Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,107
- 52,832
HAKUNA DHULMA YA MILELE, ISIYO LIPWA.
‘Mwili uliolala milele hauwezi kuamka, lakini unaweza kuzungumza ukweli kuliko mwili unaoamka kila siku’ – Pragya Santra.
Kila nyumba ina stori yake, ndoto zake, siri zake na matumaini ya watu wanao ishi na walio wahi kuishi humo. Nyumba moja mjini New York ilikuwa na siri nzito iliyotunzwa kwa miaka zaidi ya 30. Kuna mtu aliamini siri hiyo haitafichuka kamwe kwa sababu mwili wa mtu aliyemuua kwa siri umelala na hauzungumzi. Hakujua kuwa miili iliyolala inazungumza, tena ukweli zaidi kuliko miili isiyolala.
Siku ya Tarehe 2, mwaka 1999 familia ya Bw. Ronald Cohen ilikuwa inahama kutoka nyumba moja kwenda nyumba nyingine huko jijini New York. Katikati ya shughuli ya kutoa vyombo nje, Bw. Cohen aligundua kuna pipa ndani ya nyumba hiyo ambalo alilikuta miaka tisa iliyopita wakati akihamia ndani ya nyumba hiyo. Pipa hilo lilihifadhiwa kwenye stoo ndogo iliyokuwa chini ya ngazi za kupandia ghorofani. Bw. Cohen hakuwahi kulifungua pipa kwa sababu lilikuwa limefungwa kisawasawa na pia lilikuwa na lebo ya kemikali. Baba huyo wa familia hakujua kuna kemikali gani ndani ya pipa lile, na hakuona haja ya kufungua kemikali zisizomuhusu, kwa hiyo aliamua kuliacha kama alivyolikuta miaka tisa iliyopita. Lakini wasaidizi wake waliamua kulitoa nje, lichukuliwe na wazoa taka. Waliamini hakuna kitu cha maana ikiwa mmiliki wa awali wa nyumba hiyo aliliacha na hakuwahi kulitafuta kwa miaka tisa.
Kwa mshangao kidogo, wakati wakianza safari ya kuhama makazi hayo, Bw. Cohen aligundua kuwa takataka zote zilibebwa na wazoa taka isipokuwa lile pipa zito walilotoa wasaidizi wake. Kutazama vizuri kwenye pipa hilo kulikuwa na karatasi ya maelezo ambayo bila shaka iliachwa na wazoa taka. Bw. Cohen alishuka kwenye gari na kwenda kusoma karatasi ile.
‘Mpenzi mteja, tumeshindwa kubeba pipa hili kwa sababu ni zito mno. Tafadhali piga simu idara ya mazingira wafanye mpango maalum wa kuliondoa’ – Ulisomeka ujumbe kwenye karatasi ile.
Hapo ndipo Bw. Cohen alipohamasika kutaka kujua kuna nini ndani ya pipa lile. Alitafuta kisu na kukata utepe mgumu ulioshikiza mfuniko wa pipa lile na kisha akatumia chuma kuumegua mfuniko huo uliokuwa umeshikana sawasawa na pipa lile. Punde tu alipofanikiwa kulifungua, Bw. Cohen alikutana na harufu kali. Kutazama vizuri, aliona kitu kama kiganja cha mtu na kiatu cha kike. Polisi wa kitongoji cha Jericho waliitwa na kuchukua pipa lile hadi kwenye kituo kikubwa cha uchunguzi wa kimahakama.
Kila kitu kilitolewa kutoka ndani ya pipa lile. Mwili wa mwanamke uliooza kana kwamba ume hifadhiwa humo kwa miaka mingi. Pia kulikuwa na vipande vingi vya plastiki vyenye umbo la mfano wa punje za mchele, na mkoba mdogo wa kike, na mfano wa majani yaliyotengenezwa kwa plastiki.
Chini kabisa kulikuwa na majimaji ya ajabu yenye rangi ya ugoro, labda ni majimaji yaliyotoka kwenye mwili wa mwanadamu huyo aliyeoza. Ndani ya mkoba kulikuwa na karatasi zilizoharibika kabisa kiasi kwamba hazikuweza kusomeka. Yale majimaji yaliharibu kabisa zile karatasi ambazo labda zingetoa muelekeo wa kumtambua mtu huyo.
Wachunguzi wa kimahakama waliobobea katika taaluma ya patholojia wali uchunguza mwili ule na kugundua mambo kadhaa; moja, baadhi ya meno ya marehemu yalionesha kuwa yaliwahi kufanyiwa ukarabati wa kitabibu na kuwekewa nakshi maalumu. Utaratibu huo haukuwa ukifanyika nchini Marekani bali maeneo ya Amerika ya Kusini. Pili, wataalamu waligundua ni mwili wa mwanamke tena alikuwa mjamzito. Uchunguzi wa mionzi ya Xray ulionesha kichanga chenye ukubwa wa inchi 17, karibu kabisa kujifungua.
