Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,146
- 48,388
Nimeshangazwa kuwa andiko lenyewe kumbe lilikusudiwa liwe ni kwa ajili ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, lakini limekuwa ni nyaraka kwa umma (Public document)
Kwa mujibu wa andiko lenyewe, ni kwamba kundi la watu 55 liliandika barua hiyo kwenda kwa Katibu baada ya kuingia hofu kwamba maoni yao hayatasikilizwa kwenye kikao kilichokuwa kimeitishwa na Ofisi ya Katibu Mkuu na kutarajiwa kufanyika tarehe 03/04/2025, siku ambayo tamko lao lilitolewa.
Kitu ambacho sikielewi ni kwa nini watu wa G55 waliamini kuwa kwenye kikao kilichokuwa kimeitishwa hawatasikilizwa bali watasikilizwa kwa kuandika barua!?
G55 kama orodha ya waliomo ni ya kweli, wengi wao walikuwa ni viongozi wa makao makuu, hii hofu ya kutokusikilizwa inatokana na nini. Au ni picha gani wanayojaribu kuijenga kwa jamii?
Wenyewe kwenye waraka wao wanasema hofu yao ya kutosikilizwa inatokana na mambo makuu matatu.
1. Kauli ya Mwenyekiti Tundu Lissu aliyoitoa kwenye mkutano wa hadhara Iringa kuwa "wote wanaoona No reforms No Election haiwezekani, ni wana-CCM na vibaraka wao"
2. Kauli iliyotolewa na mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema kwenye mkutano Arusha kuwa " wote wanaotaka ubunge na udiwani bila reforms waondoke CHADEMA ".
3. Maandiko ya Maria Sarungi yanaonesha kuna lengo la kushughulikia wale wanaopinga harakati za No reforms No Election.
Kwa hivyo hayo mambo matatu ndiyo sababu ya G55 kuandika waraka kwenda kwa Katibu Mkuu badala ya kwenda kuhudhuria kikao walichokuwa wamealikwa.
Hoja zao Kuu ni hizi.
1. Haiwezekani kuzuia uchaguzi.
2. Mchakato wa uchaguzi Mkuu umeshaanza.
Kwenye maelezo yao wanasema kuwa No reforms ilianzia kwenye Retreat ya Kamati Kuu huko Makuweni Kenya January 2020. Kwa maana nyingine kulikuwa na "reforms" bila ya neno "No Election" kuwepo.
G55 wanasema matatizo ya rasirimali na mikakati ndani ya CHADEMA yakirekebishwa na kutafutiwa ufumbuzi uhakika wa kushinda uchaguzi 2025 upo.
Wanasema kuwa chama kisiposhiriki uchaguzi wa mwaka huu 2025, chama kitakumbwa na mambo yafuatayo:
1. Kuondokewa na wanachama waliotaka kuwagombea kwenye uchaguzi 2025
2. Chama kitapoteza mvuto na kudhalilishwa Kwa propaganda za CCM
3. Chama kupoteza ruzuku
4. Wanachama wataona hakuna sababu ya kuchangia chama kama hakitashiriki uchaguzi.
5. Watia nia kuacha kuwekeza kwenye chama.
Pia kwenye waraka husika wamesema kuwa lengo la chama ni kushika dola na ni haki ya wanachama kugombea kwa kufuata Katiba ya CHADEMA hivyo kama CHADEMA isiposhiriki uchaguzi huo itakuwa inakiuka haki hiyo ya wanachama.
Mwisho aliyesaini (John Mrema) anasema kuwa wao wapo 55 ila wanawakilisha zaidi ya watia nia 200 Tanzania nzima.
Nitaichambua barua yenyewe kwa ujumla wake.
Kwanza maudhui ya barua ni kuonesha kuwa No reforms No election hakuwa ni mpango wa chama.
Kwa ivo awali chama kilikuwa kinawaza kuwe na " reforms" bila ya kujali kuwa zisipokuwepo chama kitapata athari gani?
Yaani lengo lilikuwa ni nini hasa walipotaka reforms? Walitaka zipatikane ama zisipatikane?
Wao hiyo January 2020 walipokutana huko Makuweni Kenya, walikubaliana reforms zisipopatikana wakae kimya? Sasa walitaka reforms za nini wakati hata zisipopatikana kumbe hakuna shida?
Lakini hivi hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa CHADEMA kutoshiriki uchaguzi? Kama tuliwahi kuamua kutoshiriki chaguzi kadhaa zilizopita, kwa nini Sasa kina Mrema wanasema itakuwa ni kukiuka haki za wanachama.
