Habari
Kama kuna typing error usi mind sana.
Natumaini kuna watu wamepitia maisha ya kukaa au kulelewa na ndugu kwa mda mfupi au mda mrefu, na lazima kuna mambo ambayo ndugu zako watakuwa walikuwa wanaongea kwa masimango chukia au basi tu ili mradi.
Mimi nimewahii kukaa kwa ndugu kiukwelii nilikuwa mkimya na ni mtu wa watu sana na nilikuwa napiga story na watu tofauti tofauti nikiwa na maana watu wazima mabinti na hata wazee na nilikuwa ni mcheshii kiasi.
Sasa nilivyo ingia kwa ndugu kwa lengo la kuja utafuta maisha neno la kwanza waliniambia wewe hapa ni sawa na nyumbani kuwa na amani kabisa na kuwa huru.
Ila siku zilivyo zidi kwenda maneno yalianza chini kwa chini kuwa mimi nina tabia hizi:
1:kutongoza wanawake ovyo (napenda wanawake sana)
2:mimi ni mlevi balaa (wakati hapo nilikuwa mnywa wa mara moja kwa miezi 6)
3:napenda sana starehe (hii ni baada ya kuona picha za fb)
4:lazima niende motoni(kwakuwa sijawahiii kwenda kanisani tokea nije home na wala kuwa na hisia na kanisa)
Sasa mwanzo nilisikia hivyo nikajua labda ni njia ya kuwalinda mabinti zao hapo nyumbani maana wengi walikuwa ni kuanzia 4m4 na kuendelea.
Siku zikawa zina enda nikawa mkimya kupitilizaa ili kujiepusha na maneno ndo balaa likaanza.
Nakumbuka kuna manzi alikuwa ananiulizia akasema “napenda sana huyu kaka alivyo mpole halafu nilikuwa si mjui kumbe mcheshiii”.
Akawa karibu yangu sana kilichofuata walimfuata na kumwambia kuwa mimi nina ngoma na nime athirika mda sana hapa nilipo namezaa ARV, thanks god Yule demu alinielewa tulienda hadi DISPE tukapimaa na alivyo ona majibu kwa macho yake kuwa ni negative.
Alinitamkia kuwa ijumaa nakuja kulala na wewe na alikuja nikawa nakula sana ndani kwa ndani hahahahaha. Ila alisepaa baadae.
Sasa maisha yameenda nikawa napiga story na majirani kuongea na watu vizuri, balaa lingine likaja likajitokeza kuwa mimi nina:
1:Tembea na wake za watu na hapo waliwataja kabisa na kumbe huyo mama mdg nilikuwa na kaa kwake aliweka na kikao kabisa sema mimi sikuwepo. Ila list niliipata mwanzo mwisho na ukiangalia wote walikuwa wake za watu na jamaa zao walikuwa wananifahamu na hata nisipo onekana lazima waje wanitafute niende nika chill nao tu. Na walikuwa peace
2:Mimi nasambazaUKIMWI kwa majirani
3:Nimetemebea na mama mwenye ukimwi ambaee kila mtu anajuaa kuwa ame athirika.(na huyu alikuwa ni rafiki tu na tena mfanya biashara alinikubalii baada ya kutoa pesa 30,000 mtoto wake akatibiwe na alikuwa hana kitu kipindi hicho)
4
esa Napata ila zina ishia kwa wanawake (napenda kuhonga sana) wakati kipindi hicho sina hata mia
Jamani kukaa kwa ndugu kazi hasa hawa wanajiita walokolee ni ngumu sana kuishi nao.
Yanii ukiangalia sijawahiii kuwa na tabia kama hizo ila ni wao na uoga wao wakani batiza.
Thanks God saizi maisha fresh na niko na amani.
Toa neno lolote ambalo ume wahiii kusingiziwa au likakufanya mpaka leo uki mkumbuka ndugu yako ulie kaa kwake huna amani,