Mimi nimeshawahi kuota nafanya mapenzi na mwanamke kama mara mbili hv but sikumjua situation kama hii unafanyaje kujiokoa kama kuna pepo mmbaya!?IKIWA UMEFANYA MAPENZI KATIKA NDOTO, tafadhali acha unachofanya na usome hii.
Nikiwa mkoa mmoja kwenye hoteli niliyokuwa nikiishi.
Asubuhi moja mapema nilipokuwa nikielekea kupata kifungua kinywa changu, nilikutana na mvulana mmoja anayefanya kazi katika hoteli hiyo.
Niliamua kujibizana naye, nikamuita ili tujumuike kwenye kifungua kinywa, akafanya na tukaanza kuongea.
Katikati ya mazungumzo aliniambia jinsi alivyohitimu kutoka Chuo Kikuu kimoja shahada ya uchumi
Tangu hapo alianza kutafuta kazi bila kuipata hadi pale alipoamua kufika hotelini na kuwa mhudumu.
Sehemu ya kusikitisha ya hadithi ni kwamba kulingana na yeye, mtu yeyote anayeahidi kumsaidia kwa bahati mbaya hufa au kuwa masikini.
Hakuelewa maisha yake lakini aliamua kuishi nayo.
Aliniambia kuwa kila anapoahidiwa kazi au mtu anapojitolea kumsaidia, ghafla anatokea mwanamke wa ajabu na kufanya naye mapenzi ndotoni na mara baada ya hayo, ahadi hiyo inashindikana.
Watu wengi wanapitia haya.
Soma hii kwa makini!!! Kufanya mapenzi katika ndoto inamaanisha kuwa umeolewa na unalala na mapepo.
Hakuna kitu duniani chenye wivu zaidi ya mume au mke wa mapepo, ukifanya mapenzi kwenye ndoto hakuna kitakachofanya kazi kimwili kwako.
Mara unapofanya mapenzi katika ndoto, unakuwa umeacha damu yako ndani ya pepo kama mwanaume na kama mwanamke pepo ameiacha damu yake ndani yako.
Popote unapokwenda, umebeba pepo ndani yako ndiyo maana kila unachojaribu kufanya kinashindikana.
Maisha yako yatafadhaika hadi uulize kama kweli Mungu yupo au la.View attachment 2293999
Huwa nashangaa sana kusikia Mwafrika akisema kuwa asili na utamaduni wetu ni matambiko, ushirikina, uchawi na mengine mengi ya mkondo huo. Pengine ni kwa sababu hatuna taarifa za kina juu ya tamaduni za wazungu (Western countries and Europeans) na hii imetokana na Media Outlet nyingi zinaonyesha uzuri wa maisha yao lakini upande wa uovu/au historia yao ya uovu haionyeshwi kwenye media nyingi.Waafrika kuna mahali tumepigwa chenga ya mwili kisha tukaachwa solemba. Mabeberu (kwa jina pendwa la chama kikuu) walitukuta na sayansi yetu ya asili ikiwa imepiga hatua kubwa kwenye utafiti, matokeo na utendaji pia, wakaona tukiendelea nayo tutakuja kufanya makubwa na kuwaacha mbali na pengine hata kuwatawala.
Wakaona hatari na kitisho kinachowakabili. Wakaja na mbinu ya kukandia vya kwetu na kusifu vya kwao, wakafanikiwa kwenye hili. Kishapo badala ya kutufunza vya kwao vizuri wakatunyima maarifa haya.
Nasikitika kusema kwamba mwaka jana tulipanga kuwa na kongamano kubwa la wachawi na washirikina lakini lilishindikana kufanyika kutokana na serikali kutoitambua hii kaliba. Lakini cha ajabu kuna mkoa mwaka huu kuna waganga wachawi zaidi ya mia walikusanyika na kutoa ultimatum kwenye jambo la kisiasa. Imagine huo ni mkoa mmoja tu. Kuna walozi zaidi ya mia.
Kuna huyu ndugu yetu 4G LTE ameanza kutuletea simulizi za visa vya kushangaza visivyo na majibu huko Ulaya. Nina hakika visa kama hivyo vilivyokosa majibu ya kisayansi huko kwao hapa Africa vingepatiwa ufumbuzi kupitia kaliba ya ushirikina uchawi na ulozi.
Sasa hivi tumebaki tupotupo tu. Ushirikina tunaambiwa ni mbaya na hauna faida. Sayansi tunayohubiriwa kuwa ndio mkombozi tunabaniwa maarifa yake. Hebu katembelee tume ya sayansi ya Tanzania utaniambia.
Sasa ili kuweza kuwa na way forward ni vema sasa tukaandaa msimu wa kazi za kishirikina, kichawi na ulozi ili kuvunja ile miiko na dhana dhanifu kuwa hii tasnia haina mema wala faida. Maonesho husika yatasaidia kuleta mwamko mpya wa elimu ya giza, utafiti na hata matokeo yenye faida kwa jamii.
Maonesho husika yatasaidia kuondoa woga kwa baadhi ya mafundi na kufanya waoneshe kwa uwazi zana za maangamizi walizo nazo. Licha ya kuwa ni maonesho yatayakostua na kushangaza wengi lakini yatalifanya taifa lijulikane zaidi huku yakivutia utalii na kutoa msukumo wa wageni wengi zaidi kutaka kufahamu zaidi.
Najaribu kuandaa andiko mradi kisha nilipeleke wizara husika, pengine kipindi hiki tutasikilizwa.
Hapo mtu hachomoki!Hili limbwata hili
Siku hizi bora kusamehe tuuu maana janjajanja nyingi sanaKhaa ww mzee jaman afu mm niliibiwa tv radio na funguo zangu za gari naweza pata msaada
Sent from my SM-G935T using JamiiForums mobile app
Kweli aiseeSiku hizi bora kusamehe tuuu maana janjajanja nyingi sana