Kabewa
Senior Member
- Oct 30, 2009
- 136
- 56
UTHABITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika kupambana na ufisadi nchini, umetiliwa shaka, siku chache baada ya aliyekuwa mwanachama mwandamizi wa NCCR-Mageuzi, Mabere Marando, kujiunga nacho.
Shaka hiyo inatokana na kile kilichoelezwa na baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa, dhima aliyonayo Marando ndani na nje ya chama hicho, kuhusiana na mapambano dhidi ya ufisadi ambayo yamekuwa yakipewa kipaumbele na chama hicho cha upinzani.
Marando ambaye ni mwanasheria kitaaluma na wakili wa kujitegemea, ni mmoja wa mawakili wanaotetea watuhumiwa wa kesi za ufisadi wa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Katika kesi hizo, Marando anatetea washtakiwa wawili ambao ni Jayant Kumar Jeetu Patel, mwenye kesi nne katika Mahakama hiyo; namba 1153/08, 1154/08, 1155/08 na 1157/08 na Esther Mary Komu mwenye kesi namba 1164/08.
Shaka hiyo inatokana na kile kilichoelezwa na baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa, dhima aliyonayo Marando ndani na nje ya chama hicho, kuhusiana na mapambano dhidi ya ufisadi ambayo yamekuwa yakipewa kipaumbele na chama hicho cha upinzani.
Marando ambaye ni mwanasheria kitaaluma na wakili wa kujitegemea, ni mmoja wa mawakili wanaotetea watuhumiwa wa kesi za ufisadi wa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Katika kesi hizo, Marando anatetea washtakiwa wawili ambao ni Jayant Kumar Jeetu Patel, mwenye kesi nne katika Mahakama hiyo; namba 1153/08, 1154/08, 1155/08 na 1157/08 na Esther Mary Komu mwenye kesi namba 1164/08.