Mangula, Kinana Na Hatima ya Taifa Letu

Sikubaliani na hoja kuwa Kinana na Mungula wanaweza kuwa chanzo cha aina yoyote ile cha Mustakabali wa Taifa letu, Pili sikubaliani na hoja kuwa Mukama alishindwa kuisimamamia na kuiongoza CCM,


Tatizo kubwa la CCM ni Mwenyekiti wa Chama, Mwenyekiti anaonekana kushindwa kukiongoza Chama, kwa hiyo uwepo wa Kinana na Mangula hautaweza kubadilisha chochote kwenye Chama kama Mwenyekiti atashindwa kusimama kama Mwenyekiti wa kutekeleza ushauri atakao pewa na hao (Kinana na Mangula).

Lowassa, Membe, Mwakyembe, Sitta na watu wanaofanana na hao ndio tatizo kubwa la chama kwa sasa, na hao hawagusiki kwa sababu Mwenyekiti hana uwezo wa kuwafanya chochote, Nape alijaribu kupambana na Lowasa lakini matokeo yake kila mtu anayaona, na Mangula na Kinana pia hawataweza kufanya lolote kwani Mwenyekiti hataweza kufanya maamuzi magumu yatakayoshauriwa na Mangula na Kinana

Mwenyekiti wa Chama na familia yake, tayari wameshakigawa chama kwa kuonyesha wazi kuwa wanamsupport Membe, sasa hapa Kinana na Mangula watakuwa na kazi gani ya kukijenga na kukirekebisha chama ili hali mtu wa kugombea 2015 ana baraka za mwenyekiti wa chama? na Hili si jambo geni kwa Kinana na Mangula, kwani hata Mangula mwenyewe ni muasisi wa hayo Makundi. Mangula ni miongoni mwa watu waliompinga JK kwa nguvu zake zote, kwa Mangula Sumaye ilikuwa bora kuliko JK, na kila mtu anajua kilichompata Mangula baada ya JK kuingia ikulu, kwa sasa sidhani kama Mangula atakuwa na uwezo tena wa kupingana na mwenyekiti kuhusu nani agombee 2015. Na hapa ndipo Mukama alionekana kana kwamba ameshindwa, Mukama aliangushwa na udhaifu wa Mwenyekiti.

Mimi naweza kukubaliana na wewe kuwa nchi inaweza kuyumba kama CCM ikitoka kwenye madaraka kwa sababu ifuatayo ambayo haiusiani kabisa na Kinana wala Mangula

Wakuu wengi wa vyombo vya usalama wanaisimamia CCM kwa minajili ya kulinda maslahi yao binafsi, ushahidi ulidhihirika wakati wa uchaguzi uliopita ambako tulishuhudia wakuu wa Usalama, Police, Jeshi wakitoa kauli tata ambazo zilituonyesha CCM inasimamia wapi. Kauli ya mwenyekiti wa CCM pale dodoma (CCM wasitegemee police) Pia inaonyesha ni kwa jinsi gani CCM ilikuwa ikitegemea wakuu wa vyombo vya dola.
Kama CCM itashindwa Kihalali na hao niliowataja hapo juu wakishirikiana na TBC na Msajili wa Vyama pamoja na NEC wakijaribu kufanya hila yoyote kwa ajili ya maslahi yao basi nchi itayumba na hapo itakuwa sio Kinana wala Mangula
 
Kuhusu Azimio la Arusha napata shida nikuambie nini?Nashindwa kulipinga kwa vile tutakosa kipimo kingine ch akupimia waovu na hivyo nami nitakuwa irresponsible.Nashindwa lisuupoort sana kwa vile najua nalo ni tatizo.Nabaki nikionge kijujuu kama US wanavyojaribu tafuta namna watu waanzishe resistance toke andnai aili nao waweze tafuta suspport UN ili wapate uhalalai wa kusaidia.Kwani wakiingia hivihivi watamabia ni ubeberu na kuingilia mamabo ya ndani ya nchi nyingine.

Azimio la Arusha si great au absolute solution kama watu wanavyotaka jiaminisha kipindi hiki mambo yamekwama.Ila ndio komeo pekee tulilo nalo, na lazima tufunge lango letu.Ni kipindi sasa wasomi wetu wakajaribu litumia kwa tahadhari bila kuwapa waovu loopholes za kulikataa wanapotaka tukandamiza, na kulitumia wanapozidiwa na wanyonyaji wenzao Kma ilivyo sasa hivi.

Well said...
 
