Tuiangalie mechi yetu ya kesho, tuachane na hao Chelsix;
Tukianza na PSG kesho nakiona kikosi kikianza kama ifuatavyo;
Buffon
Kehler Kimpembe Silva Bernat
Paredes Marquinhos Veratti
Di Maria Mbappe Draxler
>Kehler anaweza kuanza kwa sababu Meunier ni majeruhi, na huyu Mjerumani Kehler anaonekana anaweza kuwa mbadala mzuri.
>Marquinhos naona akimuweka benchi Dani Alves kesho kwa sababu alicheza vizuri kwenye mechi zote za Liverpool vs PSG kwahiyo sioni nafasi ya Alves hapo kesho.
>Adrien Rabiot nasikia hata kwenye kikosi kinachokuja hatokuepo kwa sababu hataki kuongeza mkataba anataka kusepa.
>Tutarajie kumuona Paredes kesho akianza au akitokea benchi.
>Kesho Mbappe atakaa pale mbele aliaweze kuwapa tabu mabeki wetu kwasababu ndio mtu pekee aliyebaki wa kuogopwa kwasababu ya mbio zake
kama kweli Cavani hatokuepo.
>Julian Draxler na Angel Di Maria ndio watakao tuletea tabu maeneo ya pembeni kama watafanikiwa kupadhibiti na kumpitishia mipira Yule kiberenge Kylian Mbappe Lotin.
>Kama kocha anaroho ngumu sana basi atamuanzisha Di Maria kushoto, Mbappe kulia na pale mbele atakaa Choupo Moting.
Kwa upande wetu naona kikosi kikianza kama ifuatavyo;
Rashford
Martial Pogba Lingard
Matic Hererra
Shaw Bailly Lindelof Young
De Gea
Kikosi chetu kitaanza hivyo kama wengi tunavyotarajia.
>Rashford atakuepo kwasababu anaonekana kuwa kwenye wakati mzuri kuliko Lukaku.
>Martial atamuweka nje Sanchez, kwahiyo Sanchez ataweza kutokea benchi kulingana hali ya mchezo itakavyokuwa.
>Matic na Hererra shughuli yao inajulikana.
>Bailly atamuweka nje Jones kwasababu Bailly anaweza kukimbizana na Yule kiberenge wao pale mbele, ingawa kama atazidiwa tutarajie kuona akipata kadi nyekundu kwasababu Bailly akilizake huwa anazijua yeye tu.
>Kimsingi mpaka sasa mechi iko upande wetu kabisa labda tushindwe wenyewe tu, maana kama angekuepo Neymar, Cavani na Meunier basi kazi ingekuwa ni kubwa zaidi, ndio maana hata kwa ale tunaobeti tunaona kabisa odds za Man U zimeshuka sana mpaka 2 wakati kipindi Mou yupo odds zetu zilikuwa 5+…
(Naomba kesho tuwepo humu ndani, marafiki zetu wa Team za Alhamisi watakuja kututembelea na wengine watakuja kujifariji baada kipigo kikali walichokipata)
GGMU…GGMU..GGMU