Mungu Tusamehe Afrika
Senior Member
- Jan 18, 2022
- 139
- 203
Kichwa cha habari chahusika.
Kumekuwa na unyanyasaji na uvunjifu wa sheria ubaofantwa na Kamishina wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Rukwa,Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa ya Sumbawanga na dalali kutoka mbeya anayeitwa Fagio Auctioneer.
Kiuhalisia dalali huyu ametafutwa na huyo Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa ya Sumbawanga kwa jina Kabaghe ambaye analipwa 10% na Fagio Auctioneer kwa pamoja na Kamishina huyo wa ardhi.
Fagio Auctioneer kulingana na marekebisho ya sheria na. 5/2021 kifungu cha 49 kifungu kidogo cha 48A haruhusiwi kufanya kazi ya udalali wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Sunbawanga kwani hajateuliwa na Msajili wa Mabaraza ya Ardhi -Tanzania kuwa Dalali au Msambaza Nyaraka za Baraza za Ardhi na Nyumba-Sumbawanga aliyeteuliwa kufanya kazi hizo yupo ila Kamishina Msaidizi wa Ardhi -Sumbawanga na huyo Mkuu wa Idara ya Ardhi Manisipaa ya Sumbawanga hawataki kumtumia kwa vile aligoma kuwapatia 10% na alikataa kuwatoza wananchi gharama za kuwasambazia wito wa Baraza la Ardhi na Nyumba bure kwa sheria hailekezi hivyo.
Wanachokifanya na kukitaka ni kuwashitaki wananchi wanaodaiwa kodi kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba Sumbawanga kisha kuwatumia vibarua kusambaza Hati za Wito kwa wanachi kwa kuwalipa pesa kidogo ya kutwa wakati wao siyo wasambaza nyaraka wa Baraza la Ardhi na Nyumba Sumbawanga na hawarejeshi kwa kiapo hati hizo kwa kiapo na baadae wananchi wanaoitika Barazani hutozwa asilimia 10% kama gharama za dalali ambazo huingia mifukoni mwao na tena wao kujilipa posho ya uendeshaji wa zoezi hilo kutoka ofisini.
Kabla hata shauri kusikilizawa barazani Fagio Auctioneer hupewa kazi hiyo ya kuwadai wananchi kodi husika pasipokuwa na sifa wala kufuata taratibu ambapo hukamata nyumba hizo na kuanza kuziuza kinyemela kitu ambacho baadae kitaiingiza serikali na wananchi kwenye mgogoro na hasara kwa tamaa zao.
Ofisi ya Kamishina Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Rukwa imekuwa ikilalamikiwa sana juu ya dhiruma na ubadhirifu hasa kwa kutengeneza migogoro ili kkujipatia fedha za rushwa chini ya kamishina huyo na Afisa Ardhi huyo Kabaghe ikiwemo kutoa hati mara mbilimbili na kudhurumu maeneo ya wananchi.
Haiingii akilini Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa Sumbawanga kwanini anakumbatiwa na ofisi ya Kamishina msaidizi wa ardhi mkoa wa Rukwa na kukalia vyeo ofisi mbili wakati watu wengine wapo huo ni urasimu.
Tunaomba mkuu wa mkoa,msajili wa mbaraza ya ardhi na waziri wa ardhi muingilie kati hawa watu wanatubyanyasa na pia kujilipa pesa za serikali kinyume na utaratibu kwa maslahi yao pasipo kufuata sheria kanuni na taratibu.
Hatukatai kushitakiwa kwa kudaiwa lakini sheria,kanuni na taratibu zifuatwe kamishina ashitaki Barazani, wadaiwa tuletewe hati za wito kupitia msambaza nyaraka wa baraza,tufike barazani, shauri lisikilizwe na baraza pasipokuingiliwa na Kamishina msaidizi wa ardhi na mkuu wa idara ya ardhi manispaa ya sumbawanga, hikumu itolewe, kamishina/mdai akishinda mdaiwa apewe muda wa kutekeleza hukumu ai kukata rufaa na akishindwa ateuliwe dalali wa baraza wa mkoa wa Rukwa atekeleze hukumu siyo aletwe dalali bora dalali, apewe notisi ya siku 14 mshindwa tuzo kulipa deni
Mshindwa tuzo akishindwa kutekeleza hukumu baraza litowe amri ya kuuza nyumba,dalali mteuliwa atanfaze kuuza kwa siku 30 baada ya uthaminishaji, nyumba ikiuzwa dalali apeleke gharama zake baraza lizipie alipwe kwanza yeye na baadae kamishina ndipo alipwe, pesa ikibaki arejeshewe mshindwa tuzo,kinyume na hapo utekelezaji wote utakuwa batili na unaweza kupingwa mahakama za juu na mshindwa tuzo kushinda.
Sasa huyu Afisa Ardhi Kabaghe yeye ni nani au anauwezo gani kuwashinda wenzie aweze kufanya kazi na kutoa maamuzi ofisi zote za ardhi mkoani Rukwa?
Ni wakati sasa atafutiwe sehemu nyingine kwani amekuwa ni tatizo katika ofisi za ardhi hapa Sumbawanga mhasibu yeye,mtunza ofisi yeye,mwanasheria yeye,transport officer yeye,hr yeye,msaidizi wa kamishina yeye,n.k.