Kama Mangula na Kinana wakiiokoa CCM, hii itakuwa disaster kwa Tanzania. Kwa sasa ni muhimu sana CCM ife halafu izaliwe upya, ianze kwenda kwa baba na mama yake kuomba msamaha halafu iende tena mjini kutafuta kazi.

Mkulima na mfanyakazi ambaye ndio baba wa CCM sasa ametupwa kabisa, walau mtoto wa mfanyabiashara amejitokeza kujaribu kuwalea wazazi waliotelekezwa na mwanao. Kama CCM haiendi kuomba msamaha, laana itaendelea kuitafuna.

JF ina fikra pana sana.Sijui kwanini mwenyekiti waoa hataki wapati abaraka na kuwahakikihsia kuwa hawawezi kuwa corrupted na fikra za humu ndani.
 
Mchambuzi mada yako ni mwanzo mzuri wa kuweka mambo fulani wazi kati ya Reformists na Abolitionists wa CCM wakati huo conservatives wa CCM wakikosa pa kujishikia kwani kwao bado debate nyingine haijaisha.Kwao CCM si tatizo ila tatizo ni wana CCM waliopo, na wengine JK si tatizo ila tatizo ni watendaji.hapa Hata Jk mwenyewe kazama, kwani anaamini watendaji ndio shida,ndio maana yupo busy wabadili hovyo, yupo busy kuwapa seminar elekezi,bado mamabo hayaendi.Wale wanaothubutu kumpa live au kwa mafumbo kuwa yeye ndio tatatizo number moja.Huwaita wana chuki na vijiba na wanamuonea donge.As if urahisi ni riziki fulani personal.

Tatizo lingine ni kwamba CCM imekuwa traped ktk siasa za kimapinduzi na kijamaa ambazo hazina tena nafsi dunia ya leo.Ukiwauliza wana CCM wote wanaona kuwa uhuru wa habari ni hisani ya JK kwa wananchi, hawajui kuwa wananchi wanapaswa kuwa na anguvu kuliko serikali.Hawaaamini kuwa ukweli unaweza kuw anje ya CCM au ktk nchi zisizo zakijaaa.Hawaamini kuwa wananchi wanahitajia uhuru ktk nyanja nyingi sana,ikiwepo mavazi ,muziki, etc na hawahitaji serikali kuwaamulia hayo, hawajui kuwa maendeleo ya maeneo mablimablia nchi yanapaswa amuliwa na local authority kwa kushirikiana na watu wa eneo husika.Kwa vile vyote hivi si sehemu ya ujamaa.
 
Sikubaliani na hoja kuwa Kinana na Mungula wanaweza kuwa chanzo cha aina yoyote ile cha Mustakabali wa Taifa letu, Pili sikubaliani na hoja kuwa Mukama alishindwa kuisimamamia na kuiongoza CCM,


Tatizo kubwa la CCM ni Mwenyekiti wa Chama, Mwenyekiti anaonekana kushindwa kukiongoza Chama, kwa hiyo uwepo wa Kinana na Mangula hautaweza kubadilisha chochote kwenye Chama kama Mwenyekiti atashindwa kusimama kama Mwenyekiti wa kutekeleza ushauri atakao pewa na hao (Kinana na Mangula).

Lowassa, Membe, Mwakyembe, Sitta na watu wanaofanana na hao ndio tatizo kubwa la chama kwa sasa, na hao hawagusiki kwa sababu Mwenyekiti hana uwezo wa kuwafanya chochote, Nape alijaribu kupambana na Lowasa lakini matokeo yake kila mtu anayaona, na Mangula na Kinana pia hawataweza kufanya lolote kwani Mwenyekiti hataweza kufanya maamuzi magumu yatakayoshauriwa na Mangula na Kinana

Mwenyekiti wa Chama na familia yake, tayari wameshakigawa chama kwa kuonyesha wazi kuwa wanamsupport Membe, sasa hapa Kinana na Mangula watakuwa na kazi gani ya kukijenga na kukirekebisha chama ili hali mtu wa kugombea 2015 ana baraka za mwenyekiti wa chama? na Hili si jambo geni kwa Kinana na Mangula, kwani hata Mangula mwenyewe ni muasisi wa hayo Makundi. Mangula ni miongoni mwa watu waliompinga JK kwa nguvu zake zote, kwa Mangula Sumaye ilikuwa bora kuliko JK, na kila mtu anajua kilichompata Mangula baada ya JK kuingia ikulu, kwa sasa sidhani kama Mangula atakuwa na uwezo tena wa kupingana na mwenyekiti kuhusu nani agombee 2015. Na hapa ndipo Mukama alionekana kana kwamba ameshindwa, Mukama aliangushwa na udhaifu wa Mwenyekiti.

Mimi naweza kukubaliana na wewe kuwa nchi inaweza kuyumba kama CCM ikitoka kwenye madaraka kwa sababu ifuatayo ambayo haiusiani kabisa na Kinana wala Mangula

Wakuu wengi wa vyombo vya usalama wanaisimamia CCM kwa minajili ya kulinda maslahi yao binafsi, ushahidi ulidhihirika wakati wa uchaguzi uliopita ambako tulishuhudia wakuu wa Usalama, Police, Jeshi wakitoa kauli tata ambazo zilituonyesha CCM inasimamia wapi. Kauli ya mwenyekiti wa CCM pale dodoma (CCM wasitegemee police) Pia inaonyesha ni kwa jinsi gani CCM ilikuwa ikitegemea wakuu wa vyombo vya dola.
Kama CCM itashindwa Kihalali na hao niliowataja hapo juu wakishirikiana na TBC na Msajili wa Vyama pamoja na NEC wakijaribu kufanya hila yoyote kwa ajili ya maslahi yao basi nchi itayumba na hapo itakuwa sio Kinana wala Mangula

wanatafuta wa kumwachia lawama kama walivyoanza na kumlaumi Mkapa, kiasha waakendelea ongeza watu, sasa atarudi kwa hawa jamaa kuwa hawakumsadia.Akisahau kuw akipindi hichi unaweza fanya maovu kwa haraka na kiasi kikubwa within a ayear kuliko waliyowahi fanya marais wote kwa pamoja.

CCM ni very abusive party, wali abuse maana nzima ya haki za jinsia kwa ktk zoezi la kumchagua Spika, wakaja abuse tena kw akumchukua Mangula, walimpa jina baya Mkapa ila JK kamtumia sana kuzimisha hoja na movements nyingi ktk mikutano ya o ya kitaifa.Wamekuwa abusive sana ktk nafasi ya mwenyekiti, mwenyekiti ni kila kitu, mwenyekiti ndio ana define right and wrong ndani ya CCM.Na si kutumia right and wrong kama inavyofamika.
 
Mchambuzi big up!
yapo mambo matatu ya kujiuliza
  • kwa mkutano mkuu huu ccm imezaliwa upya au imezikwa kikamilifu kama chama alichokiasisi mwalimu Nyerere?
(hii itategemea na lengo la uteuzi wa kinana na mangula)
  • kwa mkutano huu mkuu ccm iko tayari kugawanyika kuwa vyama viwili kimoja kikisimamia maslahi ya kweli ya Taifa na kingine kikibaki kuwa hii ccm ya sasa?
(matokeo ya kura;KIKWETE 99%, KINANA 100%, MANGULA 100%!!!!!????)
  • kwa mkutano mkuu huu ushindi wa KIHALALI ccm 2015 ndicho kinachoandaliwa au kuruhusu DEMOKRASIA ITAMALAKI?
(jk anukuliwa akiwaambia wajumbe wasiwategemee tena POLISI) .
nimependa uchambuzi wako,tuendelee kusaidiana kuliandaa taifa kwa mabadiliko yajayo wakiwemo hata wenzako ndani ya ccm,
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,

Umenena vitu vingi vya msingi isipokuwa CCM ni sikio la kufa halisikii dawa. Viongozi wake kila kila siku wanatembelea sehemu mbalimbali za dunia lakini hawajifunzi. Kila siku watu wanasema madini na raslimali zetu zinaibiwa lakini wao wanachelewa na kupewa zaidi za kina Mangungo.

Mtaji wao mkubwa ni kuendelea kuamini kuwa Watanzania ni wajinga na hivyo hawatauliza haki na wajibu wa viongozi wasiowajibika kama wa CCM. Options hizo mbili zote ni mtihani. Njia mbili zilimshinda fisi. CCM ni janga la nchi hii na litaendelea kuwa janga mpaka litakapotolewa Magogoni.
 
CCM ni janga la nchi hii na litaendelea kuwa janga mpaka litakapotolewa Magogoni.

Ndio maana nazidi kuamini kwamba CCM kwa ndani imesha sambaratika na kugawanyika katika vyama vikuu zaidi ya viwili, kinachokosekana ni usajili tu wa vyama hivi, na pia ujasiri wa wahusika kwenda mbali zaidi na tofauti zao kwani kimtazamo na kimalengo, hawapo tena pamoja kama chama, kinachoendelea kuwaweka pamoja sana sana ni system;

Ni muhimu CCM ikasambaratika yenyewe sasahivi kuliko kusubiri kuja kusambaratishwa na upinzani (Chadema);
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom