Maoni yangu kuhusu utenguzi wa Athuman Diwani Msuya

James Hadley Chase

JF-Expert Member
Mar 25, 2020
1,578
2,664
JANA nilipokuwa UTV (Azam TV), nikifanya mahojiano kipindi cha Morning Trumpet, niliulizwa maoni yangu kuhusu mabadiliko ambayo Rais Samia aliyafanya juzi (Mei 3), Ikulu na Idara ya Usalama wa Taifa (Tiss).

Nilijibu kuwa sikuona msingi wowote wa kumwondoa Diwani Athuman Tiss, alipokuwa Mkurugenzi Mkuu na kumhamisha kuwa Katibu Mkuu Ikulu.

Kama alikuwa tatizo Tiss, maana yake watu wangetafsiri yale matatizo yake yangehamia Ikulu. Tiss na Ikulu ni taasisi zinazofanya kazi kwa upacha.

Mwisho nilisema sikuona mabadiliko bali chekecheo. Wa huku anawekwa pale. Nikasema Rais Samia mwenyewe ndiye anajua msingi wa uamuzi wake. Sisi wa nje hatujui.

AMBACHO SIKUKISEMA

Diwani amekuwa Boss wa Tiss nyakati ambazo Tanzania ilikuwa gizani totoro.

Utekaji na upoteaji watu.
Dola ilikithiri ubabe na ukandamizaji.
Miili ya watu iliokotwa baharini.
Watu waliporwa fedha zao halali benki.
Wafanyabiashara waliporwa viwanda vyao.
Wafanyabiashara walifilisiwa.
Uchaguzi Mkuu 2020 ulivurugwa.

Kisisahaulike Kikosi Kazi kilichoundwa kukusanya madeni ya kodi. Kiliwabambikia kesi za uhujumu uchumi wafanyabiashara. Fedha zikalipwa akaunti za watu binafsi.

Kuna mzaha wa Covid-19. Maradhi yakaletwa siasa. Watanzania wengi wakapoteza maisha.

Ongeza na mengine mengi ikiwemo wabunge na madiwani wa upinzani kununuliwa kwa fedha nyingi, kisha uchaguzi kurudiwa. Rushwa na ufujaji mkubwa wa fedha uliofanyika kwa lengo la kumfurahisha mtu mmoja.

Mambo yote hayo yalitendeka Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa chini ya Diwani.

Kipindi ambacho nchi iliihitaji Tiss imara na yenye uthubutu mkubwa, Diwani hakuifanya idhihirishe uwepo wake kwa ajili ya usalama kamili wa taifa. Tiss haipaswi kuwa idara yenye kuchezewa na wanasiasa. Tiss ni moyo wa nchi.

Kwa muktadha huo, sikuona sahihi kumpeleka Diwani Ikulu. Alipaswa kuwekwa kando.

Leo, uteuzi wa Diwani Ikulu umetenguliwa kabla hajaapishwa. Binafsi nimeona ni sahihi kabisa.

Iwe aligomea uteuzi wa kuwa Katibu Mkuu Ikulu kutoka DG Tiss au Rais Samia amebadili uamuzi baada ya tafakuri (afterthought), vema Diwani akae pembeni.

Nchi inahitaji hewa safi.
Tiss inahitaji usafi mkubwa.
Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Credit: Luqman MALOTO
 
Rais ndiye anajua. Hayo hayatuhusu. Sisu tunalia na unga, mahindi, maharage n.k
Lakini uteuzi ni wa rais tusimwingilie. Ana washauri wake.
 
Hivi sasa kila mtu anajua kila kitu....

Ndio raha ya uhuru wa.kutoa maoni

Kuna vijamaa vitajifanya vinajua kuliko Taasisi ya urais.... Vinafikiri maamuzi ya Ikulu anayafanya mama peke yake....
 
JANA nilipokuwa UTV (Azam TV), nikifanya mahojiano kipindi cha Morning Trumpet, niliulizwa maoni yangu kuhusu mabadiliko ambayo Rais Samia aliyafanya juzi (Mei 3), Ikulu na Idara ya Usalama wa Taifa (Tiss).

Nilijibu kuwa sikuona msingi wowote wa kumwondoa Diwani Athuman Tiss, alipokuwa Mkurugenzi Mkuu na kumhamisha kuwa Katibu Mkuu Ikulu.

Kama alikuwa tatizo Tiss, maana yake watu wangetafsiri yale matatizo yake yangehamia Ikulu. Tiss na Ikulu ni taasisi zinazofanya kazi kwa upacha.