Kumekuwa na unyanyasaji na uvunjifu wa sheria ubaofantwa na Kamishina wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Rukwa,Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa ya Sumbawanga na dalali kutoka mbeya anayeitwa Fagio Auctioneer.
Kiuhalisia dalali huyu ametafutwa na huyo Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa ya Sumbawanga kwa jina Kabaghe ambaye analipwa 10% na Fagio Auctioneer kwa pamoja na Kamishina huyo wa ardhi.
Fagio Auctioneer kulingana na marekebisho ya sheria na. 5/2021 kifungu cha 49 kifungu kidogo cha 48A haruhusiwi kufanya kazi ya udalali wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Sunbawanga kwani hajateuliwa na Msajili wa Mabaraza ya Ardhi -Tanzania kuwa Dalali au Msambaza Nyaraka za Baraza za Ardhi na Nyumba-Sumbawanga aliyeteuliwa kufanya kazi hizo yupo ila Kamishina Msaidizi wa Ardhi -Sumbawanga na huyo Mkuu wa Idara ya Ardhi Manisipaa ya Sumbawanga hawataki kumtumia kwa vile aligoma kuwapatia 10% na alikataa kuwatoza wananchi gharama za kuwasambazia wito wa Baraza la Ardhi na Nyumba bure kwa sheria hailekezi hivyo.
Wanachokifanya na kukitaka ni kuwashitaki wananchi wanaodaiwa kodi kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba Sumbawanga kisha kuwatumia vibarua kusambaza Hati za Wito kwa wanachi kwa kuwalipa pesa kidogo ya kutwa wakati wao siyo wasambaza nyaraka wa Baraza la Ardhi na Nyumba Sumbawanga na hawarejeshi kwa kiapo hati hizo kwa kiapo na baadae wananchi wanaoitika Barazani hutozwa asilimia 10% kama gharama za dalali ambazo huingia mifukoni mwao na tena wao kujilipa posho ya uendeshaji wa zoezi hilo kutoka ofisini.
Kabla hata shauri kusikilizawa barazani Fagio Auctioneer hupewa kazi hiyo ya kuwadai wananchi kodi husika pasipokuwa na sifa wala kufuata taratibu ambapo hukamata nyumba hizo na kuanza kuziuza kinyemela kitu ambacho baadae kitaiingiza serikali na wananchi kwenye mgogoro na hasara kwa tamaa zao.
Ofisi ya Kamishina Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Rukwa imekuwa ikilalamikiwa sana juu ya dhiruma na ubadhirifu hasa kwa kutengeneza migogoro ili kkujipatia fedha za rushwa chini ya kamishina huyo na Afisa Ardhi huyo Kabaghe ikiwemo kutoa hati mara mbilimbili na kudhurumu maeneo ya wananchi.
Haiingii akilini Mkuu wa Idara ya Ardhi Manispaa Sumbawanga kwanini anakumbatiwa na ofisi ya Kamishina msaidizi wa ardhi mkoa wa Rukwa na kukalia vyeo ofisi mbili wakati watu wengine wapo huo ni urasimu.
Tunaomba mkuu wa mkoa,msajili wa mbaraza ya ardhi na waziri wa ardhi muingilie kati hawa watu wanatubyanyasa na pia kujilipa pesa za serikali kinyume na utaratibu kwa maslahi yao pasipo kufuata sheria kanuni na taratibu.
Hatukatai kushitakiwa kwa kudaiwa lakini sheria,kanuni na taratibu zifuatwe kamishina ashitaki Barazani, wadaiwa tuletewe hati za wito kupitia msambaza nyaraka wa baraza,tufike barazani, shauri lisikilizwe na baraza pasipokuingiliwa na Kamishina msaidizi wa ardhi na mkuu wa idara ya ardhi manispaa ya sumbawanga, hikumu itolewe, kamishina/mdai akishinda mdaiwa apewe muda wa kutekeleza hukumu ai kukata rufaa na akishindwa ateuliwe dalali wa baraza wa mkoa wa Rukwa atekeleze hukumu siyo aletwe dalali bora dalali, apewe notisi ya siku 14 mshindwa tuzo kulipa deni
Mshindwa tuzo akishindwa kutekeleza hukumu baraza litowe amri ya kuuza nyumba,dalali mteuliwa atanfaze kuuza kwa siku 30 baada ya uthaminishaji, nyumba ikiuzwa dalali apeleke gharama zake baraza lizipie alipwe kwanza yeye na baadae kamishina ndipo alipwe, pesa ikibaki arejeshewe mshindwa tuzo,kinyume na hapo utekelezaji wote utakuwa batili na unaweza kupingwa mahakama za juu na mshindwa tuzo kushinda.
Sasa huyu Afisa Ardhi Kabaghe yeye ni nani au anauwezo gani kuwashinda wenzie aweze kufanya kazi na kutoa maamuzi ofisi zote za ardhi mkoani Rukwa?
Ni wakati sasa atafutiwe sehemu nyingine kwani amekuwa ni tatizo katika ofisi za ardhi hapa Sumbawanga mhasibu yeye,mtunza ofisi yeye,mwanasheria yeye,transport officer yeye,hr yeye,msaidizi wa kamishina yeye,n.k.