Mamilioni ya Lowassa yaingia CHADEMA

Mamilioni ya Lowassa yaingia CHADEMA

edgar chacha

Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
15
Reaction score
8
Katika kile kinachoonekana kujihakikishia Urais 2015 aliyewahi kuwa waziri mkuu (sio waziri mkuu mstaafu kwani uwaziri sio nafasi ya kuajiriwa na kisha kustaafu) ndugu Lowasa ameanza ama anaendeleza kazi ya kuwamgia mamilioni viongoz wakuu wa chadema katika kumsafishia njia.

Najua suala hili litashtusha wengi lakini ndio uhalisia kwani tangia mwaka 2010 viongozi wa kitaifa wa CHADEMA wamebakia kuwaandama viongozi wengine wa CCM huku wakifumbia madudu na uchafu anaoendelea kuufanya Lowasa kama kwamba hawaoni hadi hatua ya wanachama na wapenzi kuanza kuhoji kwanini Lowassa hazungumziwi? Ambapo majibu rahisi na yasiyo na mshiko kutoka kwa viongozi wa chama ni kwamba Lowassa kwa kuwa atapishwa na CCM mwaka 2015 kugombea urais sio sawa kumzungumzia kwa sasa kwani kutampa mwanya wa kujisafisha katika kashfa zake na hivo kukosa hoja za kumchafua kwa wananchi kama ilivyo kawaida ya siasa za Tanzania ili upendwe unatengeza fitina mwenzio achukiwe.

Ukweli ni kwamba Lowassa amekuwa akiwapa mamilioni viongozi hao ili kuwadhoofisha wapinzani wake na hatimaye kujihakikishia kupitishwa na chama chake kugombea urais.

Lowassa na Zitto Kabwe

Kuna taarifa za chinichini kuwa kufukuzwa kwa Zitto Kabwe pia kuna mkono wa Lowassa amabaye ni mmoja wa vigogo walioficha pesa nje na hivyo kama njia ya kudhoofisha mjadala wa pesa hizo kurudishwa ni kumuudhofisha mtoa mada na hivyo Lowassa alimwaga pesa zilizotumika kushawishi wajumbe wa kamati kuu ya CHADEMA kumuondoa Zitto na kufanikisha mikutano nchi nzima ya kuweka upepo sawa kujinusuru na kifo cha mpasuko wa chama.

CHADEMA WAANZA KUMPIGIA KAMPENI LOWASA.

Hivi karibuni licha ya kutokuzungumzia rushwa za kutisha ambazo lowasa anazitoa, viongozi wa CHADEMA wameanza kumpigia debe kiaina Lowassa kwa kuueleza umma kwamba anachotoa Lowassa ni misaada na isiwafanye wamuunge mkono. Chadema wanasema wananchi wamuunge mkono Lowassa kama ataamua kugombea kupitia chama kingine ambacho si CCM na kwa maana hii Chadema wako tayari kumpokea mtu huyu ambaye miaka mitatu minne iliyopita walimandama kwa kumwita FISADI wa Richmond na mengine mengi. Ama kweli PESA SABUNI YA ROHO!!!!!!

Katika operesheni ya chadema ya sasa Lowassa ananadiwa LIVE na ukitaka ushahidi wa wazi rejea gazeti la leo la mwananchi 24/01/2014 "CHADEMA: BODABODA ACHANENI NA LOWASSA" Ambapo chadema kinadai "MUNAWEZA KUMUUNGA MKONO KAMA AKIACHANA NA CCM NA KUAMUA KWENDA CHAMA KINGINE".

Hakuna kama pesa, hakuna kama rushwa, tuna safari ndefu sana kupata upinzani wa kweli na kupata viongozi sahihi.

Ninachojiuliza ni Haya mamilioni yanayopelekwa chadema na sehemu nyingine yatarudishwaje? Na hizi hasira na usongo wa uraisi anaoukimbilia Lowassa akipita nini kitajiri?
 
Sasa tunaanza kutilia shaka! ni kwanini nyie nyie CCM mnamchukia mwanachama mwenzenu kwa kigezo cha ufisadi ilihali ufisadi bado unaendelezwa na viongozi wa CCM lakini hamuwasemei hao? NI KWANINI LOWASSA TU? AU NDIO WOGA NA HOFU JUU YA HUYU JAMAA HUENDA AKIWA RAIS HAMNA RANGI MTAACHA KUONA?
 
Propaganda zingine bwana! Kwa hiyo hata Mgeja na Msindai wako CHADEMA?
 
Naona mmeshakubali kuwa Lowassa amewashinda na b7 zenu.... Poleni sana. Kama chama mmeshindwa kumuwajibisha sasa mmbaki kulia lia tu. Chezea Lowasa weye.
 
View attachment 134227

Muulize huyu(NAPE) na hii operation yake ya Kuvua Magamba iliishia wapi? na je wale MAPACHA WATATU aliokuwa akiwasema wako wapi?
 
Mh lowasa anakubalika sana Tanzania nzima,mimi nipo chadema licha ya kwamba kuna viongozi wazuri kama dr slaa LAKINI Mh Lowasa ni kiongozi mzuri zaidi na zaidi,KUMBUKA mwanzoni mwa miaka2006 hadi 2007 kasi aliokuwa nayo mh lowasa ya maendeleo leo tungekuwa wapi,.....? jibu ni mbali sana naamini hata mh rais anajua hilo kuwa mh lowasa ni mchapakazi sana,alikuwa akisimama kuongea watu wote kimya jamaa alikuwa ni mtu wa maamzi maguni binafsi sijaona kama lowasa badooooo!
 
kazi ya kuanika kashfa za watu c ya chadema tu.hata ww kama una kashfa za ufisad za lowasa kusanya watu wahubirie na mitandaon ulete.
 
Mawaziri mizigo yamewashinda mnazua mambo Jk ndio mzigo namba 1 hapa Tanzania
 
Nashitushwa sana na watu wanao amin kua kowasa anaweza kuongoza taifa hili ki ukweli watanzania ni wanafik sana yule mtu sio wa kumpa dhaman ile kubwa tena tumuchae aende chadema ambayo imaenza kufa huko lowasa ndo atapotelea kabisa
 
hakuna cha lowasa wala slaa 2015 ni mda wa vijana. Tutamtupia makamba j magogoni nyi angaiken na vikongwe tu
 
Mh lowasa anakubalika sana Tanzania nzima,mimi nipo chadema licha ya kwamba kuna viongozi wazuri kama dr slaa LAKINI Mh Lowasa ni kiongozi mzuri zaidi na zaidi,KUMBUKA mwanzoni mwa miaka2006 hadi 2007 kasi aliokuwa nayo mh lowasa ya maendeleo leo tungekuwa wapi,.....? jibu ni mbali sana naamini hata mh rais anajua hilo kuwa mh lowasa ni mchapakazi sana,alikuwa akisimama kuongea watu wote kimya jamaa alikuwa ni mtu wa maamzi maguni binafsi sijaona kama lowasa badooooo!

Kama hujaona kaulize Bumbuli na Uvccm ndo utajua mda wa wazee kwa heri kitu MAkamba ww!
 
Dogo kaingia Jukwaani kwa gia spesheli ...!!! Karibu sana
 
Back
Top Bottom