwe, wame fanya maasi sana
 
Back
Top Bottom