Wakati kina Mrema walipokuwa viongozi hawakuwahi kuhimiza wanachadema wasishiriki chaguzi mbali mbali kwa maamuzi ya chama. Wakati huo haki za wanachama zilikuwa hazivunjwi?
CHADEMA hatujawahi kuacha kushiriki chaguzi na vyama vingine vikashiriki. Hivyo vyama vimepata faida gani kwa kushiriki chaguzi hizo na sisi tulipata hasara gani?
Mara ngapi watu wanagombea kupitia CHADEMA na baadae kuhama chama. Leo inakuwaje tuwaze kuwa watu watahama CHADEMA kisa hatushiriki uchaguzi?
Hao kina John Silinde, Joshua Nassari, zitto Kabwe, Nusrat Hanje, mtela Mwampamba, Jesca Kishoa, Peter Msigwa na wengineo waliahama CHADEMA kwa kuwa hatukushiriki uchaguzi?
Nadhani waraka umejaa lugha zilizotarajiwa kutolewa na CCM dhidi ya CHADEMA na siyo mtizamo wa kutolewa na wanachadema.
Waraka mzima umejaa maelezo kuonesha kuwa tunao uwezo wa kuilazimisha CCM kuwa ya kistaarabu lakini haiwezekani kuilazimisha CCM hiyo hiyo kuona umuhimu wa kufanya uchaguzi baada ya kufanya marekebisho ya Sheria mbali mbalimbali za kiuchaguzi.
Mifano imetolewa kwenye waraka kuonesha inawezekana kushinda uchaguzi Kwa Sheria zilizopo lakini hawaelezi uwezo huo ulikuwa wapi wakati uchaguzi mzima unaibwa mwaka 2019, 2020, na 2024.
Nani asiyejua kuwa matendo ya kihuni ya CCM na watendaji wasimamizi wa uchaguzi yanalindwa kimfumo na Sheria za uchaguzi na za nchi zilizopo?
Muda wa kupambana kuzuia uchaguzi nje ya uchaguzi haupo ila kuzuia uchaguzi ndani ya uchaguzi inawezekana. Hapa Hawa jamaa wana mantiki kweli?
Kama kujaribu kuzuia uchaguzi nje ya uchaguzi ni jinai, ni kivipi kuzuia uchaguzi ndani ya uchaguzi isiwe jinai?
Waraka wenyewe unahitaji viraka vingi sana ile uwe na mantiki ya kueleweka
.
Kwa mujibu wa andiko lenyewe, ni kwamba kundi la watu 55 liliandika barua hiyo kwenda kwa Katibu baada ya kuingia hofu kwamba maoni yao hayatasikilizwa kwenye kikao kilichokuwa kimeitishwa na Ofisi ya Katibu Mkuu na kutarajiwa kufanyika tarehe 03/04/2025, siku ambayo tamko lao lilitolewa.
Kitu ambacho sikielewi ni kwa nini watu wa G55 waliamini kuwa kwenye kikao kilichokuwa kimeitishwa hawatasikilizwa bali watasikilizwa kwa kuandika barua!?
G55 kama orodha ya waliomo ni ya kweli, wengi wao walikuwa ni viongozi wa makao makuu, hii hofu ya kutokusikilizwa inatokana na nini. Au ni picha gani wanayojaribu kuijenga kwa jamii?
Wenyewe kwenye waraka wao wanasema hofu yao ya kutosikilizwa inatokana na mambo makuu matatu.
1. Kauli ya Mwenyekiti Tundu Lissu aliyoitoa kwenye mkutano wa hadhara Iringa kuwa "wote wanaoona No reforms No Election haiwezekani, ni wana-CCM na vibaraka wao"
2. Kauli iliyotolewa na mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema kwenye mkutano Arusha kuwa " wote wanaotaka ubunge na udiwani bila reforms waondoke CHADEMA ".
3. Maandiko ya Maria Sarungi yanaonesha kuna lengo la kushughulikia wale wanaopinga harakati za No reforms No Election.
Kwa hivyo hayo mambo matatu ndiyo sababu ya G55 kuandika waraka kwenda kwa Katibu Mkuu badala ya kwenda kuhudhuria kikao walichokuwa wamealikwa.
Hoja zao Kuu ni hizi.
1. Haiwezekani kuzuia uchaguzi.
2. Mchakato wa uchaguzi Mkuu umeshaanza.
Kwenye maelezo yao wanasema kuwa No reforms ilianzia kwenye Retreat ya Kamati Kuu huko Makuweni Kenya January 2020. Kwa maana nyingine kulikuwa na "reforms" bila ya neno "No Election" kuwepo.
