Mapenzi ya jinsia moja chanzo ni hiki

Himidini

JF-Expert Member
May 8, 2013
5,534
4,185
^^^
Kila mmoja wetu amesikia tabia hii ambayo inakua kwa kasi sana katika dunia Lakini pia tatizo ambalo linafanywa siri katika jamii nyingi.Pamoja na sababu nyingi zinazotolewa kukuza tatizo hili ikiwemo kuporomoka kwa maadili,athari za utandawazi n.k Lakini wataalamu wafuatao wanabainisha sababu ifuatayo ambayo kwa dhati yangu,,bado nina utata na ningependa wana MMU tujadiliane;

^^^
Dkt Howard Hendricks anasema kuwa... "Upendo usio wa kawaida,unaopita kiasi ambao mtoto huupata kutoka kwa wazazi wake,,huua kabisa uwezo wa kijana kuwapenda vijana wa jinsia tofauti ambao huwa ni wa rika lake.Wakati mwanamke hapati upendo kutoka kwa mumewe mara nyingi atajaza pengo hilo katika moyo wake kwa kumpenda sana mtoto wake wa kiume kuliko kawaida.Hata ingawa hawezi kufikiria kufanya chochote kibaya na kijana huyo ila upendo huo huleta kuua kabisa ujasiri wake wa kuanzisha uhusiano na wenzake wa jinsia tofauti..."
^^^
Tim Lahaye yeye anasema "...Msichana anapomchukia sana na kumkataa kabisa baba yake kwa sababu ambazo anazijua yeye au kutokana na kukua akiona jinsi baba yake anavyokaripiwa na mama yake basi anaweza kuwachukia kabisa wanaume..."

^^^
Wataalamu hao wawili wanaonya kuwa upendo unaozidi kiasi wa wazazi au chuki iliyokithiri katika familia huathiri watoto na kuwasababisha wajiingize katika vitendo vya ulawiti,kuchelewa kuingia katika ndoa,ulevi au kushamiri katika mapenzi ya jinsi moja

^^^
 
Back
Top Bottom