mapenzi yananisumbua

mapenzi yananisumbua

miaka saba hote hiyo uliishije????yaani uachane na mtu miaka saba bado unaendelea kumpenda??

kwangu mimi haya ni maajabu, miaka 7 umeshindwa kumsahau?unahitaji miaka mingapi tena iliuweze kukubaliana na hali halisi?
 
katika mahusiano / mapenz hakuna kitu kibaya kama kulinganisha ulikotoka na uliyenae cha msingi maadam hauko na ex basi songa mbele na huyo uliyenae na ikiwezekana mbadili awe kama uliyeachana nae .. pia week tatu ni chache sana kwa kuweza kuelewa mwisho
 
Hutaki kuchokozwa eeh!! 🙂🙂....Ni viwango rafiki ndio vinavyowarudisha wapenzi kwa maex, pamoja na kuwa wamepita huku na kule lakini kiwango cha juu bado ni cha mmoja tu. Unashangaa ex wa uteenager bado anataka utangaze ndoa tena kwa kuja juu kupita kiasi na machozi debe!!! Unabaki mdomo wazi tu.

unanichokoza rafiki....
Ila swali la amu ni kama hiyo miaka 7 yote alikuwa yupo yupo tu au alikuwa na mwingine. mimi yule wangu anakuwa na wangine but anaona hawajafikia kiwango, lol!
 
natamani siku nichukue mabinti woooteeee nikae nao kitako tuulizane hili swali kwanza....
what do u mean unaposema huwezi kupenda tena? who is he? kwani ulianzaje kumpenda huyo uliyeachana naye na utashindwa kupenda mwingine? ana nini zaidi?
huku ni kujifunga mwenyewe. na ni wewe mwenyewe ndo unaweza kujifungua. usitegemee atatokea mtu mfano wa malaika ili akufanye umpende. wewe mwenyewe ndo unatakiwa ku-let it go na kukaribisha penzi jipya.....
msiniambie hayajanikuta..... nilishapenda saaaanaaaaa, nikaumizwa saaanaaaaa, nikaumwa hadi kulazwa..... but look at me now.... I am enjoying uteja wangu, na mtu mwingineeeeee, maisha yanasonga

Mi namwelewa maana yashanikuta lakn nlikuja kugundua tatizo la hii kitu ni ule ujinga wa kufanya comparison ya cha jana na cha leo

Kama cha jana kikibaki kuwa the best kwa namna yoyote ile obvious there will be no room for someone new
 
Mi namwelewa maana yashanikuta lakn nlikuja kugundua tatizo la hii kitu ni ule ujinga wa kufanya comparison ya cha jana na cha leo

Kama cha jana kikibaki kuwa the best kwa namna yoyote ile obvious there will be no room for someone new
kwa nini uendelee kukaa na kitu kilichokufa moyoni?
comparison inaanzia wapi tena wakati yule alishapita?
 
Hutaki kuchokozwa eeh!! 🙂🙂....Ni viwango rafiki ndio vinavyowarudisha wapenzi kwa maex, pamoja na kuwa wamepita huku na kule lakini kiwango cha juu bado ni cha mmoja tu. Unashangaa ex wa uteenager bado anataka utangaze ndoa tena kwa kuja juu kupita kiasi na machozi debe!!! Unabaki mdomo wazi tu.
ha haaaa, hakuna lolote.....
hajaamua tu kupenda tena
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Viwango vya ex vikiwa ni vikubwa sana basi kupenda tena inakuwa si rahisi, unalijua hilo rafiki.....Chezeya viwango vya juu weye!!!! Utadhani uko peponi!!!!
no comment........:A S-confused1:
 
  • Thanks
Reactions: BAK
pole bt jitahid kumwambia mpenzi wako mpya akufanyie vitu ambayo unahisi unamiss kutoka kwake ambayo x wako alikuwa anakufanyia
 
duh...sasa unakuwa unfair kwa jamaaa huyo ila mhm siku tatu no mawasiliano...inaelekea jamaa mwenye na hakufeeel kivile yupo kimgegwdo zaidi au papuchi bado hujatoa?
 
habari wana MMU...ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya.
ningependa kuwashirikisha hili coz najua nitapata mawazo mbalimbali ya kujenga na si kubomoa hivyo naomba michango yenu ya dhati.
imepita miaka kama saba hivi tangu nimeachana na niliyekuwa nikimpenda kwa dhati na mpaka sasa ninampenda,tatizo nimeingia kwenye relationship na mwanaume mwingine tuna kama wiki tatu, lakini naona kama sio mtu sahihi kwangu coz moyo wangu bado unampenda my ex sijui nifanyaje naombeni mawazo yenu.

je niendelee na huyuhuyu au? note:huyu wa sasa naweza nikakaa hata siku tatu hata ngapi bila kuwasiliana naye na nikaona ni sawa tu.
Huyo ulienae nae hakupendi bora hata usimpende utaumia sana baadae, maana kama anamaliza siku tatu hajawasiliana na wewe wa kazi gani huyo, tafuta mwingine atakaekupenda na wewe utampenda tu na ndo atakaekufanya umsahau huyo wa zamani
 
Miaka saba unamkumbuka ur ex what the hell is he.....? Vp yeye bado anakukukmbuka......? Actual bado bado hujampata mtu sahihi endelea kusubiri.
 
habari wana MMU...ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya.
ningependa kuwashirikisha hili coz najua nitapata mawazo mbalimbali ya kujenga na si kubomoa hivyo naomba michango yenu ya dhati.
imepita miaka kama saba hivi tangu nimeachana na niliyekuwa nikimpenda kwa dhati na mpaka sasa ninampenda,tatizo nimeingia kwenye relationship na mwanaume mwingine tuna kama wiki tatu, lakini naona kama sio mtu sahihi kwangu coz moyo wangu bado unampenda my ex sijui nifanyaje naombeni mawazo yenu.

je niendelee na huyuhuyu au? note:huyu wa sasa naweza nikakaa hata siku tatu hata ngapi bila kuwasiliana naye na nikaona ni sawa tu.

Wa kwanza uliaachana naye kwa sababu zipi?
 
Naona takriban wengi wenu mumebase kwenye ngono tu wakati mapenzi yanahusu mambo mengi kama vile ukarimu, mapenzi, mahaba, huruma na mengi mengineo likiwemo hilo la ngono. Kama kweli umepata kiumbe unaempenda kwa dhati ya moyo wako na penzi kuliweka pahala linapostahili yaani MOYONI basi mpenzi wa aina hiyo si rahisi kumsahau hata kama inatokezea sababu mukaachana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom