Manispaa ya ilala imetoa tangazo kuhusu ugawaji wa viwanja eneo la Kinyerezi. Katika tangazo hilo unatakiwa ulipe shilingi 20,000.00 kupitia benki ya DCB akaunti 011005000075. Manispaa wameamua kuchaji sqm 1 kwa shilingi 10,000.00 hadi 15,000.00. Swali la kujiuliza hivyo viwanja ambavyo viko 3000 watavigawaje wakati wananchi kwa maelfu wamefurika kwenye hiyo benki wakitaka kupatiwa viwanja? Kama watalipa watu 100,000 hivyo viwanja 3000 itakuwaje? Je pesa zitakazo kusanywa itakuwaje? Hii si DECI nyingine? Maswali ni mengi sana.