kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,428
- 7,216
Huyu
Manara anayefanya biashara ya kuoa na kuacha anapata wapi ujasiri wa kumsema vibaya makonda. Hana uadilifu kijamii au kiroho kumsema makonda.Haji Manara ameendelea kumnanga rafiki yake wa zamani, Paul Makonda ambaye kwasasa yupo kwenye mgogoro mzito na boss wake wa sasa, Gharib Mohammed(GSM). Manara amedai watu wengi wamekimbia nchi kwasababu ya uonevu wa Paul Makonda.
Manara amemtaka Makonda kuacha kutafuta huruma mitandaoni na sasa wanaongozwa kwa utaratibu badala ya ubabe. Pia Manara amehoji nani wa kumuua Makonda zaidi ya 'Stress' na kumtaka arudi Kolomije kwani sasa hana cheo.
Mwisho Manara amemaliza kwa kusema Makonda alilazimisha kuingia chumbani kwake kwasababu choo cha public sio hadhi yake.
Anyways huyu ndugu akiondoka sehemu au hamsini zenu zikiisha hana kifua, atayasema kwa mabaya yote mliyofanya kwa siri na dhahiri, hata GSM ajiandae siku wakienda sideways. Kwa Makonda pole sana, kuna muhenga alisema cheo ni kama koti la kuazima.
Pia, soma=> Paul Makonda: Kuna makundi matano yanataka kuniua, likiwemo wanaotafuta kulipa kisasi kwa Wasaidizi wa Magufuli
=> Haji Manara: Paul Makonda ulinilaza Korokoroni, acha dunia izunguke kwenye Mhimili wake