Mi sijui ugomvi ni CUF, CDM na NCCR kutoka nje ya bunge ndo kinaleta gumzo au hofu ya kuwa huenda kweli wakaungana! Vinginevyo wanaolalamika na kutukanana humu wote si wasemaji wa vyama vyao. Duni sidhani kama ni sahihi kuwaza kuwa serikali ya chama fulani ikiwa madarakani basi na ofisi za serikali ni za chama hicho ... maana unataka kutuambia tukienda kutibiwa hospitali ya serikali tunatibiwa na CCM kwa vile ndo iko madarakani, mtaalam wa kilimo akija kutibu mazao yangu ni CCM imefanya naona ni hoja dhaifu kwa mtizamo wa maana ya serikali na vyanzo vya serikali vya kutoa huduma ... vinginevyo kila serikali ikiingia madarakani basi itafute kodi toka kwa wanachama wake ili itoze kodi na hapa ndipo udhaifu wa hoja yako ulipo zaidi achilia mbali kutumia maneno ya matusi mtu mkubwa namna hiyo...tuanze kuona aibu kwa mambo yanayotia aibu hata tukiwa wanasiasa.