G55 wanasema matatizo ya rasirimali na mikakati ndani ya CHADEMA yakirekebishwa na kutafutiwa ufumbuzi uhakika wa kushinda uchaguzi 2025 upo.
Wanasema kuwa chama kisiposhiriki uchaguzi wa mwaka huu 2025, chama kitakumbwa na mambo yafuatayo:
1. Kuondokewa na wanachama waliotaka kuwagombea kwenye uchaguzi 2025
2. Chama kitapoteza mvuto na kudhalilishwa Kwa propaganda za CCM
3. Chama kupoteza ruzuku
4. Wanachama wataona hakuna sababu ya kuchangia chama kama hakitashiriki uchaguzi.
5. Watia nia kuacha kuwekeza kwenye chama.
Pia kwenye waraka husika wamesema kuwa lengo la chama ni kushika dola na ni haki ya wanachama kugombea kwa kufuata Katiba ya CHADEMA hivyo kama CHADEMA isiposhiriki uchaguzi huo itakuwa inakiuka haki hiyo ya wanachama.
Mwisho aliyesaini (John Mrema) anasema kuwa wao wapo 55 ila wanawakilisha zaidi ya watia nia 200 Tanzania nzima.
Nitaichambua barua yenyewe kwa ujumla wake.
Kwanza maudhui ya barua ni kuonesha kuwa No reforms No election hakuwa ni mpango wa chama.
Kwa ivo awali chama kilikuwa kinawaza kuwe na " reforms" bila ya kujali kuwa zisipokuwepo chama kitapata athari gani?
Yaani lengo lilikuwa ni nini hasa walipotaka reforms? Walitaka zipatikane ama zisipatikane?
Wao hiyo January 2020 walipokutana huko Makuweni Kenya, walikubaliana reforms zisipopatikana wakae kimya? Sasa walitaka reforms za nini wakati hata zisipopatikana kumbe hakuna shida?
Lakini hivi hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa CHADEMA kutoshiriki uchaguzi? Kama tuliwahi kuamua kutoshiriki chaguzi kadhaa zilizopita, kwa nini Sasa kina Mrema wanasema itakuwa ni kukiuka haki za wanachama.
Wakati kina Mrema walipokuwa viongozi hawakuwahi kuhimiza wanachadema wasishiriki chaguzi mbali mbali kwa maamuzi ya chama. Wakati huo haki za wanachama zilikuwa hazivunjwi?
CHADEMA hatujawahi kuacha kushiriki chaguzi na vyama vingine vikashiriki. Hivyo vyama vimepata faida gani kwa kushiriki chaguzi hizo na sisi tulipata hasara gani?
Mara ngapi watu wanagombea kupitia CHADEMA na baadae kuhama chama. Leo inakuwaje tuwaze kuwa watu watahama CHADEMA kisa hatushiriki uchaguzi?
Hao kina John Silinde, Joshua Nassari, zitto Kabwe, Nusrat Hanje, mtela Mwampamba, Jesca Kishoa, Peter Msigwa na wengineo waliahama CHADEMA kwa kuwa hatukushiriki uchaguzi?
Nadhani waraka umejaa lugha zilizotarajiwa kutolewa na CCM dhidi ya CHADEMA na siyo mtizamo wa kutolewa na wanachadema.
Waraka mzima umejaa maelezo kuonesha kuwa tunao uwezo wa kuilazimisha CCM kuwa ya kistaarabu lakini haiwezekani kuilazimisha CCM hiyo hiyo kuona umuhimu wa kufanya uchaguzi baada ya kufanya marekebisho ya Sheria mbali mbalimbali za kiuchaguzi.
Mifano imetolewa kwenye waraka kuonesha inawezekana kushinda uchaguzi Kwa Sheria zilizopo lakini hawaelezi uwezo huo ulikuwa wapi wakati uchaguzi mzima unaibwa mwaka 2019, 2020, na 2024.
Nani asiyejua kuwa matendo ya kihuni ya CCM na watendaji wasimamizi wa uchaguzi yanalindwa kimfumo na Sheria za uchaguzi na za nchi zilizopo?
Muda wa kupambana kuzuia uchaguzi nje ya uchaguzi haupo ila kuzuia uchaguzi ndani ya uchaguzi inawezekana. Hapa Hawa jamaa wana mantiki kweli?
Kama kujaribu kuzuia uchaguzi nje ya uchaguzi ni jinai, ni kivipi kuzuia uchaguzi ndani ya uchaguzi isiwe jinai?
Waraka wenyewe unahitaji viraka vingi sana ile uwe na mantiki ya kueleweka
.