Manabii na Mitume mko wapi kumtetea Mwamposa?

Manabii na Mitume mko wapi kumtetea Mwamposa?

Kamgomoli

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2018
Posts
1,926
Reaction score
4,110
Kwenye video ya Gwajima tuliona jinsi akina Kakobe na manabii wengineo walivyotoka hadharani kupinga, kukanusha na kumtetea Gwajima. Ni kawaida yao kuwa pamoja hata kwenye makongamano fulani fulani.

Lakini kwenye hili la Mwamposa wote wapo kimya. Hakuna cha Nabii wala mtume aliesema chochote kumtetea Mwenzao. Nadhani ni kwa sababu hili lililomkumba mwenzao limetokea hadharani and "Beyond no doubt". La Gwajima lilitokea sirini with no concrete witness japo video ilikuwa wazi kabisa.

Ni wakati muafaka sasa mtoke hadharani mzungumze chochote si ni kawaida yenu kutoa matamko kila linapotokea jambo fulani kwa mwenzenu? Hasa Gwajima, Kakobe, Mzee wa upako, Nabii Suguye tokeni tuwasikie.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapo wapi kumtetea au kumsaidia kufufua marehemu na kuponya wagonjwa,hii si ndo nafasi ya wao kufanya ambacho huwa wanatangaza kukifanya,mi nilitegemea hapa ndo nafasi yao kutenda miujiza na nguvu ambazo huwa wanasema wanazo
Kamgomoli,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tupo mkuu.
Tatizo alituangusha alipotoka "Baru /mbio".

Inaonekana hakusoma ule mstari wa yule dogo tikiko aliyekufa Kwa ajali wakati Paulo anaendesha ibada. Paulo hakukimbia alihakikisha ameweka mambo Sawa Kwanza
 
Hahahaaaaa mnaboa bana njoni huku mwenzenu maji ya shingo.
Tupo mkuu.
Tatizo alituangusha alipotoka "Baru /mbio".

Inaonekana hakusoma ule mstari wa yule dogo tikiko aliyekufa Kwa ajali wakati Paulo anaendesha ibada. Paulo hakukimbia alihakikisha ameweka mambo Sawa Kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kwanin hawa manabii na mitume wasiwe wanaenda kuwaombea wagonjwa mahospitalini???
 
Manabii wa Ufufuo na Uzima kama mnavyojinasibu, ni muda mzuri kuwafufua hao wakanyaga-mafuta.... au tungojee siku ya tatu..?
 
huu msalaba wa mwamposa nimkubwa sana ..umeumiza hisia za,watu wengi..acha avune alichokipanda

ijapokuwa hao wachungaji wote ni matapeli
 
IMG-20191203-WA0000.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom