Intelligentsia: Lipumba ni mtu wa system. Wakati anajiondoa uenyekiti mwaka jana, system ilihitaji hivyo. Lengo linafahamika. Prof. Lipumba alijitahidisana kuvuruga UKAWA kuanzia January hadi Julai (2015), na alikuwa amefanikiwa ila kukatokea tukio la kisiasa lisilotegemewa - Lowasa kujiunga CHADEMA. Mipango ya awali yote ikabidi ibadilike.
Kutumika akiwa ndani ikashindikana. Mkakati wa muda mfupi ukabuniwa. Kwamba atoke kuona iwapo ingesaidia kuleta haueni kwa CCM. Sina uhakika iwapo alifanikiwa au la.
Lakini sasa system inamwitaji tena. Anatakiwa kutatua tatizo la Zanziar. Kwa mkakati wa muda mfupi, Jecha aliweza kufanikisha. Mkakati wa muda mrefu umeshindikana kupata fixer. Lipumba anatakiwa, akiwa ndani, siyo nje ya CUF, kuokoa jahazi la Zanzibar. Mapalala, Nyaruba, Awesi Dadi na wengineo (Enzi za Komandoo Amour) waliweza kufanya hivyo wakiwa nje ya CUF lakini hawakufanikiwa sana. Sasa anatakiwa key brain ku-run system ya utawala Zanzibar.
Kwa kuanzia Prof. Lipumba ana assignment ya kuhakikisha analeta vurugu katika uongozi wa CUF. Atatengenezewa wafuasi na washabiki wanaotaka arudi. Unaweza kushangaa ilikuwaje hao washabiki na wafuasi wake famfe walishindwaje kumzuia asiondoke CUF wakati alitakiwa awepo kuhakikisha chama hakiyumbi! Wakati wa Kampeini kuelekea uchaguzi 2015.
Mgogoro wa uongozi unaweza kusogeza mbele, siku kadhaa hata mwaka, kwa utawala wa Zanzibar kuishi kwa muda huo wakati CUF wanaumana wao kwa wao. Ni mkakati ule ule uliotumika enzi za akina Marando na kundi lake vs. Augustino Mrema (NCCR-Mageuzi: 1996-67). Makundi yote (NCCR-Mageuzi) yalishindwa. Mkapa na CCM waliweza kupeta uchaguzi Mkuu mwaka 2000.
Na ikitokea Prof. Lipumba akafanikiwa kuwa Mwenyekiti wa CUF, hatua itakayofuata ni kuendeleza mgogoro baina yake (wafuasi wake) na Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad. Kwa hiyo tutakuwa tunaendelea kusikia habari za kamati Kuu ya CUF (Lipumba) imemfukuza uanachama Maalim Seif S. H, au Kamati Kuu ya CUF (Seif S. H) yamvua Madaraka na kunfukuza uanachama Prof. Lipumba.
Hali itaendelea hivyo hadi 2020. Kila mtu atakuwa amechoka, lakini si haba kwa Prof. Lipumba. Lakini pia tutarajie kauli za Mwenyekiti Prof. Lipumba kukubaliana na matokeo ya uchaguzi Zanzibar 2015 hivyo kuunga mkono Serikali ya Dr. Sheini. Msisahau kuwa kila statement huwa inalipiwa, si haba.
Huu si utabiri, ni intelligentsia.
Tusubiri.