GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Umri wangu sio mdogo, unatosha kabisa kunifanya nami niwe Kamhenga ingawa si Mhenga kamili hivyo kama nyani mzee tu nimekwepa mishale mingi.
Miaka ya 2000+ Nilikuwa Field Lindi, Pitapita ya hapa na pale nikazama kwa mke wa mtu bila kujua (Nilidanganywa) hapo ndo nikakutana na hiyo kitu inaitwa Tego.... Mateso niliyoyapata siwezi kusahau.
Mwanzo nilifikiri ni ugonjwa wa kawaida, Namshukuru daktari mmoja ambaye aliniita chemba na kunieleza wazi kuwa tatizo ninalopambana nalo kwake Si la kawaida hivyo akanisaidia wapi niende, kweli nikapelekwa kijijini (Chiuta) na ndugu wa huyo Daktari. kuhusu mtaalam aliyenitibu kwa sasa ni Marehemu..
TATIZO LILIVYO KUWA.
Nilikuwa nakojoa mkojo mweusi kama oil chafu, nikishakojoa yalikuwa yanafuata maumivu makali ya kiuno na Sehemu za siri zilikuwa zinawaka moto na wakati mwingine kuvimba.
Nje ya yule Daktari, mdogo wake na yule mganga (Marehemu) sijawahi kumueleza yeyote siri hii, Leo naliweka hadharani ili mpate kujifunza maana ni takribani miaka 21 sasa.
Yule mzee alikataa kunisaidia mpaka pale alipojihakikishia kuwa sikutembea makusudi na Mke wa mtu. Mwisho alinionesha majani ambayo siyajui jina ambayo alisema unaweza kutumia kumgundua Mwanamke aliyetegwa.
Muhimu:
Jiepusheni na wake za watu ndugu zangu, kuna watu wanakufa bila kugundua chanzo ni hao wanawake.
Nawatakia usiku mwema.
Miaka ya 2000+ Nilikuwa Field Lindi, Pitapita ya hapa na pale nikazama kwa mke wa mtu bila kujua (Nilidanganywa) hapo ndo nikakutana na hiyo kitu inaitwa Tego.... Mateso niliyoyapata siwezi kusahau.
Mwanzo nilifikiri ni ugonjwa wa kawaida, Namshukuru daktari mmoja ambaye aliniita chemba na kunieleza wazi kuwa tatizo ninalopambana nalo kwake Si la kawaida hivyo akanisaidia wapi niende, kweli nikapelekwa kijijini (Chiuta) na ndugu wa huyo Daktari. kuhusu mtaalam aliyenitibu kwa sasa ni Marehemu..
TATIZO LILIVYO KUWA.
Nilikuwa nakojoa mkojo mweusi kama oil chafu, nikishakojoa yalikuwa yanafuata maumivu makali ya kiuno na Sehemu za siri zilikuwa zinawaka moto na wakati mwingine kuvimba.
Nje ya yule Daktari, mdogo wake na yule mganga (Marehemu) sijawahi kumueleza yeyote siri hii, Leo naliweka hadharani ili mpate kujifunza maana ni takribani miaka 21 sasa.
Yule mzee alikataa kunisaidia mpaka pale alipojihakikishia kuwa sikutembea makusudi na Mke wa mtu. Mwisho alinionesha majani ambayo siyajui jina ambayo alisema unaweza kutumia kumgundua Mwanamke aliyetegwa.
Muhimu:
Jiepusheni na wake za watu ndugu zangu, kuna watu wanakufa bila kugundua chanzo ni hao wanawake.
Nawatakia usiku mwema.