‘Mwili uliolala milele hauwezi kuamka, lakini unaweza kuzungumza ukweli kuliko mwili unaoamka kila siku’ – Pragya Santra.
Kila nyumba ina stori yake, ndoto zake, siri zake na matumaini ya watu wanao ishi na walio wahi kuishi humo. Nyumba moja mjini New York ilikuwa na siri nzito iliyotunzwa kwa miaka zaidi ya 30. Kuna mtu aliamini siri hiyo haitafichuka kamwe kwa sababu mwili wa mtu aliyemuua kwa siri umelala na hauzungumzi. Hakujua kuwa miili iliyolala inazungumza, tena ukweli zaidi kuliko miili isiyolala.
Siku ya Tarehe 2, mwaka 1999 familia ya Bw. Ronald Cohen ilikuwa inahama kutoka nyumba moja kwenda nyumba nyingine huko jijini New York. Katikati ya shughuli ya kutoa vyombo nje, Bw. Cohen aligundua kuna pipa ndani ya nyumba hiyo ambalo alilikuta miaka tisa iliyopita wakati akihamia ndani ya nyumba hiyo. Pipa hilo lilihifadhiwa kwenye stoo ndogo iliyokuwa chini ya ngazi za kupandia ghorofani. Bw. Cohen hakuwahi kulifungua pipa kwa sababu lilikuwa limefungwa kisawasawa na pia lilikuwa na lebo ya kemikali. Baba huyo wa familia hakujua kuna kemikali gani ndani ya pipa lile, na hakuona haja ya kufungua kemikali zisizomuhusu, kwa hiyo aliamua kuliacha kama alivyolikuta miaka tisa iliyopita. Lakini wasaidizi wake waliamua kulitoa nje, lichukuliwe na wazoa taka. Waliamini hakuna kitu cha maana ikiwa mmiliki wa awali wa nyumba hiyo aliliacha na hakuwahi kulitafuta kwa miaka tisa.
Kwa mshangao kidogo, wakati wakianza safari ya kuhama makazi hayo, Bw. Cohen aligundua kuwa takataka zote zilibebwa na wazoa taka isipokuwa lile pipa zito walilotoa wasaidizi wake. Kutazama vizuri kwenye pipa hilo kulikuwa na karatasi ya maelezo ambayo bila shaka iliachwa na wazoa taka. Bw. Cohen alishuka kwenye gari na kwenda kusoma karatasi ile.
‘Mpenzi mteja, tumeshindwa kubeba pipa hili kwa sababu ni zito mno. Tafadhali piga simu idara ya mazingira wafanye mpango maalum wa kuliondoa’ – Ulisomeka ujumbe kwenye karatasi ile.
Hapo ndipo Bw. Cohen alipohamasika kutaka kujua kuna nini ndani ya pipa lile. Alitafuta kisu na kukata utepe mgumu ulioshikiza mfuniko wa pipa lile na kisha akatumia chuma kuumegua mfuniko huo uliokuwa umeshikana sawasawa na pipa lile. Punde tu alipofanikiwa kulifungua, Bw. Cohen alikutana na harufu kali. Kutazama vizuri, aliona kitu kama kiganja cha mtu na kiatu cha kike. Polisi wa kitongoji cha Jericho waliitwa na kuchukua pipa lile hadi kwenye kituo kikubwa cha uchunguzi wa kimahakama.
Kila kitu kilitolewa kutoka ndani ya pipa lile. Mwili wa mwanamke uliooza kana kwamba ume hifadhiwa humo kwa miaka mingi. Pia kulikuwa na vipande vingi vya plastiki vyenye umbo la mfano wa punje za mchele, na mkoba mdogo wa kike, na mfano wa majani yaliyotengenezwa kwa plastiki.
Chini kabisa kulikuwa na majimaji ya ajabu yenye rangi ya ugoro, labda ni majimaji yaliyotoka kwenye mwili wa mwanadamu huyo aliyeoza. Ndani ya mkoba kulikuwa na karatasi zilizoharibika kabisa kiasi kwamba hazikuweza kusomeka. Yale majimaji yaliharibu kabisa zile karatasi ambazo labda zingetoa muelekeo wa kumtambua mtu huyo.
Wachunguzi wa kimahakama waliobobea katika taaluma ya patholojia wali uchunguza mwili ule na kugundua mambo kadhaa; moja, baadhi ya meno ya marehemu yalionesha kuwa yaliwahi kufanyiwa ukarabati wa kitabibu na kuwekewa nakshi maalumu. Utaratibu huo haukuwa ukifanyika nchini Marekani bali maeneo ya Amerika ya Kusini. Pili, wataalamu waligundua ni mwili wa mwanamke tena alikuwa mjamzito. Uchunguzi wa mionzi ya Xray ulionesha kichanga chenye ukubwa wa inchi 17, karibu kabisa kujifungua.