Mwitongo
JF-Expert Member
- Jan 30, 2009
- 312
- 360
Wadau yule tajiri Yusuf Manji, ameshindwa kesi na kupokwa jengo la Quality Plaza ambalo alilijenga, akaliuza kwa shirika moja la hifadhi, na kisha akawa mpangaji. Tangu alipopanga hakupata kulipa pango. Bado Tanesco nao wanamdai umeme wa mabilioni. Uamuzi umetolewa na Mahakama wiki hii, lakini jambo la ajabu ni kwamba vyombo vya habari vimekaa kimya kabisa. Hapa kuna nini? Huenda ukimya huu unatokana pia na Manji kutumia nguvu ya Mahakama kuzuia magazeti zaidi ya 10 yasimwandike kwa mazuri wala kwa mabaya! Ebu tujadili jambo hili.