Maoni: Kila Mwalimu na Mwanafunzi apimwe covid-19 kabla ya kuanza masomo

Blue Bahari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,230
1,141
Habarini wadau!
Kwa kuwa jana (17/05/2020) Mh: rais katupa matumaini ya hali nzuri ya nchi yetu na kwamba anafikiria kufungua vyuo na michezo mda si punde.

Sasa mimi nikiwa kama mdau mmojawapo wa elimu, nina pendekezo lillilo na namna mbili za kufanya:

(1) Aidha walimu na wanafunzi wapimwe covid-19 kabla hata ya shule kufunguliwa, kisha wapeleke vyeti vyao (kwa Mwalimu mkuu/Mkuu wa shule) kuthibitisha wako salama. Kisha Masomo yaendelee.

(2) Shule ikishafunguliwa, kabla ya masomo kuanza, walimu na Mwanafunzi wote wapimwe covid-19 ili kubaini nani yuko salama au ni mgonjwa.

Utaratibu wa upimaji uwe unafanyika kila baada ya wiki moja kwa kila Mwalimu na Mwanafunzi.

Nimetoa maoni hayo, kwa kuwa wanafunzi (wakiwemo na walimu) wamekuwa mtaani kwa mda mrefu wakiwa wamechangamana na watu wa aina tofauti. Hivyo, kama tutaruhusu tu wanafunzi na walimu waanze masomo kienyeji, Nina wasi wasi yanaweza kutokea kama yaliyiyotokea kule Ufaransa ambapo baada ya shule kufunguliwa, kuna bahadhi ya shule zililazimika kufunga tena baada ya bahadhi ya wanafunzi kupimwa na kugundulika kuwa covid-19 ktk shule hizo.

Hivyo, kwa usalama zaidi ya watoto wetu, ni vyema mamlaka zikashughulikia upimaji wa Mara kwa Mara kwa wanafunzi ili kuepusha balaa zito zaidi la kuambukizana covid-19 kwa kuwa kwa kiwango kikubwa kutoka ktk shule za kata, idadi ya wanafunzi ktk darasa ni 50+.

Nawasilisha.
 
Utekelezaji utakuwa mgumu sana ndugu..vipi kuhusu shule za kutwa?
Na kwa shule za boarding,ndio watapimwa,vp kuhusu walimu na wafanyakaz wengne ambao wana-interact na jamii ya nje ya shule?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabunge tu imeshindikana kupimwa licha ya kufariki wabunge watatu isitoshe walimu na wanafunzi??
Kumpima mtu mmoja tu gharama ni tsh120,000. Hizo fedha na vipimo vyenyewe tutapata wapi??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivyo vipimo ndo vina virus... Usiruhusu mwanao apimwe.
Duh! Binafsi namuunga mkono.
IMG_20200518_185405_642.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dr. Mollel wakati akiwa bado tu ni mbunge alisema ni gharama kubwa sana kupima mtu mmoja, hawawezi kupima wabunge wote, sasa ndio wapime watoto na walimu wote ? Na huyo huyo ndio kapewa rungu sasa hivi kama Naibu Waziri wa Afya?

Kitu nilichojifunza ni kutoka kwa kauli mbali mbali za viongozi wetu ni kuwa uchumi ni muhimu zaidi kuliko afya na uhai wa mtu mmoja mmoja.
 
Dr. Mollel wakati akiwa bado tu ni mbunge alisema ni gharama kubwa sana kupima mtu mmoja, hawawezi kupima wabunge wote, sasa ndio wapime watoto na walimu wote ? Na huyo huyo ndio kapewa rungu sasa hivi kama Naibu Waziri wa Afya?

Kitu nilichojifunza ni kutoka kwa kauli mbali mbali za viongozi wetu ni kuwa uchumi ni muhimu zaidi kuliko afya na uhai wa mtu mmoja mmoja.
Kwa hiyo turuhusu shule zifunguliwe kiholera. Je,hakuna hatari yoyote mbeleni kama wanafunzi wataanza masomo bila kuwapima hata joto tu?
 
Habarini wadau!
Kwa kuwa jana (17/05/2020) Mh: rais katupa matumaini ya hali nzuri ya nchi yetu na kwamba anafikiria kufungua vyuo na michezo mda si punde.

Sasa mimi nikiwa kama mdau mmojawapo wa elimu, nina pendekezo lillilo na namna mbili za kufanya:

(1) Aidha walimu na wanafunzi wapimwe covid-19 kabla hata ya shule kufunguliwa, kisha wapeleke vyeti vyao (kwa Mwalimu mkuu/Mkuu wa shule) kuthibitisha wako salama. Kisha Masomo yaendelee.

