Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Inapendeza
 
Mkuu embu nipe rejea aliposema ananunua wa bei rahisi

Wanatajwa

Pepe (Kati ya £45mil-£70mil)

Fernandes (Kati ya £60-£85mil)

Maguire (£75milion)

Sancho (£100)

Koullibaly (£75-100milion)

Daniel James (£15milion)

Conselo (£50milion)

Wan Bissaka (£40 million)

Reece (£45 million)


Hivi kusema anataka Wachezaji wenye vipaji na wenye njaa ya mafanikio tafsiri yake ni wa bei rahisi. Halafu si kila mchezaji wa bei kubwa ni mzuri, wengine ni virusi tu
 

Probably ni misinterpretation, nitaitafuta hiyo article ambayo OGS aliponda wachezaji kwenye bei na majina makubwa.

Akisema atajikita kusajili low profiled players.
 
United ni sawa na Madrid, Barca, PSG sio club ya kujenga timu ni club inayohitaji mafanikio kwa njia yoyote ile
 
HII NDIYO MAANA HALISI YA KUFA KUFAANA.

Unaambiwa kufungiwa kwa Manchester City kutawapa faida Arsenal na Manchester United kucheza Uefa.

Arsenal yupo na fasi ya 5 na Man U yupo nafasi ya 6.

Arsenal watapata faida hata kama hawajashinda Europa kwa vile wapo nafasi ya 5 watasogezwa juu ili zitimie timu nne kama kawaida.

Ila Man U wao watategemea matokeo ya Arsenal washinde Europa Arsenal wakibeba kombe la Europa watakuwa wame fudhu kupitia Europa ndipo Man U watachukuliwa kuziba nafasi ya Man City ili zitimie timu 5.

Kama Arsenal wasipochukua kombe la Europa itakua faida kwa Arsenal tu na Man U itakula kwao.

Hapo nawaona siku hiyo wale mashabiki wote wa Man U waliopanga kuishangilia Chelsea wataamia kuishangilia Arsenal sasa...
 
Tatizo linaanzia hapo kwa viungo kwani wakina scholes hawakuwa waingereza? Siku wakiwa na mechi mbaya basi ni kukaba na kublok mipira kitu ambacho pogba hawez yeye lazima azungukwe tu kila siku tunajenga timu kumu unlock pogba hahaha

Brother umepotea kitambo sana! Nilizani umebadili ID

Tulikuwa na 'Ole's at the wheel' ha ha ha
 
Mapacha wa Tatu wa Mr.Nice Guy.


Jose Moja ya kocha ambaye sjawahi kuwa muumini wa Soka lake(Soka la Uoga),Japo naheshimu Mafanikio yake dimbani.

Juzi alivyokuwa akihojiwa aliongea jambo la Msingi sana Ukiwa Ukiwa Mr nice guy sahau kapata mafaniko makubwa dimbani,kama ukiweza kuweka walau uwiano sawa Mr nice guy vs Ruthless(devil May care )itafaaa zaiidi.

A Ruthless SAF hakuwa na utani kidogo,siku Moja aliwahi kuulizwa na shabiki wa Man U,
Mbona sjawahi ona tabasamu lako Uwanjani..?
SAF akajibu sipo hapa kutoa tabasamu,Tabasamu utapewa na mkewe...nipo hapa kutoa burudani na kupata Ushindi.

Wakina Mr nice guy Giggs watapa wakati mgumu kupata mafanikio makubwa dimbani.

Mr nice guy Mwinyi,Bwana Mashirika a.k.a Nyerere alimwambia wewe bwana ni Mwema sana,Mtu safi lakini kama kiongozi wewe ni dhaifu.
(Uongozi na Hatima yetu by Nyerere ).

Sosha anauthubutu kuwaondoa wachezaji Mizigo,wavivu,Uwezo mdogo Uwanjani kama alivyowahi kutamba na kauli zake...?

Au ni bwana asiyeweza kusimamia maneno yake...?

Nani top six Epl aweza kutoa mkataba miaka Mitatu kwa Jones Plus £120K....? mechi tano yupo gereji... (Labda bodi ya Man u wanamijihela tele)

Sosha aweza kufanya mabadiliko makubwa na kutuvusha mbali au twajivika Upofu wa Imani..

Nyota njema itaonekana Majira ya joto,Pamoja na madhaifu ya Uendeshwaji wa club(Glazzer & Ed)kocha lazima uwajibike kwa kazi yako..Japo Jose Ni kocha asiyependa kuwajibika anahamisha lawama kama aina ya viongozi wengi wa Africa.

Karata kubwa ya sosha iliyobakia ni Ulenged wa Man United Fc (Uvumilivu wa Mashabiki).

Inasemekana Jose alitaka kuwaondoa mizigo na wavivu wote ndani ya timu msimu wa pili,ghafla akiitwa na bwana Mapesa (Bank teller)Ed Woodward,

Ed akasema wewe bwana shida yako nini..? si ni pesa..? chukua fedha hii hapa,Hao uwaitao mizigo ni asset,Mishahara tunagharamia sisi.

Mchezaji anaweza kukaaa man u miaka mitatu hachezi lakini kalidhika anakula posho,anajimwayamwaya katika Jacuzzi wala hana hata presha...mfano Darmian.

Sosha anamlima Mrefu sana,kama atatangulizi Ujasiri ,Umafia akiongozwa na falsafa yake ya soka (Hata sjui huyu bwana kama kweli anafalsafa ya soka) ndio vitamvusha,la sivyo kichwa chake kabla ya mwana wa adamu kuzaliwa huko Bethlehem kitatolewa sadaka ya Kuteketezwa.
 
Ed ameahidi mpunga wa kutosha kusajili, embu tusubiri tuone View attachment 1099426
After turbulent season

Signed Alexis for 500+k a week
Phil Jones,Chris smalling and Ashley young contract extensions
Sack managers
Director of football is uncertainty up to now
And last thing 3 yrs ago he said in the transfer window we can do things in the transfer market other clubs can only dream about

Worse enough appointment of director of football and priority for good players this window is absolutely ridiculous..bulls***
 
Nilichogundua we ni haters wa Mourinho, hapa ninajadili na mtu mweny chuki na mtu fulani, Et Mou ni kocha mwenye uwezo mdogo, kocha yupo kwenye top five ya makocha bora af unamwita vitu vya kipuuzi......we vip, kwanza ukitaja jina la Jose lazima utaje jina la Guardiola mana ndo the only one anayemyumbisha jamaa, uwanjan na kwenye mataj, tuchukulie Guardiola asingekuwepo Man city, EPL last season angechukua nani? Pochetno???..

Wakat Jose anafukuzwa kazi wote tulimunyoshea kdole kwamba tatizo ni yeye, ila sa hv nan anamnuoshea kidole jamaa, wengi sa hv wameturn back kuinyoshea kidole board na players, ni kweli watu wengi tuna dislike mbinu zake uwanjani, lakn tatzo la man u ni zaid ya Jose na hili yeye alilisema waz,....Ko kumbe tatzo la Man u sio mbinu za kocha tuu ni accumulation of problems...

Pote inajulikana kuwa ukimwajir Mou timu yako itakuwa ya kupak basi, sasa kwa nin usimpe support ya kutosha atimize malengo yake badala yake unaanza kumnanga ili afeli umfukuze kazi, Na ulimwajir ukijua hilo, huo si ni unafiki.....

Msimu wa kwanza Guardiola alisajili wachezaji wanane, na hakupata chochte zaid ya kuingia top 4, Rumours za kufukuzwa kazi zilikuwa nje nje lakn board ilimpa full support, msimu wa kwanza pesa iliyotumika ni Pound 186Mill,....Tafta ya Mou alitumia sh ngap...Mou akachukua Europa nafkli na FA

Msimu wa pili Guardiola alspend Pound 276Mill,....akachukua ndoo ya EPL, Tafta uone Mou alispend sh ngap....akaishia nafas ya pili, .....

Jose alijua kabisa mapungufu yaliyopo hvyo kuingia msimu wa tatu alihtaj kukiongezea nguvu kikosi ili kukabili kasi ya Man city na Liver....kilichofanyika tunakijua, akaonekana anafuja hela, ooh mbinu yake ya kupaki basi, kwanza kaishia nafs ya pili msimu uliopita na mengne mengi...

