Siri ya sifuri
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 2,014
- 1,498
Ninaempenda alishanieleza bayana kuwa haitowezekana kuwa na uhusiano wa mapenzi, ila kwa urafiki wa kawaida hana kikwazo. Japo haja nipa sababu nilishaelezwa na wanaomfahamu tatizo alilonalo na nimejiridhisha.
Sasa kuna huyu ambae sinahajanae ni king'ang'anizi sana, alianza kujilengesha kwangu kitambo sana nikampotezea baadae akaamua kufunguka yeye mwenyewe kwamba ananihitaji kwa maisha(yaani amenipenda na ataka sana tuwe wapenzi) binafsi sipendi kuwa na uhusiano na yeye ingawaje simchukii kwasababu ni binaadamu mwenzangu na sijawahi kugombana naye.
Awali alikua mpole na mnyenyekevu sana kwangu lakini tangu nimuhakikishie kwamba haitawezekana Mimi na yeye kuwa wapenzi amebadilika na sasa anaonekana kutumia nguvu na maarifa kuhakikisha anafanikiwa lengo lake, hakika simpendi na ubabe anaojaribu kunifanyia ili kunishinikiza nikubali kuwa nae ndio anazidi kuharibu.
Hata hivyo nami nimekua na maswali yakujiuliza iweje yule anaeonesha kunipenda na kunihitaji kwa hali yoyote ile Mimi nikose upendo na pengine hata huruma kwake, lakini hapohapo kuna asienipenda na pengine hata kunihurumia Mimi ndio nalizimisha kupendwa kwa gharama yoyote ile!?
Sasa kuna huyu ambae sinahajanae ni king'ang'anizi sana, alianza kujilengesha kwangu kitambo sana nikampotezea baadae akaamua kufunguka yeye mwenyewe kwamba ananihitaji kwa maisha(yaani amenipenda na ataka sana tuwe wapenzi) binafsi sipendi kuwa na uhusiano na yeye ingawaje simchukii kwasababu ni binaadamu mwenzangu na sijawahi kugombana naye.
Awali alikua mpole na mnyenyekevu sana kwangu lakini tangu nimuhakikishie kwamba haitawezekana Mimi na yeye kuwa wapenzi amebadilika na sasa anaonekana kutumia nguvu na maarifa kuhakikisha anafanikiwa lengo lake, hakika simpendi na ubabe anaojaribu kunifanyia ili kunishinikiza nikubali kuwa nae ndio anazidi kuharibu.
Hata hivyo nami nimekua na maswali yakujiuliza iweje yule anaeonesha kunipenda na kunihitaji kwa hali yoyote ile Mimi nikose upendo na pengine hata huruma kwake, lakini hapohapo kuna asienipenda na pengine hata kunihurumia Mimi ndio nalizimisha kupendwa kwa gharama yoyote ile!?