Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Martial muingereza, de gea muingereza, fred pia muingereza, Perreira na mata waingereza, lindelof muingereza, matic pia muingereza,
 
Ole ni Mnorway

DeGea,Lindelof,Fred,Martial,Matic,Pogba,Perreira..hawa vipi??

Mbona Liverpool wana Trent,Robertson(UK),Henderson,Milner,Chamberlaine,Lallana??
 
Bruno Fernandez in, Marcos Llerente in?

Wakati dili la Bruno Fernandez likiwa ni suala la lini na si suala la kama atakuja United, kiungo mkabaji wa Atletico Madrid Marcos Lloriente anatajwa kufukuziwa na Manchester United na hii kwa kiasi kikubwa imechangiwa na kuuumia kwa Pogba na Mc Tominay

Marcos Lloriente ni nani?

Ni kiungo mkabaji aliyefuzu mafunzo ya soka pale Real Madrid, alisajiliwa kwenda Atletico Madrid kuziba nafasi iliyoachwa na Rodri aliyetimkia timu Manchester City.

Mchezaji huyu ambaye babu na baba yake walicheza Real Madrid na Atletico Madrid (kama yeye) anadaiwa kuhitajiwa Man Utd kwa mkopo

Hata hivyo mashabiki wa United hawatakiwi kuufurahia sana ujio wa kijana huyo wa miaka 24 kwani hata Atletico Madrid ameshindwa kupata namba na kimachaguo amekuwa nyuma ya Partey, Niguez na Herrera

Baadhi ya wadau wanadai huu ni mwendelezo wa bodi ya United kutaka cheap badala ya quality

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Martial muingereza, de gea muingereza, fred pia muingereza, Perreira na mata waingereza, lindelof muingereza, matic pia muingereza,
Nakuhakikishia walivyo wanafiki Waingereza ngoja Muingereza mweupe mfano Maguire azingue halafu at The same time Martial azingue uone

Sajili zimekuwa za wazawa watupu rumours pia wazawa watupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakuhakikishia walivyo wanafiki Waingereza ngoja Muingereza mweupe mfano Maguire azingue halafu at The same time Martial azingue uone

Sajili zimekuwa za wazawa watupu rumours pia wazawa watupu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivyo ni vyombo vya habari mkuu, havina baraka ya man u ama bodi au team ya makocha. Na Vyombo vya habari vinataka kuuza hata ikiwa wanaemponda ni muingereza mwenzao as long as atauza magazeti watamponda. Refer wayne Rooney Alikuwa ni muingereza ila kapondwa sana tu.

Angalia bruno huyo, juzi juzi tumemkosa Haaland, kabla ya dirisha lililopita kufungwa kulikuwa na Dybala na mandzukic wote hao si waingereza.
 
Rashford alitoka mapema kwenye mechi ya Norwich kama pre caution (alikuwa ana feelings za maumivu)

Huyu dogo amecheza mechi nyingi sana mfulululizo, isitoshe jumapili lazima acheze kwenye game ya Liverpool, hivyo nadhani ni kama pre caution ili asije akaumia
Sure...hakuna Raahford na Pereira ambaye siku hizi amekuwa mpambanaji sana, TUTAPATA TABU SANA. Eti Martial ....


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba utupe 1st Eleven ya Man U tuangalie huenda sisi hatuwaoni wa hispain wa brazil n Wa Faransa mule ama wewe unaongerea 1st eleven ya Timu ya Taifa Ya ENGLAND
.

NoTe:Usiongee vitu bila uchunguzi COPYDAT.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…