Guardiola akamwaga tena Pesa Pound mill 63, Sjui hata United ilitumia sh ngap....alaf mtu anademand matokeo mazur uwanjani how comes? unaweza kufight na best managers kama Klopp na Guardiola wenye kila aina ya silaha wanayotaka, huku ww silaha unazozitak hupati, unaletewa Pogba na Sanchez, et lengo wanakuforce ubadili mbinu ucheze mpira wa kuintertain mana wachezaji hao sio wa kupaki basi, et una rashford na Lingard huo si utani kabisaa...anyway mambo ni meng na mda ni mchache...

Kwa misimu miwili tu Guardiola alitumia zaid ya pound mill 525,....
Mou amespend pound 390 Mill in total....

Wewe ni mcheza FOREX mzuri sana, na njia hyo ya kujipatia kipato imekufikisha hapo ulipo japo wengine wanakudharau kwa kusema FOREX ni utapeli. ko usimdharau Mou kwa style yake ya kupaki basi, ndo ilipomfikisha hapo alipo, na akienda timu yyte lazima aondoke na vikombe, sa unaanzaje kumwita kocha kama huyo uwezo mdogo.... Jamaa ana mapungufu yake ndio, ila sio kumshusha hadhi kias hcho aisee....
 
Jose ameongea mambo mengi sana ambayo sasa hivi watu wameanza kuyaamini
 
Ole kwangu mm sio kocha bora na nadhani timu yetu itamshinda kama haiijamshinda bado.

Ole hana plan uwanjani hajui timu inacheza vipi watu wanacheza tu uwanjani ovyoovyo kama vile hawajawai kucheza pamoja. Hana tactic yoyote uwanjani jamaa anaonekana kabisa hana experience yoyote. Klop anatumia high press..na fast buildup kwenye kushambulia..pep anatumia constant pressure kwenye kukaba na high possiesion kwenye attack..nk nk nk. Ukija kwa kocha wetu ole haijulikani anacheza mfumo upi yupoyupo tu anategemea miujiza na vibe la wachezaji kushinda.


Pili jamaa yuko poor sana kuselect wachezaji wa kuanza mechi na nadhani ana ubaguzi flani kweye kuselect first eleven kuna kipind unaona kabisa lingard anazingua lakini kila siku utamuona ndani anacheza kila saa anamweka nje mtu kama lukaku amabae anainekana kabisa anapambana anapanga watu wasiojituma kina rashford(yaan huyu dogo kocha hawez kumkanya kabisa..dogo anajiona ronaldo sijui ni mchoyo balaa anataka kupiga kila saa anakaa na mpira mpaka anapoteza analalamika mno uwanajani kuna mda mpaka anazira mpira aisipopewa faulu. Kocha mzuri angeshamnyoosha dogo toka kitambo) kila siku tunaona tabia ni ileile haibadiliki ata

Tatu jamaa anazingua kwenye kuongeza mikataba ya wachezaji. Yaaani ni uingereza tu umemjaa waingereza wabovu wanapewa mikataba mizuri na kuongezewa mpunga na bado wapambanaji wakina herera wanaachwa kusepa kisa kuongezewa pesa tu kidogo.
Yaan anaonesha ubaguz wa wazi kabisa unamuongezea mshahara martial asiejituma herera akiomba kumuongezea pesa unagoma??? Daah

Nne jamaa kwenye sub ni mbovu sana yaan unaona timu inazingua toka mda tu yeye katulia tu anasubir sijui mpak dakika ya 70 au mpaka mpigwe goli ndo anajifanya kushtuka na kufanya sub zake mbovu fasta. Unakuta lukaku ndo kacheza vizuri anamtoa anamwacha rashford aliekuwa anacheza fyongo. Rashford kacheza fyongo sana na jamaa alikuwa hamtoi hata iweje naona juzi ndo kaanza kumpiga sub dogo

Mwisho jamaa anaonekana kabisa sio mkali kwa wachwzaji na kuna wwachezaji anawaogopa mfano pogba..jamaa anawez zingua mechi anapoteza pasi hakab nk ila atampiga sub fred anaecheza vizuri. Huu upendeleo wa wazi ndio unaopunguza morali ya timu.Tatizo la kuchukua nakocha wadogo ndio hili kocha hawez kumwambia chochote star wa timu unadhani ole anaweza kumkaripia pogba au martial wakabe?? Ndio maana timu letu linacheza kivivu tu

Hao kina mourinho pep na fergie ni wakali ndio maaana wanamafanikio na timu zao huyu kocha wetu mselamsela sidhan kama ataweza irudisha timu kuwa bingwa tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…