Mwisho nilisema sikuona mabadiliko bali chekecheo. Wa huku anawekwa pale. Nikasema Rais Samia mwenyewe ndiye anajua msingi wa uamuzi wake. Sisi wa nje hatujui.

AMBACHO SIKUKISEMA

Diwani amekuwa Boss wa Tiss nyakati ambazo Tanzania ilikuwa gizani totoro.

Utekaji na upoteaji watu.
Dola ilikithiri ubabe na ukandamizaji.
Miili ya watu iliokotwa baharini.
Watu waliporwa fedha zao halali benki.
Wafanyabiashara waliporwa viwanda vyao.
Wafanyabiashara walifilisiwa.
Uchaguzi Mkuu 2020 ulivurugwa.

Kisisahaulike Kikosi Kazi kilichoundwa kukusanya madeni ya kodi. Kiliwabambikia kesi za uhujumu uchumi wafanyabiashara. Fedha zikalipwa akaunti za watu binafsi.

Kuna mzaha wa Covid-19. Maradhi yakaletwa siasa. Watanzania wengi wakapoteza maisha.

Ongeza na mengine mengi ikiwemo wabunge na madiwani wa upinzani kununuliwa kwa fedha nyingi, kisha uchaguzi kurudiwa. Rushwa na ufujaji mkubwa wa fedha uliofanyika kwa lengo la kumfurahisha mtu mmoja.

Mambo yote hayo yalitendeka Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa chini ya Diwani.

Kipindi ambacho nchi iliihitaji Tiss imara na yenye uthubutu mkubwa, Diwani hakuifanya idhihirishe uwepo wake kwa ajili ya usalama kamili wa taifa. Tiss haipaswi kuwa idara yenye kuchezewa na wanasiasa. Tiss ni moyo wa nchi.

Kwa muktadha huo, sikuona sahihi kumpeleka Diwani Ikulu. Alipaswa kuwekwa kando.

Leo, uteuzi wa Diwani Ikulu umetenguliwa kabla hajaapishwa. Binafsi nimeona ni sahihi kabisa.

Iwe aligomea uteuzi wa kuwa Katibu Mkuu Ikulu kutoka DG Tiss au Rais Samia amebadili uamuzi baada ya tafakuri (afterthought), vema Diwani akae pembeni.

Nchi inahitaji hewa safi.
Tiss inahitaji usafi mkubwa.
Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Credit: Luqman MALOTO
Tuache uzuzu kwani Rais Hassan hakuwa Makamu wa Rais nyakati za Magufuli, tuache upofu wa akili na maarifa, Hii ni collective accountability, integrity na professional services.

Everything that happened was jointly executed.

Na kuhusu Viroba msitukumbushe Alshabab wenu Wa Kibiti, mkuranga na rufiji, Magufuli won a very difficult battle, Kikwete alishindwa kuua upandikizi ongeeni mengine sio kuhusu Viroba, Mkianza kuongelea Viroba Ikulu haitakuwa salama kabisa
 
JANA nilipokuwa UTV (Azam TV), nikifanya mahojiano kipindi cha Morning Trumpet, niliulizwa maoni yangu kuhusu mabadiliko ambayo Rais Samia aliyafanya juzi (Mei 3), Ikulu na Idara ya Usalama wa Taifa (Tiss).

Nilijibu kuwa sikuona msingi wowote wa kumwondoa Diwani Athuman Tiss, alipokuwa Mkurugenzi Mkuu na kumhamisha kuwa Katibu Mkuu Ikulu.

Kama alikuwa tatizo Tiss, maana yake watu wangetafsiri yale matatizo yake yangehamia Ikulu. Tiss na Ikulu ni taasisi zinazofanya kazi kwa upacha.

Mwisho nilisema sikuona mabadiliko bali chekecheo. Wa huku anawekwa pale. Nikasema Rais Samia mwenyewe ndiye anajua msingi wa uamuzi wake. Sisi wa nje hatujui.

AMBACHO SIKUKISEMA

Diwani amekuwa Boss wa Tiss nyakati ambazo Tanzania ilikuwa gizani totoro.

Utekaji na upoteaji watu.
Dola ilikithiri ubabe na ukandamizaji.
Miili ya watu iliokotwa baharini.
Watu waliporwa fedha zao halali benki.
Wafanyabiashara waliporwa viwanda vyao.
Wafanyabiashara walifilisiwa.
Uchaguzi Mkuu 2020 ulivurugwa.

Kisisahaulike Kikosi Kazi kilichoundwa kukusanya madeni ya kodi. Kiliwabambikia kesi za uhujumu uchumi wafanyabiashara. Fedha zikalipwa akaunti za watu binafsi.

Kuna mzaha wa Covid-19. Maradhi yakaletwa siasa. Watanzania wengi wakapoteza maisha.

Ongeza na mengine mengi ikiwemo wabunge na madiwani wa upinzani kununuliwa kwa fedha nyingi, kisha uchaguzi kurudiwa. Rushwa na ufujaji mkubwa wa fedha uliofanyika kwa lengo la kumfurahisha mtu mmoja.

Mambo yote hayo yalitendeka Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa chini ya Diwani.

Kipindi ambacho nchi iliihitaji Tiss imara na yenye uthubutu mkubwa, Diwani hakuifanya idhihirishe uwepo wake kwa ajili ya usalama kamili wa taifa. Tiss haipaswi kuwa idara yenye kuchezewa na wanasiasa. Tiss ni moyo wa nchi.

Kwa muktadha huo, sikuona sahihi kumpeleka Diwani Ikulu. Alipaswa kuwekwa kando.

Leo, uteuzi wa Diwani Ikulu umetenguliwa kabla hajaapishwa. Binafsi nimeona ni sahihi kabisa.

Iwe aligomea uteuzi wa kuwa Katibu Mkuu Ikulu kutoka DG Tiss au Rais Samia amebadili uamuzi baada ya tafakuri (afterthought), vema Diwani akae pembeni.

Nchi inahitaji hewa safi.
Tiss inahitaji usafi mkubwa.
Mungu Ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Credit: Luqman MALOTO
Unahisi Diwani anaweza kumgomea Amiri Jeshi Mkuu Komandoo SAMIA SULUHU HASSAN ?
 
Rais ndiye anajua. Hayo hayatuhusu. Sisu tunalia na unga, mahindi, maharage n.k
Lakini uteuzi ni wa rais tusimwingilie. Ana washauri wake.
Kwani wewe ni mtoto halisi wa Yusuph Makamba?

Kuona nchi nzima ni ya wapumbafu wanaotaka huduma za kijamii pekee, lakini mambo mengine yanayohusu mustakabali wao yasiwahusu?

Kwa mawazo finyu kiwango hiki, ndiyo maana wazungu hutuita "manyani" ama nusu watu!
 
Watendaji tendeni haki ila uchaguzi msitende haki only in Tz nadhani siku yake kila mtu atashangaa asiamini anachokiona. Haki ikanze kwenye box la kura mambo mengine yatafuwata. Nafurahi Dola wanaona wenyewe... Wanatumia big power kuwaweka ila wakisha ingia wao wanakuwa wahanga wa mabaya yalio tokea while wakijuwa bila hayo madhila wao wasinge shika Dola... Katiba ndio msumari wa mwisho kwa haki na uhuru wa Taifa hili.
 
Tuache uzuzu kwani Rais Hassan hakuwa Makamu wa Rais nyakati za Magufuli, tuache upofu wa akili na maarifa, Hii ni collective accountability, integrity na professional services.

Everything that happened was jointly executed.

Na kuhusu Viroba msitukumbushe Alshabab wenu Wa Kibiti, mkuranga na rufiji, Magufuli won a very difficult battle, Kikwete alishindwa kuua upandikizi ongeeni mengine sio kuhusu Viroba, Mkianza kuongelea Viroba Ikulu haitakuwa salama kabisa
Haya tunayarudia sana kuyaeleza na kuyafafanua humu kwamba hayo mauaji ya kikatili ndiyo yaliyosaidia kutimua hao majahili na kukimbilia Msumbiji.

Vinginevyo utitiri huo hadi leo ungelikuwa bado tumeuvaa.

Tukaeleza tena kuwa, tatizo lililokuwepo katika operesheni hiyo ni kutokujenga ama kuteua echelon ya kuhifadhia mateka, kuwahoji na mahali pa kuzika maiti zao kwa kuzilebo majina kama kulikuwa na mpango wa kuwaangamiza na si kuwajaza kwenye viroba kuleta taharuki ya nchi na lawama zisizokuwa za lazima kwa watawala.

Makamanda wa majeshi walioendesha operesheni pamoja na kufanya kwa ushindi mkubwa, lakini walistahili kuwajibishwa kwa kutoishauri vyema serikali namna fanisi ya kuendesha na kupigana vita hiyo.
 
Back
Top Bottom