Mwaka 2007 nilikutana na kijana mtanashati sana. Kweli nilimpenda sana sina uhakika kama na yeye alinipenda pia. Nilitoa muda wangu mwingi kwake. Lakini siku moja tu alikata kabisa mawasiliano na mimi. Kweli nililia sana nilichanganyikiwa sana. Nikafanikiwa kwenda nyumbani kwake maeneo ya Tabata aroma. Nikamuomba aniambie kwanini hapokei simu yangu.
Akaniambia kuwa mimi sijasoma na yeye alikuwa anataka kuoa msomi. Kiukweli nilijiunga na Qt nikasoma kwa bidii mpaka nikafanikiwa kufika kidato cha nne na hatimae kidato cha sita mwisho chuo. Namshukuru sana X wangu kwa kuniumiza maana yale maumivu ndio yamenifikisha hapa nilipo sasa.
Akaniambia kuwa mimi sijasoma na yeye alikuwa anataka kuoa msomi. Kiukweli nilijiunga na Qt nikasoma kwa bidii mpaka nikafanikiwa kufika kidato cha nne na hatimae kidato cha sita mwisho chuo. Namshukuru sana X wangu kwa kuniumiza maana yale maumivu ndio yamenifikisha hapa nilipo sasa.
