Bufa
JF-Expert Member
- Mar 31, 2012
- 13,862
- 29,317
Mkasi kila nikijaribu kuangalia show yenu on Youtube ili kuwa updated na habari za nyumbani nazidi kuwa disappointed, badala ya kwenda mbele mnarudi nyuma. Mwishowe sitakua na budi ila kuacha kuangalia hiki kipindi.
Matatizo yale yale kila siku, mpangilio wa maswali, kuingiliana kwa waulizaji na kumuingilia anaehojiwa. Hii inatutoa watazamaji nje ya hamu ya kuendelea kuangalia kipindi
Utambulisho. Hamtoi utambulisho wa kutosha kuhusu wageni, mfano Chegere, huyu jamaa yawezekana wengi wanamjua ila naamini tuliowengi hatumjui. Kama ni uwezo wake kielimu ilibidi mtoe utambulisho wa kina ili muweze kwenda sambasamba na watazamaji. Ilibidi aulizwe alama zake ili watu wajue uwezo wake na mambo kama hayo
Mpangilio wa maswali yenu ni hovyo sana yani mnauliza hili mnaenda huku mnarudi kule mnaruka tena sijui mnatumia mfumo gani wa kuuliza maswali. Pamoja na kwamba theme ya kipindi ni kimtaa/kijiweni/maskani zaidi ila professionalism lazima izingatiwe since mnarusha kwa TV.
Nipende kutoa rai pia juu ya maswali yaulizwayo, uzito wa maswali uongezwe hasa kwa watu ambao ni "Public figures" na wageni wote kwa ujumla. Baada ya utambulisho, maswali mepesi na maswali ya kizushi ulizeni maswali mazito ambayo yataacha mchango katika jamii. Boresheni maswali yenu. Kujua maisha binafsi ya wageni kiundai isiwe main focus ya kipindi. Sio mbaya kama mtakua mnafanya research kidogo kabla hamjawahoji wageni wenu
I wonder kama hizi ni extended versions hizo short versions kwenye runinga zinakuaje smh
Matatizo yale yale kila siku, mpangilio wa maswali, kuingiliana kwa waulizaji na kumuingilia anaehojiwa. Hii inatutoa watazamaji nje ya hamu ya kuendelea kuangalia kipindi
Utambulisho. Hamtoi utambulisho wa kutosha kuhusu wageni, mfano Chegere, huyu jamaa yawezekana wengi wanamjua ila naamini tuliowengi hatumjui. Kama ni uwezo wake kielimu ilibidi mtoe utambulisho wa kina ili muweze kwenda sambasamba na watazamaji. Ilibidi aulizwe alama zake ili watu wajue uwezo wake na mambo kama hayo
Mpangilio wa maswali yenu ni hovyo sana yani mnauliza hili mnaenda huku mnarudi kule mnaruka tena sijui mnatumia mfumo gani wa kuuliza maswali. Pamoja na kwamba theme ya kipindi ni kimtaa/kijiweni/maskani zaidi ila professionalism lazima izingatiwe since mnarusha kwa TV.
Nipende kutoa rai pia juu ya maswali yaulizwayo, uzito wa maswali uongezwe hasa kwa watu ambao ni "Public figures" na wageni wote kwa ujumla. Baada ya utambulisho, maswali mepesi na maswali ya kizushi ulizeni maswali mazito ambayo yataacha mchango katika jamii. Boresheni maswali yenu. Kujua maisha binafsi ya wageni kiundai isiwe main focus ya kipindi. Sio mbaya kama mtakua mnafanya research kidogo kabla hamjawahoji wageni wenu
I wonder kama hizi ni extended versions hizo short versions kwenye runinga zinakuaje smh