Monyiaichi
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 1,826
- 508
Wana JF,
Nimeamua niandike kuhusu zabuni iliyotolewa na manispaa ya Kinondoni kwa kampuni ya Mwamkinga Auction Mart.
Labda niulize swali kwanza, lengo hasa la hizi kampuni ni nini?
Kama ni kwa ajili ya kupunguza shida zitokanazo na makosa ya madereva wanaopaki hovyo sehemu zisizoruhusiwa na barabrani, basi kitakachoendelea hapa mostly ni uonevu na ulaji wa rushwa kama ilivyokuwa kwa majembe, tena manispaa wala haitopata kodi stahiki kwa kuwa wengi watapenda kumalizana njiani bila kufikisha pesa husika kwenye ofisi husika.
Usumbufu bado ni mkubwa, wafanyakazi wa hiyo mart njaa zao ni kali hazina mfano.
Suggestion:
Kwa nini kitengo cha kufuatilia uvunjaji wa sheria barabarani kisiwekwe chini ya jeshi la polisi ambao ni wazoefu na niwahusika wa usalama barabarani?
Au ni swala la kupeana ulaji? Wengine wanaweza kujibu kuwa polisi pia wanakula rushwa, sikatai. Lakini niseme tu ukweli si polisi wote ni wala rushwa, nimeshakutana na polisi wazuri tu na waanaojituma, tena polisi huwa wanapima na extent ya kosa lenyewe kuliko hawa walafi na waongo.
Sijui wenzangu kama mme experience haya na mmeyaonaje.
Nimeamua niandike kuhusu zabuni iliyotolewa na manispaa ya Kinondoni kwa kampuni ya Mwamkinga Auction Mart.
Labda niulize swali kwanza, lengo hasa la hizi kampuni ni nini?
Kama ni kwa ajili ya kupunguza shida zitokanazo na makosa ya madereva wanaopaki hovyo sehemu zisizoruhusiwa na barabrani, basi kitakachoendelea hapa mostly ni uonevu na ulaji wa rushwa kama ilivyokuwa kwa majembe, tena manispaa wala haitopata kodi stahiki kwa kuwa wengi watapenda kumalizana njiani bila kufikisha pesa husika kwenye ofisi husika.
Usumbufu bado ni mkubwa, wafanyakazi wa hiyo mart njaa zao ni kali hazina mfano.
Suggestion:
Kwa nini kitengo cha kufuatilia uvunjaji wa sheria barabarani kisiwekwe chini ya jeshi la polisi ambao ni wazoefu na niwahusika wa usalama barabarani?
Au ni swala la kupeana ulaji? Wengine wanaweza kujibu kuwa polisi pia wanakula rushwa, sikatai. Lakini niseme tu ukweli si polisi wote ni wala rushwa, nimeshakutana na polisi wazuri tu na waanaojituma, tena polisi huwa wanapima na extent ya kosa lenyewe kuliko hawa walafi na waongo.
Sijui wenzangu kama mme experience haya na mmeyaonaje.