Wawili wanaoitwa wapendanao wameoana kwa sherehe na vifijo,sasa mmoja au wote wanatoka nje ya ndoa.Swali kwa nini watoke nje ya ndoa?Wamechokana au kuna tatizo baina yao?Ndo watoke nje ya ndoa?Wenye kutoka nje ya ndoa wanamaanisha ni kwa wenzao?Hawana mapenzi na kwanini wamewaoa/kuolewa nao? Piga picha mume/mke anavua nguo tena kwa khiari yake kwa asiye mume/mke wake,je kweli kuna mapenzi kwa walioona wenye michezo kama hii.Ajabu kuna kesi nyingi za usaliti wa ndoa kwa viongozi dini,serikali za mitaa na mahakama za mwanzo.Ndugu zangu hivi kuna mapenzi ya kweli baina ya mume na mke kwa sasa? Nasubiri michango yenu