Maoni: Ifanyike tathmini ya Uchaguzi wa 2019/2020 kabla ya kufanyika uchaguzi 2024/2025

Zanzibar wamewahi jaribu Kwa njia ngumu zaidi ya hizi za kwetu katika chaguzi zao lakini wakaendelea kupotea Ushindi Kwa mabavu.

Mikakati thabiti ndiyo inayohutajika, maandamano yakiwemo.
Sijui nisemeje hapa, na huo mfano wa Zanzibar.
Nashukuru sana kukumbushia mfano huo, huo ni mchango muhimu wa kutafuta majibu kwa CHADEMA na sisi wote.

Lakini nadhani kuna tofauti kubwa sana kati ya hayo ambayo hufanyika Zanzibar, na yanayoweza kufanyika hapa Tanzania Bara kukiwa na maandalizi mazuri.

Kumbuka pia, mazingira yatakuwa ni tofauti sana wakati huu, hata huko huko CCM kwenyewe.

Ngoja tuzidi kukuna vichwa.

Na katika "mikakati thabiti", binafsi ule wa kutoshiriki uchaguzi kwa kususa tu, huo siyo mkakati hata kidogo.

"Maandamano" yakihusu nini, kudai Katiba Mpya, huku CCM akiendelea na maandalizi yake ya kufanya uhalifu kwenye uchaguzi?

Historia ya waTanzania inaonyesha siyo watu wa maandamano sana. Sijui CHADEMA watafanya juhudi zipi za ziada kuwatoa watu wa kutosha barabarani, tena bila kikomo. Hii itakuwa kazi ngumu sana!
 
Zanzibar wamewahi jaribu Kwa njia ngumu zaidi ya hizi za kwetu katika chaguzi zao lakini wakaendelea kupotea Ushindi Kwa mabavu.

Mikakati thabiti ndiyo inayohutajika, maandamano yakiwemo.
Na wakatengeneza katiba yao 'mpya' ambayo kwenye uchaguzi mkuu ikampa Maalim Seif ushindi wa asilimia 19 huku Hussein Mwinyi akipata asilimia 81 ya kura zilizopigwa. Yaani Maalim harakati zote alizokuwa anafanya kumbe kukubalika kwake ni asilimia zisizofika hata 20.
 
Maoni yangu ni kuwa, acha CCM na viongozi wao wafanyemaigizo yote wanayoweza kuyafanya, lakini inapokuja kwenye uchaguzi utakaokuja katika mazingira yoyote yale, wananchi wakiwa wameandaliwa vizuri, CCM hatafurukuta tena.

Kazi sasa ipo hapo, pa kufanya kazi na wananchi hao; kuwaelimisha na kuwapanga vizuri kuzuia uhalifu toka CCM.
Mkuu umenena vyema sana. Mwananchi ndio mwamuzi wa mwisho kuhusu kuiondoa CCM madarakani. Sasa badala ya vyama vya siasa kujipambania vyenyewe kushika dola, vingekazana kuelimisha wananchi juu ya ukuu wao dhidi ya watawala.

Vingejikita kuwaelimisha kuwa wananchi ndio wanaoweza kuamua hata nchi iwe na cheo kisichopo katibani, wao wakiamua basi nchi nzima imeamua. Waangalie Misri na Tunisia, wananchi walipata viongozi pasipo kufuata masharti ya katiba.

Sasa vyama vya upinzani kikiwemo CHADEMA, vitambue kuwa CCM hawana mpango na katiba, iwe ni mpya au ya zamani. Vipambane kuelimisha wananchi, waiondoe CCM na kulinda kura zao, halafu vikiingia madarakani vyenyewe ndio vitengeneze katiba mpya.
 
Mkuu umenena vyema sana. Mwananchi ndio mwamuzi wa mwisho kuhusu kuiondoa CCM madarakani. Sasa badala ya vyama vya siasa kujipambania vyenyewe kushika dola, vingekazana kuelimisha wananchi juu ya ukuu wao dhidi ya watawala.

Vingejikita kuwaelimisha kuwa wananchi ndio wanaoweza kuamua hata nchi iwe na cheo kisichopo katibani, wao wakiamua basi nchi nzima imeamua. Waangalie Misri na Tunisia, wananchi walipata viongozi pasipo kufuata masharti ya katiba.

Sasa vyama vya upinzani kikiwemo CHADEMA, vitambue kuwa CCM hawana mpango na katiba, iwe ni mpya au ya zamani. Vipambane kuelimisha wananchi, waiondoe CCM na kulinda kura zao, halafu vikiingia madarakani vyenyewe ndio vitengeneze katiba mpya.
Umelieleza vizuri sana hili jambo, hata kuliko nilivyo lieleza mimi hapo mwanzo.

Asante sana, mkuu 'sajo', kwa ufafanuzi huo.
 
Sijui nisemeje hapa, na huo mfano wa Zanzibar.
Nashukuru sana kukumbushia mfano huo, huo ni mchango muhimu wa kutafuta majibu kwa CHADEMA na sisi wote.

Lakini nadhani kuna tofauti kubwa sana kati ya hayo ambayo hufanyika Zanzibar, na yanayoweza kufanyika hapa Tanzania Bara kukiwa na maandalizi mazuri.

Kumbuka pia, mazingira yatakuwa ni tofauti sana wakati huu, hata huko huko CCM kwenyewe.

Ngoja tuzidi kukuna vichwa.

Na katika "mikakati thabiti", binafsi ule wa kutoshiriki uchaguzi kwa kususa tu, huo siyo mkakati hata kidogo.

"Maandamano" yakihusu nini, kudai Katiba Mpya, huku CCM akiendelea na maandalizi yake ya kufanya uhalifu kwenye uchaguzi?

Historia ya waTanzania inaonyesha siyo watu wa maandamano sana. Sijui CHADEMA watafanya juhudi zipi za ziada kuwatoa watu wa kutosha barabarani, tena bila kikomo. Hii itakuwa kazi ngumu sana!
 
Muswada wa Tume ya Uchaguzi ni changa la macho!!

Wananchi tuamue sasa au Tukae kimya milele.
 
Ikitupendeza uchaguzi ufanywe hata October 2026,

kwa kuundwa serikali ya mpito chini ya Rais huyu huyu,ili suala la KATIBA MPYA ILIYO BORA na TUME HURU ya uchaguzi vipatikane..
Una HOJA.

Ninachokupinga, ni kuwa aliyepo hafai kusimamia, sababu alikuwa na muda wa kutosha, akachagua kufanya hadaa ya maridhiano fake.
 
Ikitupendeza uchaguzi ufanywe hata October 2026,kwa kuundwa serikali ya mpito chini ya Rais huyu huyu,ili suala la KATIBA MPYA ILIYO BORA na TUME HURU ya uchaguzi vipatikane..ila kufanya uchaguzi kwa Katiba hii KUU KUU na tume hii MBOFU MBOFU,itakuwa ni sawa na kupaka Upepo RANGI...wakati wa KATIBA MPYA iliyobora ni SASA

..Raisi wa mpito huwa hagombei.

..huyu wa sasa anataka kugombea.

..kwa ujumla hana nia ya kuleta mabadiliko makubwa ya kweli.

..wanachotaka ni kufanya ni mabadiliko madogo yatakayowaingiza madarakani halafu tatizo hilo lirithiwe na awamu itakayofuata.
 
Back
Top Bottom