MMU!
Ni utumwa au Uhuru? Ukiwa katika mapenzi, unakuwa hauna privacy. Muda wowote mpenzi wako anaweza akachukua simu yako na kuipekua.
Wengine unakuta mpenzi wako anakuwa na passwords zako za akaunti zako za benki, na hata za mitandao ya kijamii.
Kwa baadhi ya ndoa, kama mwanamke ni mwajiriwa au mjasiriamali, atafanya kazi, siku ya mwisho kipato chote anakikabidhi kwa mume.
Kwa baadhi ya ndoa, unapangiwa namna ya kuvaa, marafiki mpaka maadui.
Kama si utumwa ni nini? Na kama ni utumwa, mbona tunayalilia mapenzi?
Beauty Eva mapenzi siyo utumwa bali ni sehemu Tu ya maisha ambayo unapaswa kuishi hivyo. Kuwa ndoa huwa kwa kiasi Fulani hukupunguzia Uhuru Fulani katika maisha yako ambao uliweza kuufanya wakati uko nje ya ndoa lakini haimanishi kuwa umekuwa mtumwa.
Kuhusu privacy ya wanandoa. Labda niulize why kuwe na privacy wakati mmekuwa Kitu kimoja? Ukweli ni kwamba ndoa ina misingi yake misingi hiyo ikikiukwa ndoa huvunjika Tu au isipovunjika basi wahusika hukosa furaha katika ndoa hiyo.
1 lazima kuwe na Upendo wa dhati
2 lazima kuwe na kuaminiana kati ya wanandoa
3 heshima kati ya wanandoa wanandoa lazima waheshimiane
4 kuthaminiana wanandoa lazima wathaminiane
5 uvumilivu. Wanadamu tumeumbwa na mapungufu mengi hivyo tunapokuwa kwenye ndoa ni lazima tukubali mapungufu ya wenzi wetu kama yanarekebishika turekebishane kwa Upendo na unyenyekevu.
6 ushirikiano familia ni kama kiwanda hufanya kwa utegemeano wa mitambo ya kiwanda hivyo hivyo na familia lazima mume na make washirikiane katika kujenga familia yao
Kwa mantiki hiyo.
1 usiri ni sumu na panga zuri Tu la kuvunja ndoa maana hujenga dhana ya kutokuaminiana japo yapo ambayo yanaweza yakawekwa kama Siri lakini kumbuka pia mume au mke ndo huwa MTU wa karibu kuliko MTU mwingine maishani mwako sasa kwanini umfiche Kitu Fulani ?,kwa faida ya nani?
2 ndoa huondoa Uhuru wa kitoto na kuingia katika Uhuru was kiutu uzima.hivyo Uhuru wa kiutu uzima hauathiriki na kuwa kwenye ndoa.
3 kuhusu namna ya kuishi kwa wenzi hilo ni chaguo la wanandoa wenyewe ndiyo maana Kitu cha muhimu sana katika ndoa ni mazungumzo ni lazima wana ndoa wazungumze na kuelewana juu ya tabia na namna ya kuishi kwao kwenye ndoa huwezi kuishi maisha ya kwenye adolescent age .
Kwa maana hiyo ndoa siyo utumwa.
Na kwa urembo wako wewe ukikutana na HUSBAND MATERIAL HAUTAJUTIA KUOLEWA.