(2) Shule ikishafunguliwa, kabla ya masomo kuanza, walimu na Mwanafunzi wote wapimwe covid-19 ili kubaini nani yuko salama au ni mgonjwa.

Utaratibu wa upimaji uwe unafanyika kila baada ya wiki moja kwa kila Mwalimu na Mwanafunzi.

Nimetoa maoni hayo, kwa kuwa wanafunzi (wakiwemo na walimu) wamekuwa mtaani kwa mda mrefu wakiwa wamechangamana na watu wa aina tofauti. Hivyo, kama tutaruhusu tu wanafunzi na walimu waanze masomo kienyeji, Nina wasi wasi yanaweza kutokea kama yaliyiyotokea kule Ufaransa ambapo baada ya shule kufunguliwa, kuna bahadhi ya shule zililazimika kufunga tena baada ya bahadhi ya wanafunzi kupimwa na kugundulika kuwa covid-19 ktk shule hizo.

Hivyo, kwa usalama zaidi ya watoto wetu, ni vyema mamlaka zikashughulikia upimaji wa Mara kwa Mara kwa wanafunzi ili kuepusha balaa zito zaidi la kuambukizana covid-19 kwa kuwa kwa kiwango kikubwa kutoka ktk shule za kata, idadi ya wanafunzi ktk darasa ni 50+.

Nawasilisha.
Tatizo Nani atagharimia? Unajua idadi ya wanafunzi na waalimu Tanzania nzima?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Title inazungumzia vyuo,habari shule .
Btw muda na rasilimali za kupima walimu na wanafunzi wote haupo.
 
Kwa hiyo turuhusu shule zifunguliwe kiholera. Je,hakuna hatari yoyote mbeleni kama wanafunzi wataanza masomo bila kuwapima hata joto tu?

Tuachane na wanafunzi wa chuo tuangalie tu wa shule za msingi na sekondari.
Kutokana na takwimu za mwaka 2017:
  • Idadi ya wanafunzi wa shule zote za msingi ni 9,317,410 tuchukulie tu sasa idadi imepungua mpaka 9,000,000 (Ila siku zote huongezeka)
  • Idadi ya wanafunzi wa shule za msingi kwa 2017 iliripotiwa kuwa 1,909,017, tuchukulie tu nayo imepungua mpaka 1,900,000 (Siku zote huongezeka)
  • Sasa gharama ya kupima Corona ni 100,000 kwa mtu mmoja.
  • Fanya 9,000,000 x 100,000 = 900,000,000,000 TZS Kwa shule ya msingi
  • Fanya 1,900,000 x 100,000 = 190,000,000,000 TZS Kwa shule za sekondari
Tumla ni shilingi 1,090,000,000,000 TZS.
Hapo hatujajumlisha wafanyakazi wa shule kama walimu na bado watoto wanaosoma shule za kutwa watajichanganya tu na watoto wengine.

Je nchi inaweza kugharamia hicho kiasi cha kupima watu wasio chini ya milioni 10 ?
Je tunauwezo wa kupima hao watu milioni 10 ndani ya muda mfupi ?
Marekani mpaka leo ndio taifa pekee lililofanikiwa kupima watu zaidi ya milioni 10 na imewachukua zaidi ya miezi 2 kufikia kiwango hicho. Sisi itatuchukua muda gani ?
Screenshot from 2020-05-18 19-18-20.png

Kama lengo kuu ni kuhakikisha usalama wa raia wetu basi kulikuwa hamna haja ya kutaka kurudisha maisha kama kawaida. Lengo kuu ni kuhakikisha usalama wa uchumi. Kwa viongozi wetu uchumi ni muhimu kuliko uhai wa mtu mmoja mmoja.
 
Wazo zuri pia kila mwanafunzi awe na sanitizer, iwe ni lazima. Wazazi wawasisitize watoto kuhusu matumizi na umuhimu wake. Kwa wale wadogo zaidi, walimu wawajibike vema kuwalinda wakiwa huko shuleni
 
Tuachane na wanafunzi wa chuo tuangalie tu wa shule za msingi na sekondari.
Kutokana na takwimu za mwaka 2017:
  • Idadi ya wanafunzi wa shule zote za msingi ni 9,317,410 tuchukulie tu sasa idadi imepungua mpaka 9,000,000 (Ila siku zote huongezeka)
  • Idadi ya wanafunzi wa shule za msingi kwa 2017 iliripotiwa kuwa 1,909,017, tuchukulie tu nayo imepungua mpaka 1,900,000 (Siku zote huongezeka)
  • Sasa gharama ya kupima Corona ni 100,000 kwa mtu mmoja.
  • Fanya 9,000,000 x 100,000 = 900,000,000,000 TZS Kwa shule ya msingi
  • Fanya 1,900,000 x 100,000 = 190,000,000,000 TZS Kwa shule za sekondari
Tumla ni shilingi 1,090,000,000,000 TZS.
Hapo hatujajumlisha wafanyakazi wa shule kama walimu na bado watoto wanaosoma shule za kutwa watajichanganya tu na watoto wengine.

Je nchi inaweza kugharamia hicho kiasi cha kupima watu wasio chini ya milioni 10 ?
Je tunauwezo wa kupima hao watu milioni 10 ndani ya muda mfupi ?
Marekani mpaka leo ndio taifa pekee lililofanikiwa kupima watu zaidi ya milioni 10 na imewachukua zaidi ya miezi 2 kufikia kiwango hicho. Sisi itatuchukua muda gani ?
View attachment 1453526
Kama lengo kuu ni kuhakikisha usalama wa raia wetu basi kulikuwa hamna haja ya kutaka kurudisha maisha kama kawaida. Lengo kuu ni kuhakikisha usalama wa uchumi. Kwa viongozi wetu uchumi ni muhimu kuliko uhai wa mtu mmoja mmoja.
Uko sahihi mkuu katika estimation zako, lakini binafsi naamini "penye nia pana njia " kwa kuwa upimaji wa viashiria vya ugonjwa unaweza kufanyika kama ule wa kwenye mabasi (bahadhi ya mikoa ya mipakani mwa nchi) ambapo kila abiria hupimwa "dalili za covid-19" na kisha wale wanaohisia huwa wanatengwa na hatimaye kuchukuliwa sampuli for more diagnosis. Je, njia hii nayo si mujarabu ktk upimaji?
Umetaja marekani kama ndiyo taifa lilofanikiwa kupima idadi ya watu wengi, lakini pia kuna bahadhi ya nchi hapa barani Africa (nafikiri ni Ghana kama sijakosea) walikuja na program kabambe ya kupima watu wake mtaa kwa mtaa, sikufatilia kama waliweza.
Hivyo, kupanga ni kuchagua, kama kipaumbele ni uchumi na si usalama wa wananchi basi inabidi twende hivyo hivyo.
 
Issue ipo kwenye vipimo. Siamini serikali haina uwezo wa kuweka vipimo kila hospitali ya wilaya, Bali ni kuogopa namna ya kudhibiti taarifa. Kwa idadi ya shule tulizonazo, muda wa masomo utavurugika kwa kusubiri majibu kutoka Kenya au Uganda maana sisi maabara imefungwa.
Habarini wadau!
Kwa kuwa jana (17/05/2020) Mh: rais katupa matumaini ya hali nzuri ya nchi yetu na kwamba anafikiria kufungua vyuo na michezo mda si punde.

Sasa mimi nikiwa kama mdau mmojawapo wa elimu, nina pendekezo lillilo na namna mbili za kufanya:

(1) Aidha walimu na wanafunzi wapimwe covid-19 kabla hata ya shule kufunguliwa, kisha wapeleke vyeti vyao (kwa Mwalimu mkuu/Mkuu wa shule) kuthibitisha wako salama. Kisha Masomo yaendelee.

(2) Shule ikishafunguliwa, kabla ya masomo kuanza, walimu na Mwanafunzi wote wapimwe covid-19 ili kubaini nani yuko salama au ni mgonjwa.

Utaratibu wa upimaji uwe unafanyika kila baada ya wiki moja kwa kila Mwalimu na Mwanafunzi.

Nimetoa maoni hayo, kwa kuwa wanafunzi (wakiwemo na walimu) wamekuwa mtaani kwa mda mrefu wakiwa wamechangamana na watu wa aina tofauti. Hivyo, kama tutaruhusu tu wanafunzi na walimu waanze masomo kienyeji, Nina wasi wasi yanaweza kutokea kama yaliyiyotokea kule Ufaransa ambapo baada ya shule kufunguliwa, kuna bahadhi ya shule zililazimika kufunga tena baada ya bahadhi ya wanafunzi kupimwa na kugundulika kuwa covid-19 ktk shule hizo.

Hivyo, kwa usalama zaidi ya watoto wetu, ni vyema mamlaka zikashughulikia upimaji wa Mara kwa Mara kwa wanafunzi ili kuepusha balaa zito zaidi la kuambukizana covid-19 kwa kuwa kwa kiwango kikubwa kutoka ktk shule za kata, idadi ya wanafunzi ktk darasa ni 50+.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom