Mangula, Kinana Na Hatima ya Taifa Letu

lakini ningependa kusikia zaidi upande wako wa hoja juu ya u-sumu wake katika mazingira ya sasa ya CCM na siasa za nchi kwa ujumla;


Sumu ni aina ya kitu cho chote kinachoathiri kwa kuthiri uhalisia wa sehemu au kuua kabisa. Kuna hatua na kiwango cha athari. Kuna kutibika, kuna kulemaa, kuna kupoteza maisha, hayo ni baadhi ya madhira tu.

Uhai wa CCM una misingi kwenye kuwatetea wafanyakazi na wakulima katika kuwaletea maendeleo, kuwapa fursa za kutoa maoni yao, kuchangia kitaifa katika mambo ya kijamii na maendeleo. KUWA NA UTAMBUZI WA KITAIFA kuwa. wana hisa wao na vizazi vyao. Kwa hayo yote hawa wakulima na wafanyakazi WALIKUWA WANAFAIDIKA NA RASILIMALI ZA TAIFA NA UVUJAJI JASHO WAO. Hii ilikuwa ndani ya Azimio la Arusha. Nalilinganisha na chakula cha nchi yangu Tanzania. Ulikuwa huwezi vimbiwa(sumu) katika kutekeleza azimio lile. Lakini kwa kiwango tulishuhudia kiwango cha juu kabisa cha UTAIFA na uchumi wenye mwelekeo acha mshikamano wa watu.

Awamu ya pili kwa makusudi ilianzisha Azimio la Zanzibar, haikusema imeua Azimio la Arusha; wala haikuwashirikisha wananchi kuhusu azimio hilo. Ni azimio la watu fulani. Azimio hili liliunda CCM ya sasa yenye maana ya Chama Cha Waporaji. Hii ilifanikiwa sana kutenganisha kwa kutotengamana kwa watawala na watawaliwa, wenye maamuzi ya mustakabali wa nani anastahili na rasilimali za nchi na nani hastahili; wenye kuweka tabaka la nani ana stahili zipi za kijamii zinazotokana na mavuno ya nchi na nani hawatahili nini. Haya yote yakitokea kumekuwa na usimamizi mbovu katika utekelezaji kwa kila upande. Kwa msingi huo, KUMEZALISHA SUMU inayotafuna FIKRA. FIKRA YA WATANZANIA kwa sasa HAITENGAMANI. Ukitumia lugha rahisi TUMESONGWA NA MAWAZO KWA KUPOTEZA MWELEKEO WA TAIFA. Mawazo yetu kwa sasa NI KILA MTU NA LWAKE, mwenye kupata apate, mwenye kukosa akose. Kibaya, wote tumejaliwa macho, masikio, hisia, fahamu na ladha. Kwa usawa wa kibanadamu inauma kuyashuhudia haya. Kwa hiyo sumu ya usongo inaongezeka siku hadi siku.

Awamu ya tatu ilitekeleza kwa vitendo Azimio la Zanzibar kubinafsisha hata fikra za watu ili zidumu fikra za watawala kwa nguvu ya dola. USHIRIKISHWAJI KATIKA MAAMUZI ULIPIGILIWA MSUMARI WA MWISHO. Nakukumbusha tu kuwa Mkapa alisifiwa sana na Taasisi za kimataifa, ni kwa sababu alikabidhi fikra, rasilimali na nchi kwa mabingwa wa kunufaika na upepari.

Awamu ya nne hii tunajua walivyoingia madarakani; kama njia sahihi zingetumika hakungekuwa na awamu ya JK. Tuseme awamu ya nne ni FURSA ILIYOPOTEA katika historia ya Tanzania. Mfano mdogo tu wameshiriki kuhujumu uchumi kupitia mambo mawili. 1. Kujiingiza kwenye biashara kwa kutumia madaraka na hususan kuwanufaisha wageni. 2. Uendeshaji mbovu wa nchi (Management) amabao hatujawahi kuushuhudia. Kwenye hali hii hata ukiwekewa sumu (kwa maana ya maamuzi maovu) utameza. Kama kufa ganzi ni awamu hii. Hapa ndipo nina maana ya kuwa mazuri yaliyoasisiwa kwa manufaa yetu sote KWAO NI SUMU hawawezi kunywa iwauwe.

Tukirudi upande mwingine wa wanaonufaika na hali hii. Mawazo yao na mwenendo wao ni kuwa WAMEFANIKIWA na wanashangaa kwa nini wengine wanalalamika (Ni wavivu wa kufikiri kwa kauli ya MKapa). Ni sawa kumuwekea sumu panya kuondoa udhia. Kwa matendo yote haya tamu ya mambo yalivyo kwa watawala CCM hawawezi kuona kwa macho, kusikia kwa masikio, kuhisi, kufahamu na kuonja adha za wananchi na wafanyakazi. Kwao wamejitenga na tabu hizo. Baadhi yetu na sisi tunajitahidi au kujikomba tujiunge nao au tushirikiane nao hata kwa makombo (rushwa). Sumu hii inatafuna uhai wa taifa. Taifa ambalo CCM si sehemu yao kwa hiyo hawako tayari kula sumu ili kurudisha nchi kwenye mwelekeo wa kitaifa wenye uadilifu, bidii na kuona matumani miaka 50 ijayo. Kwa sasa hii ni awamu yao.

Swali lako ni kifanyike nini? Kuna kanuni ya maumbile nadhani ni ya Mungu mwenyewe MBEGU LAZIMA IZIKWE IFE, ILI ICHIPUE. CCM lazima ife izikwe ili ichipue. Haiwezi kujiua kwa sababu hakuna aliyerudi kueleza kuna nini baada ya kufa. Lakini, ni kweli kinachofanywa na CCM kinavyoonekana na waadhirika wa matendo yao Wafanyakazi na Wakulima kamwe machoni pao hawakitanabahi. Sasa mtu aliyepoteza fahamu kiasi hicho atapewa dawa na nani? Dawa yo yote kwake sumu si Mangula, Kinana au JK.

Mustakabali wa taifa ni kweli unahitaji Leadership siyo Leader. CCM ni mabingwa wa viongozi ambao hawana leadership kwa maana wana tunu za kukubalika na waongozwa. "Leadership is a sum of ideals, comprehension and common direction by a community" Uongozi unajumuisha maadili, mtazamo, na mwelekeo wa pamoja wa jumuia(Taifa). CCM wanalo hilo? Wao wanataja fulani, fulani bila kuangalia jumuia ina mwelekeo upi.

Kurudi kwenye uadilifu, tafakuri, na mwelekeo wa pamoja wa kitaifa ni SUMU litaua matabaka yaliyoundwa.
 
Kama Mangula na Kinana wakiiokoa CCM, hii itakuwa disaster kwa Tanzania. Kwa sasa ni muhimu sana CCM ife halafu izaliwe upya, ianze kwenda kwa baba na mama yake kuomba msamaha halafu iende tena mjini kutafuta kazi.

Mkulima na mfanyakazi ambaye ndio baba wa CCM sasa ametupwa kabisa, walau mtoto wa mfanyabiashara amejitokeza kujaribu kuwalea wazazi waliotelekezwa na mwanao. Kama CCM haiendi kuomba msamaha, laana itaendelea kuitafuna.

Huu ni ukweli ingawa mchungu; Njia sahihi ya CCM kujirudi ni kukaa pembeni kwa muda kwani ikitokea hivyo, wachumia tumbo wengi pia wataondoka na watabakia wachache wenye mapenzi ya dhati na CCM, hivyo kuwa na nafasi nzuri ya kujipanga; kwa sasa wengi waliopo mle ni kwa ajili ya madaraka tu na ndio wanaokivuruga chama;
 
Unahoja nzuri lakini tatizo lake unataka CCM iendelee kukaa madarakani!!!
Sisi tumechoka na CCM tunataka itoke madarakani!!!

Pengine mawazo haya yatafaa kwa CCM wakiwa upinzani ili wayatumie kurudi madarakani!!

Ni kweli, mambo mengi nayozungumzia yanaweza kutumiwa hata na wapinzani; Nilichozungumza kililenga zaidi kuwaletea wananchi mabadiliko ya kweli, sio upuuzi wa ilani za uchaguzi ambazo hizo zinawapa huduma za msingi waone jua la kesho; Isitoshe, Mwalimu Nyerere alisema miaka ya tisini kwamba - "Wananchi Wanataka Mabadiliko, na Wasipoyapata Kupitia CCM, Watayatafuta Kupitia Chama Kingine" - Na kwa sasa inaonekana Chama Kingine Cha Kutafuta Mabadiliko Kinazidi kuwa Chadema, kwahiyo ni sahihi kabisa hata wao wakichukua mawazo yangu kwani yanalenga kujenga Taifa;
 
Mchambuzi.
Kuanzia kwenye Heading tu, ni nini kinakufanya uweke au ukose matumaini ya muenendo wa ccm kwa kuangalia watu hawa wadogo tu kwenye chama? chama hakina mwenyekiti? si ndie anayepaswa kuonyesha njia? sio issue ya kinana na mangula, bali ukweli ni kwamba makamu mwenyekiti yeyote yule na katibu wa chama yeyote yule hawawezi kumlazimisha mwenyekiti yeyote yule kufanya kitu chochote kile.
 
Leo ndio nimejua na mimi naipenda CCM, nilipofika hapo mahala umeelezea UNIP kupoteza kiti chake cha mwisho bungeni, mwili umenisisimka kwa kukiona kifo cha CCM mpaka machozi yamenitiririka, ila sina njia nyingine, sina budi kuliacha titi la mama.
 
Mchambuzi.
Kuanzia kwenye Heading tu, ni nini kinakufanya uweke au ukose matumaini ya muenendo wa ccm kwa kuangalia watu hawa wadogo tu kwenye chama? chama hakina mwenyekiti? si ndie anayepaswa kuonyesha njia? sio issue ya kinana na mangula, bali ukweli ni kwamba makamu mwenyekiti yeyote yule na katibu wa chama yeyote yule hawawezi kumlazimisha mwenyekiti yeyote yule kufanya kitu chochote kile.
Sangarara,
Nimejenga hoja kujibu maswali kama haya, na wapo baadhi ya watu wameuliza swali kama lako lakini waliporudi kusoma kwa umakini zaidi wakaelewa msingi wa hoja yangu ni nini; Vile vile wapo waliosoma na kunielewa na kuingia moja kwa moja katika mjadala wa kwanini uamuzi wa CCM baada ya 2015 aidha utaokoa au utaangamiza taifa letu; Ni katika muktadha huu ndio nimewajadili hawa wawili kwa hoja;
 
Leo ndio nimejua na mimi naipenda CCM, nilipofika hapo mahala umeelezea UNIP kupoteza kiti chake cha mwisho bungeni, mwili umenisisimka kwa kukiona kifo cha CCM mpaka machozi yamenitiririka, ila sina njia nyingine, sina budi kuliacha titi la mama.

Ni kweli, na haupo peke yake, tupo wengi, CCM sio Mama Yetu, tunaweza achana nayo wakati wowote; Hata Nyerere alitamka haya; Kinachosubiriwa ni wakati muafaka, hasa iwapo matumaini ya mabadiliko yatakuwa less than 25%;
 
Tukubaliane jambo moja: CCM inaumwa gonjwa ambalo halina tiba. Dawa za kurefusha maisha ya CCM bado zipo. Kila aliposhauriwa kuzitumia dawa hizi, Mwenyekiti Kikwete amekuwa akizitumia. Tumeona mabadiliko kadhaa kwenye Cabinet yake serikalini. Tumeona pia mabadiliko kwenye secretariet ya CCM. Mwenyekiti Kikwete ameweka rekodi ya kuwa na Makatibu wakuu watatu wa CCM, Makamba, Mukama na sasa Kinana ndani ya miaka hii sita ya Uenyekiti wake!

Tukumbuke pia jambo moja muhimu: Kikwete huyuhuyu alikuwa tayari kuiua CCM endapo ingemnyima kugombea URAIS wa JMT mwaka 2005! Sasa itafia mikononi mwake pamoja na tambo zake zote. Pamoja na akili nyingi alizonazo mtu kama Mangula amekubali kurudi kumsaidia mtu waliehitilafiana pakubwa kuimalizia CCM. Mangula naye amekubali kuwa dawa ya kurefusha maisha ya CCM. Historia itakuja kuliweka wazi hili.
 
Tukubaliane jambo moja: CCM inaumwa gonjwa ambalo halina tiba. Dawa za kurefusha maisha ya CCM bado zipo. Kila aliposhauriwa kuzitumia dawa hizi, Mwenyekiti Kikwete amekuwa akizitumia. Tumeona mabadiliko kadhaa kwenye Cabinet yake serikalini. Tumeona pia mabadiliko kwenye secretariet ya CCM. Mwenyekiti Kikwete ameweka rekodi ya kuwa na Makatibu wakuu watatu wa CCM, Makamba, Mukama na sasa Kinana ndani ya miaka hii sita ya Uenyekiti wake!

Tukumbuke pia jambo moja muhimu: Kikwete huyuhuyu alikuwa tayari kuiua CCM endapo ingemnyima kugombea URAIS wa JMT mwaka 2005! Sasa itafia mikononi mwake pamoja na tambo zake zote. Pamoja na akili nyingi alizonazo mtu kama Mangula amekubali kurudi kumsaidia mtu waliehitilafiana pakubwa kuimalizia CCM. Mangula naye amekubali kuwa dawa ya kurefusha maisha ya CCM. Historia itakuja kuliweka wazi hili.

Ukweli ni kwamba miti yote sasa inateleza
 
Sangarara,
Nimejenga hoja kujibu maswali kama haya, na wapo baadhi ya watu wameuliza swali kama lako lakini waliporudi kusoma kwa umakini zaidi wakaelewa msingi wa hoja yangu ni nini; Vile vile wapo waliosoma na kunielewa na kuingia moja kwa moja katika mjadala wa kwanini uamuzi wa CCM baada ya 2015 aidha utaokoa au utaangamiza taifa letu; Ni katika muktadha huu ndio nimewajadili hawa wawili kwa hoja;

Mchambuzi
Hii mambo ya Jakaya kubadirisha watu kila siku sijui ni nani kamuambia ndio jibu, mambo yalianza kuharibika pale azimio la arusha lilipowekwa pembeni, hapo ndio milango ilifunguliwa na uchafu wa kila aina kuingia kila mahala ndani ya nyumba, badala ya ccm kufanya structural change imekuwa kama kipofu, blindly inabadirisha viongozi kila kukicha, tena this time anasema kapewa ushauri na mkapa, the same person aliyechukua nchi blindly akaanza kutekeleza sera za soko huria.

Watanzania ni watu humble na very patient, mbona kipindi cha nyerere tunaambiwa nchi iliwahi kupitia kipindi kigumu sana kichumi na hakukuwa na kelele za kuichukia serikali wala ccm, nini kimetutokea sasa? badala ya ccm kuangalia namna ya kutuweka sawa inaendelea kutubadirishia watu, hawa watu sio watakaobadirisha hali ya maisha yetu japo kwa taratibu, we need structural changes kwenye uchumi wetu, vyombo vya ulinzi,usalama na sheria, huduma za afya, elimu na zaidi rushwa, Ama sivyo muda si mrefu na yeye ataamini kwamba yeye ndio tatizo kubwa zaidi.
 
Mimibaba,

Kwenye bandiko lako namba ‘62' una hoja za msingi na muhimu sana; Nitazijadili kwa ufupi;


  • I agree & understand u-sumu unaouongelea when it comes to CCM kurejea kwenye Azimio La Arusha; Lakini nadhani una maanisha zaidi kwamba tatizo sio kwamba hakuna mambo mazuri mle kutumika katika mazingira ya sasa, bali tatizo ni viongozi, hasa LACK OF POLITICAL WILL;


  • I agree kwamba Mangula na Kinana sio Mwarobaini; Lakini wana nafasi japo kidogo ya kurudisha matumaini kwa wananchi au to set the trend ili wengine huko mbele waje kujenga kwenye misingi waliyoweka; Misingi ipi? Ni pamoja na niliyoshauri; Je wataweza? I doubt it, na ndio tunarudi kwenye hoja yako kwamba pengine lazima CCM ife kwanza, na binafsi ningependa sana Mangula na Kinana waiue aidha kwa kuigawanya au kushawishi CCM kukubali matokeo iwapo CCM itaanguka 2015 na kuanza upya;


  • Kama nilivyoanza kujadili hapo juu, I Agree kwamba ili CCM iwe imara zaidi, ni lazima itoke madarakani na kujipanga upya – sio ife; Njia sahihi zaidi kwa mtazamo wangu ni aidha kumeguka sasa au kubakia hivyo hivyo na kuanguka 2015 ili tuone sasa nani atabakia, nani ataondoka, kwani imekuwa ni vigumu kuondokana na wanao kiharibu chama, lakini kikitoka madarakani, wchumia tumbo wote watakimbilia kwingine, hivyo kukiacha chama na watu wachache wenye mapenzi ya dhati na chama chao na taifa kwa ujumla; Vinginevyo kusema CCM Lazima ife, haitawezekana kutokana na ukweli kwamba CCM ina mizizi mirefu sana, hili lingewezekana tu miaka ile ile ya mwanzo ya mageuzi ya kisiasa nchini; Isitoshe, CCM ikifa, Chadema bila ushindani itafanya kazi vizuri kweli? Au una amini kwamba vitaibuka vyama vingine kupambana nayo? Sina imani sana na vyama vingine vya upinzani vya sasa kama NCCR, au vingine ambavyo vitasimamia masuala ya TANGANYIKA kwanza, TANZANIA baadae;


  • I Agree juu ya lack of leadership quality ndani ya CCM; CCM hatuna Viongozi au at least hatuonyeshi Uongozi, tulichonacho ni Siasa/Wanasiasa, na kuna utofauti kati ya haya mawili:

1. Kiongozi anajali watu/wananchi anaowatumikia; Mwanasiasa anajali chama chake, nafsi yake, familia yake, lakini muhimu zaidi viongozi wake wakuu, hasa waliomteua kushika wadhifa husika. Mara nyingi tumeona jinsi gani wanasiasa wa CCM wamekuwa na unconditional obedience kwa wakubwa waliowateua. Hili linachangia sana matatizo ambayo Lowassa aliyazungumzia katika hoja yake juu ya matatizo ya uongozi ndani ya CCM- lakini nisingependa kumjadili Lowassa hapa).

2. Kiongozi ni mtu ambae hufanya maamuzi yanayolenga maslahi ya taifa au jamii inayomzunguka; Mwanasiasa hufanya maamuzi yanayokilinda chama chake, lakini hasa kuwaimarisha wanasiasa au makundi yaliyomfadhili/yaliyompa nafasi yake ya uongozi.

3. Kiongozi uhimiza matumizi ya fedha za walipa kodi kwa ajili ya miradi ya muda mrefu na yenye manufaa kwa jamii/maslahi ya taifa; Mwanasiasa uangalia zaidi miradi ambayo aidha inamnufaisha yeye binafsi katika kipindi chake cha madaraka au pamoja na wote waliomfadhili wadhifa husika;

4. Kiongozi hufukuza kazi watumishi wa umma wasiofaa; Mwanasiasa huwajenga na huwakinga kila wanapofanya maovu;

5. Kiongozi hujifunza kutokana na makosa; Mwanasiasa hakubali makosa, badala yake hujiona yupo sahihi wakati wote;

6. Kiongozi hufanya kazi vyema na wenzake bila ya kujali itikadi za vyama ili mradi ni kwa manufaa ya umma/maslahi ya taifa; Mwanasiasa mara nyingi huwa ni mnafiki, mfitini na mwoga. Mara nyingi, mwanasiasa hutumikia waliomteua au mfadhili wadhifa wake na hivyo huwa anaishi na kufanya kazi katika mazingira yaliyojaa hofu ya kuvuliwa wadhifa alionao, aidha na chama chake au wakubwa zake.

7. Kiongozi wakati wote husema ukweli; kwa Mwanasiasa, ni desturi kuwa muongo na mara nyingi huwekeza zaidi katika kugeuza uongo kuwa ukweli;

8. Na mwisho, katika usimamizi wa fedha za walipa kodi na rasilimali za umma, Kiongozi hujali kubana matumizi yasio ya lazima, na uhimiza matumizi yenye kulenga kuendeleza taifa na watu wake; Mwanasiasa mara nyingi hujikitika zaidi kuhakikisha fedha za walipa kodi na rasilimali za umma zinamnufaisha yeye na familia yake pamoja na wale waliompa fadhili ya uongozi.
 
Tukubaliane jambo moja: CCM inaumwa gonjwa ambalo halina tiba. Dawa za kurefusha maisha ya CCM bado zipo. Kila aliposhauriwa kuzitumia dawa hizi, Mwenyekiti Kikwete amekuwa akizitumia. Tumeona mabadiliko kadhaa kwenye Cabinet yake serikalini. Tumeona pia mabadiliko kwenye secretariet ya CCM. Mwenyekiti Kikwete ameweka rekodi ya kuwa na Makatibu wakuu watatu wa CCM, Makamba, Mukama na sasa Kinana ndani ya miaka hii sita ya Uenyekiti wake!

Tukumbuke pia jambo moja muhimu: Kikwete huyuhuyu alikuwa tayari kuiua CCM endapo ingemnyima kugombea URAIS wa JMT mwaka 2005! Sasa itafia mikononi mwake pamoja na tambo zake zote. Pamoja na akili nyingi alizonazo mtu kama Mangula amekubali kurudi kumsaidia mtu waliehitilafiana pakubwa kuimalizia CCM. Mangula naye amekubali kuwa dawa ya kurefusha maisha ya CCM. Historia itakuja kuliweka wazi hili.

Na ndio maana nimekuwa nasema kwamba kilichotokea ni mabadiliko ya Kichwa (na sio chote), huku shingo ikibakia kuwa ni ile ile; Na tunajua kwamba Shingo ndio hugeuza kichwa kulia kushoto, ku-nod ndio, hapana, yote haya ni kazi ya shingo na misuli yake na sio kichwa per se;
 
Hivi mabadiliko yanaweza kuletwa na watu wawili tu, tena wastaafu na wachafu katika chama kichafu, mfumo mchafu na wanachama wachafu?

na Kinana tayari ameanza wizi wa meno ya tembo..maandalizi ya kuhonga wapiga kura na siyo utendaji
 
Na ndio maana nimekuwa nasema kwamba kilichotokea ni mabadiliko ya Kichwa (na sio chote), huku shingo ikibakia kuwa ni ile ile; Na tunajua kwamba Shingo ndio hugeuza kichwa kulia kushoto, ku-nod ndio, hapana, yote haya ni kazi ya shingo na misuli yake na sio kichwa per se;
Nikuulize jambo moja Mchambuzi: Kwa nini bado watu na akili zao timamu kabisa wanabanana kugombea nafasi za UONGOZI ndani ya CCM inayokufa kwa kasi hivi? Au hili linafanana na masuala ya ngono na ukimwi( nisamehe kwa lugha hii ya kuudhi)?
 
Sangarara, in regards to post yako namba 71:

Kinachofanyika kinafanana na kisa kimoja kilichotokea Kenya miaka ya tisini; ambapo raia mmoja wa ulaya aliekuwa anaishi Kenya kikazi alifiwa na mke wake; Badala ya kumzika, akaamua kumweka kwenye freezer kwani hakukubaliana kabisa hali ya kuondokewa na mkewe; Yani Mke aondoke hivi hivi tu? Hell No!; Baada ya kuanza kumtunza kwenye freezer, akawa anaenda kuchukua Malaya usiku kwenye ma-bar, na kuwaleta nyumbani kwake na kuwalipa hela nyingi sana wakidhania wanaenda kulala nae, kumbe wanaenda kumsafishia maiti ya mkewe kwa kuitoa kweney freezer na kuiosha, kuipaka makeup zile zile alizokuwa nazo wakati wa uhai wake, kumbadilisha nguo mara kwa mara, zile zile za kwenye kabati wakati wa uhai wake, kisha wanamlaza kwenye kochi, na mzee yule anawasha mziki mtamu tamu, na anaaza kunywa whisky zake huku akiongea na mkewe kama vile yupo hai, huku Malaya wale wakishuhudia kwa woga; baada ya masaa kadhaa, anawaambia malaay wale wamrudishe kwenye freezer; Ilifikia hatua ikabidi Malaya wale waende kutoa ripoti polisi, na huo ndio ukawa mwisho wa yule mzee kuishi Kenya kwani aliondolewa nchini mle ndani ya masaa 24;
 
Nikuulize jambo moja Mchambuzi: Kwa nini bado watu na akili zao timamu kabisa wanabanana kugombea nafasi za UONGOZI ndani ya CCM inayokufa kwa kasi hivi? Au hili linafanana na masuala ya ngono na ukimwi( nisamehe kwa lugha hii ya kuudhi)?

Wildcard,

Lugha yako sidhani kama ni ya kuudhi, badala yake ni ya kuudhika na kuna sababu za msingi; Jibu langu ambalo pengine linaweza kua finyu ni hili:

Kuna personal investments in reciprocal relations ambazo watu hawa hufanya na viongozi wa CCM na serikali yake, kama njia ya kufanikisha malengo yao binafsi ambayo ni dhahiri hayawezi kufanikiwa nje ya CCM; Hii ni tofauti na kufanikisha malengo ya UMMA ambayo ni dhahiri yanaweza kufanikiwa kupitia Chadema na vyama vingine;

Sought Goods (bidhaa wanazotafuta) hawa watu hazina uhusiano na PUBLIC GAIN bali PRIVATE GAIN; Bidhaa hizi ‘ADIMU' ni pamoja na Prestige, Social Status & Wealth, ambazo kwa kweli zote hizi have a 'Scarcity Value' - kwa maana ya kwamba – they may be available, but they may not be accessible to many; Kutokana na hili, wengi ya hawa watu hutumia kila njia to invest in relations na CCM, viongozi wake na Serikali Yake kama njia rahisi ya kupata bidhaa hizi adimu;

Huu ndio mtazamo wangu, hasa juu ya swali lako;
 
NImependa ulivyowashauri wafanya kazi kumshauri mgombea wa CCM, na JK atakayemwachia lazim ajiandae kukubali "will of people".Hapa ndipo hata wachangiaji wa CCM humu hawawezi amini kama wale watu wasioamini kuwa ipo siku mwanamume atahitaji kupeleka mtoto wake clinic na ikawezekana.Na wengi sana wapo kwa vile kiasi walichoweza CCM in terms time, money, lifestyle etc na hata muwaandaa watoto wao waje pand angazi za CCM haiwaaingii akilini kusikia kuwa CDM wanaweza ichukua hii haraka zaidi ya wafikiriavyo.

Pengine kukurekebisha kidogo ni pale ukipoonyesha kuwa wapiga kura watakaokuwa wengi ni vijana kweli,ila uli attribute to umasikini and the sort.Hukupenda tazama vinana proffessionals wanaojisikia raha kuwa CDM, wanao enjoy ujinga wa magamba kila kukicha na jinsi CDM wanavyo wa diagnosis .Hawa wanapenda CDM kama trend ya kisasa, wanapenda CDM kama chama kinye watu wa kawaida katk uongozi na hivyo kuwafanya vijana professional waweze wasiliana nao, na kufurahi kama vijana bila master- slave relationship. CDM wana vitu vingi rahisi sana vinavyovutia professionals, waktai huo huo CCM hawawezi provide food for the souls and minds.
 
Tukubaliane jambo moja: CCM inaumwa gonjwa ambalo halina tiba. Dawa za kurefusha maisha ya CCM bado zipo. Kila aliposhauriwa kuzitumia dawa hizi, Mwenyekiti Kikwete amekuwa akizitumia. Tumeona mabadiliko kadhaa kwenye Cabinet yake serikalini. Tumeona pia mabadiliko kwenye secretariet ya CCM. Mwenyekiti Kikwete ameweka rekodi ya kuwa na Makatibu wakuu watatu wa CCM, Makamba, Mukama na sasa Kinana ndani ya miaka hii sita ya Uenyekiti wake!

Tukumbuke pia jambo moja muhimu: Kikwete huyuhuyu alikuwa tayari kuiua CCM endapo ingemnyima kugombea URAIS wa JMT mwaka 2005! Sasa itafia mikononi mwake pamoja na tambo zake zote. Pamoja na akili nyingi alizonazo mtu kama Mangula amekubali kurudi kumsaidia mtu waliehitilafiana pakubwa kuimalizia CCM. Mangula naye amekubali kuwa dawa ya kurefusha maisha ya CCM. Historia itakuja kuliweka wazi hili.

well said.
 
Mchambuzi
Hii mambo ya Jakaya kubadirisha watu kila siku sijui ni nani kamuambia ndio jibu, mambo yalianza kuharibika pale azimio la arusha lilipowekwa pembeni, hapo ndio milango ilifunguliwa na uchafu wa kila aina kuingia kila mahala ndani ya nyumba, badala ya ccm kufanya structural change imekuwa kama kipofu, blindly inabadirisha viongozi kila kukicha, tena this time anasema kapewa ushauri na mkapa, the same person aliyechukua nchi blindly akaanza kutekeleza sera za soko huria.
kabadili kila kitu ila dunia yake haiendi vyema,sasa wote wabeadilishwa na mambo hayaendi ni wazi kuwa sasa yeye ndio tatizo.


Kuhusu Azimio la Arusha napata shida nikuambie nini?Nashindwa kulipinga kwa vile tutakosa kipimo kingine ch akupimia waovu na hivyo nami nitakuwa irresponsible.Nashindwa lisuupoort sana kwa vile najua nalo ni tatizo.Nabaki nikionge kijujuu kama US wanavyojaribu tafuta namna watu waanzishe resistance tokea ndani ili nao waweze tafuta suspport UN na wapate uhalali wa kusaidia.Kwani wakiingia hivi hivi watamabia ni ubeberu na kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine.

Azimio la Arusha si great au absolute solution kama watu wanavyotaka jiaminisha kipindi hiki mambo yamekwama.Ila ndio komeo pekee tulilo nalo, na lazima tufunge lango letu.Ni kipindi sasa wasomi wetu wakajaribu litumia kwa tahadhari bila kuwapa waovu loopholes za kulikataa wanapotaka tukandamiza, na kulitumia wanapozidiwa na wanyonyaji wenzao Kma ilivyo sasa hivi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom