nimejaribu kusoma kwa makini sana lakini sijakuelewa hata kidogo.
naomba urekebishe uandishi wako ili ueleweke ama la Baba V aje atutafsirie.
sioni kuwa mstaarabu hata kidogo ambae anataka kutenda unyama kisa hajapewa huduma-fadhila!tupo pamoja brodah!!
But unamwonaje yul;e mtu anayetaka hadi kutenda unyama juu ya mtu kisa tu hajalipwa fadhila ya penzi alokuwa analitaka??
Wana MMU herini ya mwaka mpya!
Nawapenda sana,
Haya naombeni mnijibu swali langu hili kama mapenzi/upendo ni fadhila?.
Sijui kama mtanielewa lakini naombeni mnielewe tu manake nimekuwa nakosa jibu juu ya swali hili.
Kila siku utakuta mtu analalamika mie bwana fulan nilimfanyia hivi bi fulan ama mie bi fulani nilimtendea hivi bwana fulani nikijua atakuwa mume/mke lakini mwisho wa siku kaniacha kaoa/kaolewa na mwingine.
sasa je wewe ulitenda hayo ili ulipwe fadhila?
Eeeka mbee!!
Mie ninachojiuliza ina maana mtu ategemee kulipwa fadhila ya ndoa baada ya msaada aloutoa?? manake kwa jinsi niwazavyo mimi haipaswi kuwa hivi.
imagine mtu anadai nimemsomesha binti fulan nikijua atakubali kuolewa na mimi............kweli??
ina maana msingeyafanya asingekuoa sio??
Wana MMU herini ya mwaka mpya!
Nawapenda sana,
Haya naombeni mnijibu swali langu hili kama mapenzi/upendo ni fadhila?.
Sijui kama mtanielewa lakini naombeni mnielewe tu manake nimekuwa nakosa jibu juu ya swali hili.
Kila siku utakuta mtu analalamika mie bwana fulan nilimfanyia hivi bi fulan ama mie bi fulani nilimtendea hivi bwana fulani nikijua atakuwa mume/mke lakini mwisho wa siku kaniacha kaoa/kaolewa na mwingine.
sasa je wewe ulitenda hayo ili ulipwe fadhila?
Heri ya mwaka mpya nawe ''Neambatso baana''
Hii kitu imekuwa kama kulipa fadhila. Baadhi ya wanawake pia wameweka akili yao hivyo... Nimewahi kung'ang'aniwa kulipwa fadhila kwa namna hio na wasichaa tofauti... kila mmoja nilikua msaada kwake kwa namna flani hivi. Na mamna waliodhani kunishukuru waliona kusema asante haitoshi ni hadi ngono maana wengi wanafikiri tunaithamini sana (si kweli).... Hii dunia hii!!..... Pia baadhi yetu wanaume tunatumia shida za wanawak kujinufaish kingono au kimahusiano.... Hii ni mbaya
Nachojua ni kitu kibaya sana kutumia SHIDA au MATATIZO Ya mwanadamu mwenzako kujinufaisha kwa jina la MSAADA.
Ila ikawa kupitia msaada mengine yametokea na hayakuwa msingi wa huo msaada... well and fine.
spare my ribs mwl khaaa!!Hawa watroto tangu wamepewa hizo tablets huko mashuleni imekuwa taabu tupu utaskia mara c, x, mxuka,xana,,xhenzi.... kungekuwa na button ya kofi humu wangenikoma wallah.
Mapenzi ni mabaya ndo maana hakuna anayeyafurahia wala kujivunia %#http://
nikianza na maandiko ni kwamba upendo huleta fadhila kutoka kwa Mungu na si kwa mwanadamu manake upendo ni amri ya Mungu.Heri ya mwaka mpya na wewe pia,
Bestito mm nadhani nitakuwa mbali kidogo hapa kwenye mada hii
1. Mara nyingi katika upendo wowote wa kikawaida lazima ukifanyia mtu panapokuwepo na kafadhila kidogo
ila katika mapenzi hiyo kitu sijaona kabisa.
2. Katika maandiko hunena kuwa upendo uondoa wingi wa hasira, na huleta fadhila sasa sijui katika mapenzi inakuwaje
Hivi kuna umuhimu wa kumtendea mema/fadhila yule umpendaye au ni kule kuonesha kuwa unampenda kwa kufanya hivyo?
my brooKaribu Mae!
Yap, Tunawaza sawa kwenye hili.... Haipaswi kuwa hivi kabisa... acha upendo uhamue katikati yenu.... si kujitolea au zawadi ndio ziamue uelekeo wa upendo wa mmoja wapo.... hii kusaidia kwa kigezo cha kuja kuoana ndio mara nyingi inasababisha watu wanaolewa au kuoa wasiowapenda.. ila kwa sababu anamuonea mwenzake huruma.. au pengine kwa kuhesabu gharama alizoingia kwa ajili yake.
Ndio maana haishauriwi kabisa kufanya kitu chochote cha kipamoja(partnership) kama biashara, kujenga, kununua kiwanja au vinginevyo wakati wa uchumba kwa kuwa wanajua baadae mawazo ya mmoja yanaweza kubadilika the hivo vitu vikawa ndio kinachomshikilia kwenye huo uhusiano (sio mapenzi tena)
Ukitaka uishi maisha yasiyokuwa na majuto na kuumia roho kirahisi rahisi.... Jitahidi kufanya vitu kwa moyo na jitahidi kupunguza matarajio (expectations) maana kinachowaumiza wengi ni matarajio yao kutofikiwa na wale wanaotegemewa kufikia.
yaani umeongea mapwoint bestito ila sasa hawa jamaa wa mjengoni hapa wamekiondoa kitufe cha like
sijui kwanini ajamani